1Odlučih dakle u sebi da neću k vama opet sa žalošću.
1Basi nimeamua nisiwatembelee tena kuwatia huzuni.
2Jer ako ja vas ražalostim, a tko će mene obradovati ako ne onaj koga ja žalostim?
2Maana nikiwahuzunisha ninyi, basi, ni nani atakayenifariji? Ni walewale niliowahuzunisha!
3Zato vam to i napisah da me, kada dođem, ne ražaloste oni koji bi mi imali biti na radost. Uzdam se doista u sve vas, da je moja radost - radost svih vas.
3Ndiyo maana niliwaandikia--sikutaka kuja kwenu na kuhuzunishwa na ninyi ambao ndio mngepaswa kuwa furaha yangu. Nina hakika kwamba, mimi nikifurahi, ninyi nyote pia mnafurahi.
4Pisah vam uistinu uz mnoge suze, iz velike nevolje i tjeskobe srca, ne da se ražalostite, nego da upoznate moju preveliku ljubav prema vama.
4Nilipowaandikia hapo awali katika hali ya huzuni na sikitiko moyoni na kwa machozi mengi, haikuwa kwa ajili ya kuwahuzunisha ninyi, bali kwa ajili ya kuwaonyesheni kwamba nawapenda mno.
5Ako me tko ražalostio, nije ražalostio mene, nego u neku ruku - da ne pretjeram - sve vas.
5Ikiwa kuna mtu aliyemhuzunisha mwingine, hakunihuzunisha mimi--ila amewahuzunisha ninyi nyote, na sipendi kuwa mkali zaidi.
6Dosta je takvu ona kazna od većine
6Adhabu aliyokwisha pata kutoka kwa wengi wenu inamtosha.
7pa ga vi radije pomilujte i utješite da ga pretjerana žalost ne shrva.
7Iliyobakia ni afadhali kwenu kumsamehe mtu huyo na kumpa moyo ili asije akahuzunika mno na kukata tamaa kabisa.
8Zato vas molim, iskažite mu ljubav.
8Kwa hiyo nawasihi: mwonyesheni kwamba mnampenda.
9Ta zato vam i pisah da vidim jeste li prokušani, jeste li u svemu poslušni.
9Madhumuni yangu kuandika ile barua yalikuwa kutaka kujua kama mko tayari kutii katika kila jambo.
10Komu dakle vi što oprostite, tomu i ja; jer i ja, ako kome što oprostih, oprostih poradi vas - pred Kristom,
10Mkimsamehe mtu, nami pia ninamsamehe. Maana ninaposamehe--kama kweli ninacho cha kusamehe--nasamehe mbele ya Kristo kwa ajili yenu,
11da nas ne nadmudri Sotona. Ta znamo njegove namjere!
11ili tusimpe nafasi Shetani atudanganye; maana twaijua mipango yake ilivyo.
12Kada dođoh u Troadu poradi evanđelja Kristova, premda mi se otvoriše vrata u Gospodinu,
12Nilipofika Troa kuhubiri Habari Njema ya Kristo, nilikuta mlango u wazi kwa ajili ya kazi ya Bwana.
13ne bijaše mi duši spokoja što ne nađoh Tita, brata svoga; oprostih se stoga s njima i pođoh u Makedoniju.
13Lakini nilifadhaika sana kwa kutomkuta ndugu yetu Tito. Ndiyo maana niliwaaga wote pale nikaenda Makedonia.
14Ali hvala Bogu koji nas u Kristu uvijek proslavlja te širi po nama na svakome mjestu miris svoga spoznanja.
14Lakini, shukrani kwa Mungu anayetuongoza daima katika msafara wa ushindi wa Kristo. Yeye hutufanya tuueneze ukweli wa Kristo kama harufu nzuri, kila mahali.
15Da, Kristov smo miomiris Bogu i među onima koji se spasavaju i među onima koji propadaju:
15Maana sisi ni kama harufu nzuri ya ubani ambayo Kristo anamtolea Mungu, harufu nzuri inayofikia wote wanaookolewa na wanaopotea.
16ovima miris iz smrti za smrt, onima miris iz života za život. A tko je za to podoban?
16Kwa wale wanaopotea, harufu hiyo ni kifo; lakini kwa wale wanaookolewa, harufu hiyo ni uhai. Nani basi, awezaye kushiriki katika kazi ya namna hiyo?
17Uistinu, mi nismo kao mnogi koji trguju riječju Božjom, nego iskreno - kao od Boga pred Bogom - u Kristu govorimo.
17Sisi si kama wengine ambao hufanya biashara na ujumbe wa Mungu; sisi tunahubiri kwa unyofu mbele ya Mungu, kama watu tuliotumwa na Mungu, tukiwa tumeungana na Kristo.