1Budući da Zakon ima tek sjenu budućih dobara, a ne sam lik zbiljnosti, on uistinu žrtvama koje se - iz godine u godinu iste - neprestano prinose ne može nikada usavršiti one što pristupaju.
1Sheria ya Wayahudi si picha kamili ya mambo yale halisi: ni kivuli tu cha mema yanayokuja. Dhabihu zilezile hutolewa daima, mwaka baada ya mwaka. Sheria yawezaje, basi, kwa njia ya dhabihu hizo, kuwafanya wale wanaoabudu wawe wakamilifu?
2Ta ne bi li se prestale prinositi kad bogoslužnici, jednom očišćeni, ne bi više imali nikakve svijesti grijeha?
2Kama hao watu wanaomwabudu Mungu wangekuwa wametakaswa dhambi zao kweli, hawangejisikia tena kuwa na dhambi, na dhabihu hizo zote zingekoma.
3Ali po njima se iz godine u godinu podsjeća na grijehe.
3Lakini dhabihu hizo hufanyika kila mwaka kuwakumbusha watu dhambi zao.
4Jer krv bikova i jaraca nikako ne može odnijeti grijeha.
4Maana damu ya fahali na mbuzi haiwezi kamwe kuondoa dhambi.
5Zato On ulazeći u svijet veli: Žrtva i prinos ne mile ti se, nego si mi tijelo pripravio;
5Ndiyo maana Kristo alipokuwa anakuja ulimwenguni, alimwambia Mungu: "Hukutaka dhabihu wala sadaka, lakini umenitayarishia mwili.
6paljenice i okajnice ne sviđaju ti se.
6Sadaka za kuteketezwa au za kuondoa dhambi hazikupendezi.
7Tada rekoh: "Evo dolazim!" U svitku knjige piše za mene: "Vršiti, Bože, volju tvoju!"
7Hapo nikasema: Niko hapa ee Mungu, tayari kufanya mapenzi yako kama ilivyoandikwa juu yangu katika kitabu cha Sheria."
8Pošto gore reče: Žrtve i prinosi, paljenice i okajnice - koje se po Zakonu prinose - ne mile ti se i ne sviđaju,
8Kwanza alisema: "Hutaki, wala hupendezwi na dhabihu na sadaka, sadaka za kuteketezwa na za kuondoa dhambi." Alisema hivyo ingawa sadaka hizi zote hutolewa kufuatana na Sheria.
9veli zatim: Evo dolazim vršiti volju tvoju! Dokida prvo da uspostavi drugo.
9Kisha akasema: "Niko hapa, ee Mungu, tayari kufanya mapenzi yako." Hivyo Mungu alibatilisha dhabihu za zamani na mahali pake akaweka dhabihu nyingine moja.
10U toj smo volji posvećeni prinosom tijela Isusa Krista jednom zauvijek.
10Kwa kuwa Yesu Kristo alitimiza mapenzi ya Mungu, sisi tunatakaswa dhambi zetu kwa ile dhabihu ya mwili wake aliyotoa mara moja tu, ikatosha.
11I svaki je svećenik dan za danom u bogoslužju te učestalo prinosi iste žrtve, koje nikako ne mogu odnijeti grijeha.
11Kila kuhani Myahudi humhudumia Mungu kila siku, akitoa dhabibu zilezile mara nyingi, dhabibu ambazo haziwezi kuondoa dhambi.
12A ovaj, pošto je prinio jednu jedincatu žrtvu za grijehe, zauvijek sjede zdesna Bogu
12Lakini Kristo alitoa dhabihu moja tu kwa ajili ya dhambi, dhabihu ifaayo milele, kisha akaketi upande wa kulia wa Mungu.
13čekajući otad dok se neprijatelji ne podlože za podnožje nogama njegovim.
13Huko anangoja mpaka adui zake watakapowekwa kama kibao chini ya miguu yake.
14Jednim uistinu prinosom zasvagda usavrši posvećene.
14Basi, kwa dhabihu yake moja tu, amewafanya kuwa wakamilifu milele wale wanaotakaswa dhambi zao.
15A to nam svjedoči i Duh Sveti. Pošto je doista rekao:
15Naye Roho Mtakatifu anatupa ushahidi wake. Kwanza anasema:
16"Ovo je Savez kojim ću se svezati s njima nakon ovih dana", Gospodin govori: "Zakone ću svoje staviti u njihova srca i upisati ih u dušu njihovu.
16"Hili ndilo agano nitakalofanya nao, katika siku zijazo, asema Bwana: Nitaweka sheria zangu mioyoni mwao, na kuziandika akilini mwao."
17I grijeha se njihovih i bezakonja njihovih neću više spominjati."
17Kisha akaongeza kusema: "Sitakumbuka tena dhambi zao, wala vitendo vyao vya uhalifu."
18A gdje su grijesi oprošteni, nema više prinosa za njih.
18Basi, dhambi zikisha ondolewa, hakutakuwa na haja tena ya kutoa dhabihu za kuondoa dhambi.
19Imamo dakle, braćo, slobodan ulaz u Svetinju po krvi Isusovoj -
19Basi, ndugu, kwa damu ya Yesu tunapewa moyo thabiti wa kuingia Mahali Patakatifu.
