1I ja, braćo, nisam mogao govoriti vama kao duhovnima, nego kao tjelesnima, kao nejačadi u Kristu.
1Ndugu, mimi sikuweza kusema nanyi kama watu mlio na huyo Roho. Nilipaswa kusema nanyi kama watu wa kidunia, kama watoto wachanga katika maisha ya Kikristo.
2Mlijekom vas napojih, ne jelom: još ne mogoste, a ni sada još ne možete
2Ilinibidi kuwalisheni kwa maziwa, na si kwa chakula kigumu, kwani hamkuwa tayari kukipokea. Hata sasa hamko tayari.
3jer još ste tjelesni. Doista, dok je među vama zavist i prepiranje, zar niste tjelesni, zar po ljudsku ne postupate?
3Maana bado mu watu wa kidunia. Je, si kweli kwamba bado uko wivu na magombano kati yenu? Mambo hayo yanaonyesha wazi kwamba ninyi bado ni watu wa kidunia, mnaishi mtindo wa kidunia.
4Jer kad jedan govori: "Ja sam Pavlov", a drugi: "Ja Apolonov", niste li odveć ljudi?
4Mmoja wenu anaposema, "Mimi ni wa Paulo", na mwingine, "Mimi ni wa Apolo", je, hiyo haionyeshi kwamba mnaishi bado kama watu wa dunia hii tu?
5Ta što je Apolon? Što je Pavao? Poslužitelji po kojima povjerovaste - kako već komu Gospodin dade.
5Apolo ni nani? na Paulo ni nani? Sisi ni watumishi tu ambao tuliwaleteeni ninyi imani. Kila mmoja wetu anafanya kazi aliyopewa na Bwana.
6Ja zasadih, Apolon zali, ali Bog dade rasti.
6Mimi nilipanda mbegu, Apolo akamwagilia maji; lakini aliyeiotesha mbegu ni Mungu.
7Tako niti je što onaj tko sadi ni onaj tko zalijeva, nego Bog koji daje rasti.
7Wa maana si yule aliyepanda mbegu, au yule aliyemwagilia maji; wa maana ni Mungu aliyeiwezesha mbegu kuota.
8Tko sadi i tko zalijeva, jedno su; a svaki će po svome trudu primiti plaću.
8Yule aliyepanda na yule aliyemwagilia maji wote ni sawa, ingawa kila mmoja atapokea tuzo lake kufuatana na jitihada yake mwenyewe.
9Jer Božji smo suradnici: Božja ste njiva, Božja građevina.
9Maana sisi ni ndugu, wafanyakazi pamoja na Mungu; na ninyi ni shamba lake; ninyi ni jengo lake.
10Po milosti Božjoj koja mi je dana ja kao mudri graditelj postavih temelj, a drugi naziđuje; ali svaki neka pazi kako naziđuje.
10Kwa msaada wa neema aliyonipa Mungu, nimefaulu, kama mwashi stadi mwenye busara, kuweka msingi ambao juu yake mtu mwingine anajenga. Basi, kila mmoja awe mwangalifu jinsi anavyojenga juu yake.
11Jer nitko ne može postaviti drugoga temelja osim onoga koji je postavljen, a taj je Isus Krist.
11Hakuna mtu awezaye kuweka msingi mwingine badala ya ule uliokwisha wekwa, yaani Yesu Kristo.
12Naziđuje li tko na ovom temelju zlatom, srebrom, dragim kamenjem, drvom, sijenom, slamom -
12Juu ya msingi huo mtu anaweza kujenga kwa dhahabu, fedha au mawe ya thamani; anaweza kutumia miti, majani au nyasi.
13svačije će djelo izići na svjetlo. Onaj će Dan pokazati jer će se u ognju očitovati. I kakvo je čije djelo, oganj će iskušati.
13Iwe iwavyo, ubora wa kazi ya kila mmoja utaonekana wakati Siku ile ya Kristo itakapoifichua. Maana, Siku hiyo itatokea na moto, na huo moto utaipima na kuonyesha ubora wake.
14Ostane li djelo, primit će plaću onaj tko ga je nazidao.
14Ikiwa alichojenga mtu juu ya huo msingi kitaustahimili huo moto, atapokea tuzo;
15Izgori li čije djelo, taj će štetovati; ipak, on će se sam spasiti, ali kao kroz oganj.
15lakini kama alichojenga kitaunguzwa, basi, atapoteza tuzo lake; lakini yeye mwenyewe ataokolewa kana kwamba ameponyoka kutoka motoni.
16Ne znate li? Hram ste Božji i Duh Božji prebiva u vama.
16Je, hamjui kwamba ninyi ni hekalu la Mungu, na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
17Ako tko upropašćuje hram Božji, upropastit će njega Bog. Jer hram je Božji svet, a to ste vi.
17Basi, mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu; maana hekalu la Mungu ni takatifu, na hekalu hilo ni ninyi wenyewe.
18Nitko neka se ne vara. Ako tko misli da je mudar među vama na ovome svijetu, neka bude lud da bude mudar.
18Msijidanganye! Mtu yeyote miongoni mwenu akijidhania mwenye hekima mtindo wa kidunia, heri awe mjinga kusudi apate kuwa na hekima ya kweli.
19Jer mudrost ovoga svijeta ludost je pred Bogom. Ta pisano je: On hvata mudre u njihovu lukavstvu.
19Maana, hekima ya kidunia ni upumbavu mbele ya Mungu. Kwani Maandiko Matakatifu yasema: "Mungu huwanasa wenye hekima katika ujanja wao."
20I opet: Gospodin poznaje namisli mudrih, one su isprazne.
20Na tena: "Bwana ajua kwamba mawazo ya wenye hekima hayafai."
21Zato neka se nitko ne hvasta ljudima jer sve je vaše.
21Basi, mtu asijivunie watu. Maana kila kitu ni chenu.
22Bio Pavao, ili Apolon, ili Kefa, bio svijet, ili život, ili smrt, ili sadašnje, ili buduće: sve je vaše,
22Paulo, Apolo na Kefa, ulimwengu, maisha na kifo; mambo ya sasa na ya baadaye, yote ni yenu.
23vi Kristovi, a Krist Božji.
23Lakini ninyi ni wa Kristo naye Kristo ni wa Mungu.