Croatian

Swahili: New Testament

3 John

1

1Starješina ljubljenom Gaju koga ljubim u Istini.
1Mimi mzee nakuandikia wewe Gayo, rafiki yangu, ninayekupenda kweli.
2Ljubljeni! Želim ti u svemu dobro i da budeš zdrav, kao što je dobro tvojoj duši.
2Mpenzi wangu, nakutakia mafanikio mema ya kila aina; nakutakia afya njema ya mwili kama ulivyo nayo rohoni.
3Veoma se obradovah kada dođoše braća i posvjedočiše za tvoju istinu: kako ti živiš po Istini.
3Nimefurahi sana ndugu kadhaa walipofika hapa, wakaiambia juu ya uaminifu wako kuhusu ukweli; naam, wewe unaishi daima katika ukweli.
4Čuti da moja djeca po Istini žive! - nema mi veće radosti od toga.
4Hakuna kitu kinachonifurahisha zaidi kuliko kusikia kwamba watoto wangu wanaishi katika ukweli.
5Ljubljeni, pravi si vjernik u svemu što činiš za braću, i to za došljake.
5Mpenzi wangu, wewe ni mwaminifu kila mara unapowahudumia ndugu, hata kama ni wageni.
6Oni posvjedočiše tvoju ljubav pred Crkvom i dobro ćeš učiniti ako ih ispratiš Boga dostojno.
6Ndugu hao wamelieleza kanisa hapa habari za upendo wako. Tafadhali uwasaidie waendelee na safari yao kwa namna itakayompendeza Mungu,
7Jer poradi Imena iziđoše i ne primaju ništa od pogana.
7Maana wanaanza safari yao katika utumishi wa Kristo bila kupokea msaada wowote kutoka kwa watu wasioamini.
8Mi smo dakle dužni takve primati da budemo suradnici Istine.
8Basi, sisi tunapaswa kuwasaidia watu hawa, ili nasi tupate kushiriki katika kazi yao kwa ajili ya ukweli.
9Pisao sam nešto Crkvi: ali Diotref, koji hoće da bude prvi među njima, ne prima nas.
9Niliandika barua fupi kwa hilo kanisa; lakini Diotrefe, ambaye hupenda kuwa kiongozi wao, hataki kabisa kunisikiliza.
10Zato ako dođem, spočitnut ću mu djela koja čini naklapajući zlobne riječi o nama. Ni to mu nije dosta, nego ne prima braće, a onima koji bi to htjeli, brani i izgoni ih iz Crkve.
10Basi, nitakapokuja nitayafichua mambo yote anayofanya, maneno mabaya anayotutolea na uongo anaosema juu yetu. Isitoshe, yeye hukataa kuwakaribisha hao ndugu walio safarini, na hata huwazuia watu wengine wanaotaka kuwakaribisha, na hujaribu kuwafukuzia nje ya kanisa.
11Ljubljeni! Ne nasljeduj zlo, nego dobro. Tko dobro čini, od Boga je; tko zlo čini, nije vidio Boga.
11Mpenzi wangu, usifuate mfano mbaya, bali mfano mwema. Kila atendaye mema ni wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hajapata kumwona Mungu.
12Za Demetrija svjedoče svi, i sama Istina, a i mi svjedočimo. A znaš da je naše svjedočanstvo istinito.
12Kila mtu anamsifu Demetrio; naam, ukweli wenyewe unamsifu. Nasi pia tunatoa ushahidi wetu juu yake, nawe wajua kwamba tunachosema ni kweli.
13Mnogo bih ti imao pisati, ali neću da ti pišem crnilom i perom.
13Ninayo bado mengi ya kukwambia, lakini sipendi kuyaandika kwa kalamu na wino.
14Nadam se da ću te uskoro vidjeti pa ćemo iz usta u usta govoriti.
14Natumaini kukuona karibuni na hapo tutazungumza ana kwa ana. (G1-15) Nakutakia amani. Rafiki zako wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu wote kila mmoja binafsi.
15Mir tebi! Pozdravljaju te prijatelji. Pozdravi prijatelje poimence.