1Htio bih uistinu da znate koliko mi se boriti za vas, za one u Laodiceji i za sve koji me nisu vidjeli licem u lice:
1Napenda mjue jinsi ninavyofanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu, kwa ajili ya watu wa Laodikea na kwa ajili ya wote ambao hawajapata kuniona kwa macho.
2da se ohrabre srca njihova, povezana u ljubavi, te se vinu do svega bogatstva, punine shvaćanja, do spoznanja otajstva Božjega - Krista,
2Nafanya hivi kusudi mioyo yao ifarijiwe na kuvutwa pamoja katika upendo, ili wajazwe uthabiti mwingi uletwao na elimu ya kweli. Hapo wataijua siri ya Mungu ambayo ni Kristo mwenyewe.
3u kojem su sva bogatstva mudrosti i spoznaje skrivena.
3Ndani yake zimefichika hazina zote za hekima na elimu.
4To govorim zato da vas tko ne prevari zavodljivim riječima.
4Basi, nawaambieni, msikubali kudanganywa na mtu yeyote kwa maneno ya uongo hata kama ni ya kuvutia sana.
5Jer ako sam tijelom nenazočan, duhom sam ipak s vama: s radošću promatram vaš red i čvrstoću vaše vjere u Krista.
5Maana, ingawa mimi niko mbali nanyi kwa mwili, lakini niko pamoja nanyi kwa roho, na ninafurahi kuona uthabiti kamili mnaosimama nao pamoja katika imani yenu kwa Kristo.
6Kao što primiste Krista Isusa, Gospodina, tako u njemu živite:
6Maadamu ninyi mmemkubali Kristo Yesu kuwa Bwana, basi, ishini katika muungano naye.
7ukorijenjeni i nazidani na njemu i učvršćeni vjerom kako ste poučeni, obilujte zahvaljivanjem.
7Mnapaswa kuwa na mizizi ndani yake, kujijenga juu yake na kuwa imara katika imani yenu kama mlivyofundishwa. Muwe na shukrani tele.
8Pazite da vas tko ne odvuče mudrovanjem i ispraznim zavaravanjem što se oslanja na predaju ljudsku, na "počela svijeta", a ne na Krista.
8Angalieni basi, mtu asiwapotoshe kwa udanganyifu mtupu wa hekima ya kibinadamu, ambayo chanzo chake ni mafundisho ya mapokeo ya watu na ya pepo watawala, na wala si Kristo mwenyewe!
9Jer u njemu tjelesno prebiva sva punina božanstva; te ste i vi
9Maana, ndani yake Kristo katika ubinadamu wake, umo ukamilifu wote wa Mungu,
10ispunjeni u njemu, koji je glava svakoga Vrhovništva i Vlasti.
10nanyi mmepewa uzima kamili katika kuungana naye. Yeye yuko juu ya pepo watawala wote na wakuu wote.
11U njemu ste i obrezani obrezanjem nerukotvorenim - svukoste tijelo puteno - obrezanjem Kristovim:
11Katika kuungana na Kristo ninyi mlitahiriwa, lakini si kwa tohara ifanywayo na watu, bali inayofanywa na Kristo mwenyewe, na ambayo inahusikana na kukombolewa kutoka katika utu wa dhambi.
12s njime suukopani u krštenju, u njemu ste i suuskrsli po vjeri u snagu Boga koji ga uskrisi od mrtvih.
12Maana, mlipobatizwa mlizikwa pamoja na Kristo, na katika ubatizo, mlifufuliwa pia pamoja naye kwa imani yenu katika nguvu ya Mungu ambaye alimfufua Kristo kutoka wafu.
13On i vas, koji bijaste mrtvi zbog prijestupa i neobrezanosti svoga tijela, i vas on oživi zajedno s njime. Milostivo nam je oprostio sve prijestupe,
13Wakati mmoja nanyi mlikuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kwa sababu ninyi mlikuwa watu wa mataifa mengine. Lakini Mungu amewapa ninyi uzima pamoja na Kristo. Mungu ametusamehe dhambi zetu zote;
14izbrisao zadužnicu koja propisima bijaše protiv nas, protivila nam se. Nju on ukloni pribivši je na križ.
14alifutilia mbali ile hati ya deni iliyokuwa inatukabili na masharti yake, na kuifuta kabisa kwa kuipigilia msalabani.
15Skinu Vrhovništva i Vlasti, javno to pokaza: u pobjedničkoj ih povorci s njime vodi.
15Juu ya msalaba Kristo aliwapokonya nguvu zao hao pepo watawala na wakuu; aliwafanya kuwa kitu cha fedheha hadharani kwa kuwaburuta kama mateka katika msafara wa ushindi wake.
16Neka vas dakle nitko ne sudi po jelu ili po piću, po blagdanima, mlađacima ili subotama.
16Kwa hiyo, basi, msikubali kupewa masharti na mtu yeyote kuhusu vyakula au vinywaji, siku za sherehe, sikukuu ya Mwezi mpya au Sabato.
17To je tek sjena onoga što dolazi, a zbiljnost jest - tijelo Kristovo.
17Mambo ya aina hiyo ni kivuli tu cha yale yatakayokuja; ukweli wenyewe ndiye Kristo.
18Nitko neka vas ne podcjenjuje zato što on sam uživa u "poniznosti i štovanju anđela", zadubljuje se u svoja viđenja, bezrazložno se nadima tjelesnom pameću svojom,
18Msikubali kuhukumiwa na mtu yeyote anayejitakia kuwa wa maana kwa sababu ya maono ya pekee na ambaye anasisitiza juu ya unyenyekevu wa uongo na ibada kwa malaika. Mtu wa namna hiyo amepumbazika kwa fikira danganifu za kidunia
19a ne drži se Glave, Njega od kojeg sve Tijelo, zglobovima i svezama zbrinuto i povezano, raste rastom Božjim.
19na amejitenga na Kristo aliye kichwa cha huo mwili. Chini ya uongozi wa Kristo, mwili wote unalishwa na kuunganishwa pamoja kwa viungo na mishipa yake, nao hukua kama atakavyo Mungu.
20Ako ste s Kristom umrli za počela svijeta, zašto se, kao da još u ovom svijetu živite, dajete pod propise:
20Ninyi mmekufa pamoja na Kristo na kukombolewa kutoka nguvu za pepo watawala wa ulimwengu. Kwa nini, basi, kuishi tena kama vile mngekuwa wa ulimwengu huu? Ya nini kuwekewa masharti:
21"Ne diraj, ne kušaj, ne dotiči"?
21"Msishike hiki," "Msionje kile," "Msiguse kile!"
22Sve će to uporabom propasti. Uredbe i nauci ljudski!
22Mambo hayo yote yanahusika na vitu vyenye kuharibika mara tu vinapotumiwa; hayo ni maagizo na mafundisho ya kibinadamu tu.
23Po samozvanu bogoštovlju, poniznosti i trapljenju tijela sve to doduše slovi kao mudrost, ali nema nikakve vrijednosti, samo zasićuje tijelo.
23Kweli, masharti hayo yaonekana kuwa ya hekima katika namna ya ibada ya kujitakia wenyewe, unyenyekevu wa uongo na kuutendea mwili kwa ukali; lakini kwa kweli, haifai chochote kuzuia tamaa za mwili.