20put nov i živ što nam ga On otvori kroz zavjesu, to jest svoje tijelo;
20Yeye ametufungulia njia mpya na yenye uzima kupitia lile pazia, yaani kwa njia ya mwili wake mwenyewe.
21imamo i Velikog svećenika nad kućom Božjom.
21Basi, tunaye kuhani maarufu aliye na mamlaka juu ya nyumba ya Mungu.
22Pristupajmo stoga s istinitim srcem u punini vjere, srdaca škropljenjem očišćenih od zle savjesti i tijela oprana čistom vodom.
22Kwa hiyo tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu na imani timilifu, kwa mioyo iliyotakaswa dhamiri mbaya, na kwa miili iliyosafishwa kwa maji safi.
23Čuvajmo nepokolebljivu vjeru nade jer je vjeran Onaj koji dade obećanje.
23Tushikilie imara tumaini lile tunalokiri, maana Mungu aliyefanya ahadi zake ni mwaminifu.
24I pazimo jedni na druge da se potičemo na ljubav i dobra djela
24Tujitahidi kushughulikiana kwa ajili ya kuongezeana bidii ya kupendana na kutenda mema.
25te ne propuštamo svojih sastanaka, kako je u nekih običaj, nego se hrabrimo, to više što više vidite da se bliži Dan.
25Tusiache ile desturi ya kukutana pamoja, kama vile wengine wanavyofanya. Bali tunapaswa kusaidiana kwani, kama mwonavyo, Siku ile ya Bwana inakaribia.
26Jer ako svojevoljno griješimo pošto primismo spoznanje istine, nema više žrtve za grijehe,
26Maana, tukiendelea kutenda dhambi makusudi baada ya kufahamu ukweli, hakuna dhabihu iwezayo kutolewa tena kwa ajili ya kuondoa dhambi.
27nego strašno isčekivanje suda i bijesa ognja što će proždrijeti protivnike.
27Linalobaki ni kungojea tu kwa hofu hukumu ya Mungu na moto mkali utakaowaangamiza wote wanaompinga.
28Je li tko prekršio Zakon Mojsijev, bez milosrđa biva pogubljen na osnovi dvojice ili trojice svjedoka.
28Mtu yeyote asiyeitii Sheria ya Mose, huuawa bila ya huruma kukiwa na ushahidi wa watu wawili au watatu.
29Zamislite koliko li će goru kaznu zavrijediti tko Sina Božjega pogazi, i nečistom smatra krv Saveza kojom je posvećen, i Duha milosti pogrdi?
29Je, mtu yule anayempuuza Mwana wa Mungu na kuidharau damu ya agano la Mungu iliyomtakasa, mtu anayemtukana Roho wa Mungu, anastahili kupata adhabu kali ya namna gani?
30Ta poznajemo Onoga koji je rekao: Moja je odmazda, ja ću je vratiti; i još: Sudit će Gospodin svome puku.
30Maana tunamfahamu yule aliyesema, "Mimi nitalipiza kisasi, mimi nitalipiza," na ambaye alisema pia, "Bwana atawahukumu watu wake."
31Strašno je upasti u ruke Boga živoga.
31Kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai ni jambo la kutisha mno!
32A spomenite se onih prvih dana kada ste, tek prosvijetljeni, izdržali veliku patničku borbu:
32Kumbukeni yaliyotokea siku zile za kwanza mlipoangaziwa mwanga wa Mungu. Ingawa siku zile mlipatwa na mateso mengi, ninyi mlistahimili.
33ovamo javno izvrgnuti porugama i nevoljama, onamo postavši zajedničari onih s kojima se tako postupalo.
33Mara nyingine mlitukanwa na kufedheheshwa hadharani; mara nyingine mlikuwa radhi kuungana na wale walioteswa namna hiyohiyo.
34I doista, sa sužnjevima ste suosjećali i s radošću prihvatili otimanje dobara znajući da imate bolji, trajan posjed.
34Mlishiriki mateso ya wafungwa, na mliponyang'anywa mali yenu mlistahimili kwa furaha, maana mlijua kwamba mnayo mali bora zaidi na ya kudumu milele.
35Ne gubite dakle pouzdanja! Pripada mu velika plaća!
35Basi, msipoteze uhodari wenu, maana utawapatieni tuzo kubwa.
36Postojanosti vam uistinu treba da biste vršeći volju Božju zadobili obećano.
36Mnahitaji kuwa na uvumilivu, ili mweze kufanya anayotaka Mungu na kupokea kile alichoahidi.
37Jer još malo, sasvim malo, i Onaj koji dolazi doći će i neće zakasniti
37Maana kama yasemavyo Maandiko: "Bado kidogo tu, na yule anayekuja, atakuja, wala hatakawia.
38A pravednik će moj od vjere živjeti, ako li pak otpadne, ne mili se on duši mojoj.
38Lakini mtu wangu aliye mwadilifu ataamini na kuishi; walakini akirudi nyuma, mimi sitapendezwa naye."
39A mi nismo od onih koji otpadaju, sebi na propast, nego od onih koji vjeruju na spas duše.
39Basi, sisi hatumo miongoni mwa wale wanaorudi nyuma na kupotea, ila sisi tunaamini na tunaokolewa.