Croatian

Swahili: New Testament

1 Timothy

4

1Duh izričito govori da će u posljednja vremena neki otpasti od vjere i prikloniti se prijevarnim duhovima i zloduhovskim naucima.
1Roho asema waziwazi kwamba siku za baadaye watu wengine wataitupilia mbali imani; watazitii roho danganyifu na kufuata mafundisho ya pepo.
2A sve to pod utjecajem himbe lažljivaca otupjele savjesti
2Mafundisho ya namna hiyo yanaenezwa na watu waongo wadanganyifu, ambao dhamiri zao ziko kama zimechomwa kwa chuma cha moto.
3koji zabranjuju ženiti se i nameću uzdržavati se od jela što ih je Bog stvorio da ih sa zahvalnošću uzimaju oni koji vjeruju i znaju istinu.
3Watu hao hufundisha kwamba ni makosa kuona na pia kula vyakula fulani. Lakini Mungu aliviumba vyakula hivyo, ili wale walio waumini na ambao wanapata kuujua ukweli, wavitumie kwa shukrani.
4Doista, svako je Božje stvorenje dobro i ne valja odbaciti ništa što se uzima sa zahvalnošću
4Kila kitu alichoumba Mungu ni chema, wala hakuna kinachohitaji kukataliwa, bali vyote vipokelewe kwa sala ya shukrani,
5jer se posvećuje riječju Božjom i molitvom.
5kwa sababu neno la Mungu na sala hukifanya kitu hicho kikubalike kwa Mungu.
6To izlaži braći i bit ćeš dobar poslužitelj Krista Isusa, hranjen riječima vjere i dobroga nauka za kojim postojano ideš.
6Kama ukiwapa ndugu wote maagizo haya, utakuwa mtumishi mwema wa Kristo Yesu, ukijiendeleza kiroho kwa maneno ya imani na mafundisho ya kweli, ambayo wewe umeyafuata.
7Svjetovne pak i bablje priče odbijaj! Vježbaj se u pobožnosti!
7Lakini achana na hadithi zile zisizo za kidini na ambazo hazina maana. Jizoeshe kuishi maisha ya uchaji wa Mungu.
8Uistinu, tjelesno vježbanje malo čemu koristi, a pobožnost je svemu korisna jer joj je obećan život - sadašnji i budući.
8Mazoezi ya mwili yana faida yake, lakini mazoezi ya kiroho yana faida za kila namna, maana yanatuahidia uzima katika maisha ya sasa, na pia hayo yanayokuja.
9Vjerodostojna je to riječ i vrijedna da se posve prihvati.
9Usemi huo ni wa kusadikika kabisa na unastahili kukubaliwa.
10Ta za to se trudimo i borimo jer se pouzdajemo u Boga živoga koji je Spasitelj svih ljudi, ponajpače vjernika.
10Sisi tunajitahidi na kufanya kazi kwa bidii kwani tumemwekea tumaini letu Mungu aliye hai ambaye ni Mwokozi wa watu wote, na hasa wale wanaoamini.
11Zapovijedaj to i naučavaj!
11Wape maagizo hayo na mafundisho hayo.
12Nitko neka ne prezire tvoje mladosti, nego budi uzor vjernicima u riječi, u vladanju, u ljubavi, u vjeri, u čistoći.
12Usikubali mtu yeyote akudharau kwa sababu wewe ni kijana, lakini jitahidi uwe mfano kwa wanaoamini: katika usemi wako, mwenendo wako, upendo, imani na maisha safi.
13Dok ne dođem, posveti se čitanju, poticanju, poučavanju.
13Tumia wakati wako na juhudi yako katika kusoma hadharani Maandiko Matakatifu, kuhubiri na kufundisha, mpaka nitakapokuja.
14Ne zanemari milosnog dara koji je u tebi, koji ti je dan po proroštvu zajedno s polaganjem ruku starješinstva.
14Usiache kukitumia kile kipaji cha Kristo ndani yako ulichopewa kwa maneno ya manabii na kwa kuwekewa mikono na wazee.
15Oko toga nastoj, sav u tom budi da tvoj napredak bude svima očit.
15Fikiri kwa makini juu ya hayo yote na kuyatekeleza kusudi maendeleo yako yaonekane na wote.
16Pripazi na samog sebe i na poučavanje! Ustraj u tome! Jer to vršeći, spasit ćeš i sebe i one koji te slušaju.
16Angalia sana mambo yako mwenyewe, na mafundisho yako. Endelea kufanya hayo maana ukifanya hivyo utajiokoa mwenyewe na wale wanaokusikiliza.