1Nakon toga vidjeh: četiri anđela stoje na četiri kraja zemlje zadržavajući četiri vjetra zemaljska da nikakav vjetar ne puše ni zemljom ni morem nit ikojim drvećem.
1Baada ya hayo nikawaona malaika wanne wamesimama katika pembe nne za dunia wakishika pepo nne za dunia ili upepo usivume hata kidogo: wala katika nchi, wala baharini, wala kwenye miti.
2I vidjeh drugoga jednog anđela gdje uzlazi od istoka sunčeva s pečatom Boga živoga. On povika iza glasa onoj četvorici anđela kojima bi dano nauditi zemlji i moru:
2Kisha nikamwona malaika mwingine akipanda juu kutoka mashariki akiwa na mhuri wa Mungu aliye hai. Akapaaza sauti na kuwaambia hao malaika wanne waliokabidhiwa jukumu la kuiharibu nchi na bahari,
3"Ne udite ni zemlji ni moru ni drveću dok ne opečatimo sluge Boga našega na čelima!"
3"Msiharibu nchi, wala bahari, wala miti, mpaka tutakapokwisha wapiga mhuri watumishi wa Mungu wetu katika paji la uso."
4I začujem broj opečaćenih - sto četrdeset i četiri tisuće opečaćenih iz svih plemena sinova Izraelovih:
4Kisha nikasikia idadi ya hao waliopigwa mhuri: Watu mia moja arobaini na nne elfu wa makabila yote ya watu wa Israeli.
5iz plemena Judina dvanaest tisuća opečaćenih, iz plemena Rubenova dvanaest tisuća, iz plemena Gadova dvanaest tisuća,
5Kabila la Yuda walikuwa watu kumi na mbili elfu; kabila la Reubeni, kumi na mbili elfu, kabila la Gadi, kumi na mbili elfu;
6iz plemena Ašerova dvanaest tisuća, iz plemena Naftalijeva dvanest tisuća, iz plemena Manašeova dvanaest tisuća,
6Kabila la Asheri, kumi na mbili elfu; kabila la Naftali, kumi na mbili elfu; kabila la Manase, kumi na mbili elfu;
7iz plemena Šimunova dvanaest tisuća, iz plemena Levijeva dvanaest tisuća, iz plemena Jisakarova dvanaest tisuća,
7kabila la Simeoni, kumi na mbili elfu, kabila la Lawi, kumi na mbili elfu, kabila la Isakari, kumi na mbili elfu;
8iz plemena Zebulunova dvanaest tisuća, iz plemena Josipova dvanaest tisuća, iz plemena Benjaminova dvanaest tisuća opečaćenih.
8kabila la Zabuloni, kumi na mbili elfu; kabila la Yosefu, kumi na mbili elfu, na kabila la Benyamini, kumi na mbili elfu.
9Nakon toga vidjeh: eno velikoga mnoštva, što ga nitko ne mogaše izbrojiti, iz svakoga naroda, i plemena, i puka, i jezika! Stoje pred prijestoljem i pred Jaganjcem odjeveni u bijele haljine; palme im u rukama.
9Kisha nikatazama, nikaona umati mkubwa wa watu wasiohesabika: watu wa kila taifa, ukoo, jamaa na lugha. Nao walikuwa wamesimama mbele ya kiti cha enzi na mbele ya Mwanakondoo, wakiwa wamevaa mavazi meupe na kushika matawi ya mitende mikononi mwao.
10Viču iz glasa: "Spasenje Bogu našemu koji sjedi na prijestolju i Jaganjcu!"
10Wakapaaza sauti: "Ukombozi wetu watoka kwa Mungu wetu aketiye juu ya kiti cha enzi, na kutoka kwa Mwanakondoo!"
11I svi anđeli, što stajahu uokolo prijestolja i starješina i četiriju bića, padoše pred prijestoljem ničice, na svoja lica,
11Malaika wote wakasimama kukizunguka kiti cha enzi, wazee na vile viumbe hai vinne. Wakaanguka kifudifudi mbele ya kiti cha enzi, wakamwabudu Mungu,
12i pokloniše se Bogu govoreći: "Amen! Blagoslov i slava, i mudrost, i zahvalnica, i čast, i moć i snaga Bogu našemu u vijeke vjekova. Amen."
12wakisema, "Amina! Sifa, utukufu, hekima, shukrani, heshima, uwezo na nguvu viwe kwa Mungu wetu, milele na milele! Amina!"
13I jedan me od starješina upita: "Ovi odjeveni u bijele haljine, tko su i odakle dođoše?"
13Mmoja wa hao wazee akaniuliza, "Hawa waliovaa mavazi meupe ni watu gani? Na wametoka wapi?"
14Odgovorih mu: "Gospodine moj, ti to znaš." A on će mi: "Oni dođoše iz nevolje velike i oprali su haljine svoje i ubijelili ih u krvi Jaganjčevoj.
14Nami nikamjibu, "Mheshimiwa, wewe wajua!" Naye akaniambia, "Hawa ni wale waliopita salama katika ule udhalimu mkuu. Waliyaosha mavazi yao katika damu ya Mwanakondoo, yakawa meupe kabisa.
15Zato su pred prijestoljem Božjim i služe mu dan i noć u hramu njegovu, i Onaj koji sjedi na prijestolju razapet će Šator svoj nad njima.
15Ndiyo maana wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Humtumikia Mungu mchana na usiku katika Hekalu lake; naye aketiye juu ya kiti cha enzi atatandaza hema lake juu yao kuwalinda.
16Neće više gladovati ni žeđati, neće ih više paliti sunce nit ikakva žega
16Hawataona tena njaa wala kiu; jua wala joto kali halitawachoma tena,
17jer - Jaganjac koji je posred prijestolja bit će pastir njihov i vodit će ih na izvore voda života. I otrt će Bog svaku suzu s očiju njihovih."
17kwa sababu Mwanakondoo aliye katikati ya kiti cha enzi atakuwa mchungaji wao, naye atawaongoza kwenye chemchemi za maji ya uzima. Naye Mungu atayafuta machozi yote machoni mwao."