Croatian

Swahili: New Testament

1 Corinthians

9

1Nisam li ja slobodan? Nisam li apostol? Nisam li vidio Isusa, Gospodina našega? Niste li vi djelo moje u Gospodinu?
1Je, mimi si mtu huru? Je, mimi si mtume? Je, mimi sikumwona Yesu Bwana wetu? Je, ninyi si matokeo ya kazi yangu kwa ajili ya Bwana?
2Ako drugima nisam apostol, vama svakako jesam. Ta vi ste pečat mojega apostolstva u Gospodinu.
2Hata kama kwa watu wengine mimi si mtume, lakini walau kwenu ninyi mimi ni mtume. Ninyi ni uthibitisho wa mtume wangu kwa sababu ya kuungana kwenu na Bwana.
3Moj odgovor mojim tužiteljima jest ovo:
3Hoja yangu kwa wale wanaonipinga ndiyo hii:
4Zar nemamo prava jesti i piti?
4Je, hatuna haki ya kula na kunywa?
5Zar nemamo prava ženu vjernicu voditi sa sobom kao i drugi apostoli i braća Gospodnja i Kefa?
5Je, hatuna ruhusa kumchukua mke Mkristo katika ziara zetu, kama vile wafanyavyo mitume wengine, ndugu zake Bwana, na pia Kefa?
6Ili samo ja i Barnaba nemamo prava ne raditi?
6Au ni mimi tu na Barnaba ambao tunapaswa kujipatia maslahi yetu kwa kufanya kazi?
7Tko ikada vojuje o svojem trošku? Tko sadi vinograd pa roda njegova ne jede? Ili tko pase stado pa od mlijeka stada ne jede?
7Je, mwanajeshi gani anayelipia utumishi wake jeshini? Mkulima gani asiyekula matunda ya shamba lake la mizabibu? Mchungaji gani asiyekunywa maziwa ya mifugo yake?
8Zar to govorim po ljudsku? Ne kaže li to i Zakon?
8Je, nasema mambo haya kibinadamu tu? Je, Sheria nayo haisemi hivyo?
9Jer u Mojsijevu zakonu piše: Ne zavezuj usta volu koji vrši! Zar je Bogu do volova?
9Imeandikwa katika Sheria ya Mose: "Usimfunge kinywa ng'ombe anapoliwata nafaka." Je, ndio kusema Mungu anajishughulisha na ng'ombe?
10Ne govori li on baš radi nas? Doista, radi nas je napisano, jer tko ore, u nadi treba da ore; i tko vrši, u nadi da će dobiti dio.
10Je, hakuwa anatufikiria sisi aliposema hivyo? Naam, haya yaliandikwa kwa ajili yetu; kwani yule anayelima na yule anayevuna, wote wawili wana haki ya kutumaini kupata sehemu ya mavuno.
11Ako smo mi vama sijali dobra duhovna, veliko li je nešto ako vam požanjemo tjelesna?
11Ikiwa sisi tumepanda mbegu ya kiroho kati yenu, je, ni jambo kubwa tukichuma kwenu faida ya kidunia?
12Ako drugi sudjeluju u vašim dobrima, zašto ne bismo mi mogli još većma. Ali nismo se poslužili tim pravom, nego sve teglimo da ne bismo postavili kakvu zapreku evanđelju Kristovu?
12Ikiwa wengine wanayo haki ya kutazamia hayo kutoka kwenu, je, sisi hatuna haki zaidi kuliko hao? Lakini, sisi hatukuitumia haki hiyo, Badala yake, tumestahimili kila kitu ili tusiiwekee kizuizi chochote Habari Njema ya Kristo.
13Ne znate li: koji obavljaju svetinje, od svetišta se hrane; i koji žrtveniku služe, sa žrtvenikom dijele?
13Je, hamjui kwamba wanaotumikia Hekaluni hupata chakula chao Hekaluni, na kwamba wanaotolea sadaka madhabahuni hupata sehemu ya hiyo sadaka?
14Tako je i Gospodin onima koji evanđelje navješćuju odredio od evanđelja živjeti.
14Bwana aliagiza vivyo hivyo; wahubiri wa Habari Njema wapate riziki zao kutokana nayo.
15No ja se ničim od toga nisam poslužio. A i ne napisah toga da bi se tako postupilo prema meni. Radije umrijeti, nego... Te mi slave nitko neće oduzeti!
15Lakini, mimi sikutumia hata mojawapo ya haki hizo. Na wala siandiki nijipatie haki hizo; kwangu mimi ni afadhali kufa kuliko kumfanya yeyote aone kwamba najisifu bure.
16Jer što navješćujem evanđelje, nije mi na hvalu, ta dužnost mi je. Doista, jao meni ako evanđelja ne navješćujem.
16Ikiwa ninaihubiri Habari Njema, hilo si jambo la kujivunia; hilo ni jukumu nililopewa. Na, ole wangu kama sitaihubiri Habari Njema!
17Jer ako to činim iz vlastite pobude, ide me plaća; ako li ne iz vlastite pobude - služba je to koja mi je povjerena.
17Ningekuwa nimeichagua kazi hii kwa hiari, basi, ningetazamia malipo; lakini maadam naifanya ikiwa ni wajibu, hiyo ina maana kwamba ni jukumu nililopewa nitekeleze.
18Koja mi je dakle plaća? Da propovijedajući pružam evanđelje besplatno ne služeći se svojim pravom u evanđelju.
18Mshahara wangu ni kitu gani, basi? Mshahara wangu ni fursa ya kuihubiri Habari Njema bure, bila kudai haki ninazostahili kwa kuihubiri.
19Jer premda slobodan od sviju, sam sebe svima učinih slugom da ih što više steknem.
19Kwa hiyo, ingawa mimi si mtumwa wa mtu yeyote, nimejifanya mtumwa wa kila mtu ili nimpatie Kristo watu wengi iwezekanavyo.
20Bijah Židovima Židov da Židove steknem; onima pod Zakonom, kao da sam pod Zakonom - premda ja nisam pod Zakonom - da one pod Zakonom steknem;
20Kwa Wayahudi nimeishi kama Myahudi ili niwapate Wayahudi; yaani, ingawa mimi siko chini ya Sheria, nimejiweka chini ya Sheria kwao, ili niwapate hao walio chini ya Sheria.
21onima bez Zakona, kao da sam bez zakona - premda nisam bez Božjega zakona, nego u Kristovu zakonu - da steknem one bez Zakona;
21Na kwa wale walio nje ya Sheria, naishi kama wao, nje ya Sheria, ili niwapate hao walio nje ya Sheria. Hii haimaanishi kwamba mimi niko nje ya sheria ya Mungu, maana nabanwa na sheria ya Kristo.
22bijah nejakima nejak da nejake steknem. Svima bijah sve da pošto-poto neke spasim.
22Kwao walio dhaifu nimejifanya dhaifu ili niwapate hao walio dhaifu. Nimejifanya kila kitu kwa wote ili nipate kuwaokoa baadhi yao kwa kila njia.
23A sve činim poradi evanđelja da bih i ja bio suzajedničar u njemu.
23Nafanya haya yote kwa ajili ya Habari Njema, nipate kushiriki baraka zake.
24Ne znate li: trkači u trkalištu svi doduše trče, ali jedan prima nagradu? Tako trčite da dobijete.
24Je, hamjui kwamba katika uwanja wa michezo, ingawa wapiga mbio wote hukimbia, ni mmoja tu anayejinyakulia zawadi?
25Svaki natjecatelj sve moguće izdržava; oni da dobiju raspadljiv vijenac, mi neraspadljiv.
25Wanariadha hujipa mazoezi na nidhamu kali; hufanya hivyo ili wajipatie taji iharibikayo! Lakini sisi twafanya hivyo tupate taji ya kudumu daima.
26Ja dakle tako trčim - ne kao besciljno, tako udaram šakom - ne kao da mlatim vjetar,
26Ndivyo basi, ninavyopiga mbio nikiwa na nia ya kushinda; ndivyo ninavyopigana, na si kama bondia anayetupa ngumi zake hewani.
27nego krotim svoje tijelo i zarobljavam da sam ne budem isključen pošto sam drugima propovijedao.
27Naupa mwili wangu mazoezi magumu na kuutia katika nidhamu kamili, nisije mimi mwenyewe nikakataliwa baada ya kuwahubiria wengine.