Darby's Translation

Swahili: New Testament

1 Corinthians

16

1Now concerning the collection for the saints, as I directed the assemblies of Galatia, so do *ye* do also.
1Sasa, yahusu ule mchango kwa ajili ya watu wa Mungu: fanyeni kama nilivyoyaagiza makanisa ya Galatia.
2On [the] first of [the] week let each of you put by at home, laying up [in] whatever [degree] he may have prospered, that there may be no collections when I come.
2Kila Jumapili kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha kadiri ya mapato yake, ili kusiwe na haja ya kufanya mchango wakati nitakapokuja.
3And when I am arrived, whomsoever ye shall approve, these I will send with letters to carry your bounty to Jerusalem:
3Wakati nitakapokuja kwenu, nitawatuma wale mtakaowachagua miongoni mwenu wapeleke barua na zawadi zenu Yerusalemu.
4and if it be suitable that *I* also should go, they shall go with me.
4Kama itafaa nami niende, basi, watakwenda pamoja nami.
5But I will come to you when I shall have gone through Macedonia; for I do go through Macedonia.
5Nitakuja kwenu, baada ya kupitia Makedonia--maana nataraji kupitia Makedonia.
6But perhaps I will stay with you, or even winter with you, that *ye* may set me forward wheresoever I may go.
6Labda nitakaa kwenu kwa muda fulani, au huenda nitakaa pamoja nanyi wakati wote wa baridi, ili mpate kunisaidia niendelee na safari yangu kokote nitakakokwenda.
7For I will not see you now in passing, for I hope to remain a certain time with you, if the Lord permit.
7Sipendi kupita kwenu harakaharaka na kuendelea na safari. Natumaini kukaa kwenu kwa kitambo fulani, Bwana akiniruhusu.
8But I remain in Ephesus until Pentecost.
8Lakini nitabaki hapa Efeso mpaka siku ya Pentekoste.
9For a great door is opened to me and an effectual [one], and [the] adversaries many.
9Mlango uko wazi kabisa kwa ajili ya kazi yangu muhimu hapa, ingawa wapinzani nao ni wengi.
10Now if Timotheus come, see that he may be with you without fear; for he works the work of the Lord, even as I.
10Timotheo akija, angalieni asiwe na hofu yoyote wakati yupo kati yenu, kwani anafanya kazi ya Bwana kama mimi.
11Let not therefore any one despise him; but set him forward in peace, that he may come to me; for I expect him with the brethren.
11Kwa hiyo mtu yeyote asimdharau, ila msaidieni aendelee na safari yake kwa amani ili aweze kurudi kwangu, maana mimi namngojea pamoja na ndugu zetu.
12Now concerning the brother Apollos, I begged him much that he would go to you with the brethren; but it was not at all [his] will to go now; but he will come when he shall have good opportunity.
12Kuhusu ndugu Apolo, nimemsihi sana aje kwenu pamoja na ndugu wengine, lakini hapendelei kabisa kuja sasa ila atakuja mara itakapowezekana.
13Be vigilant; stand fast in the faith; quit yourselves like men; be strong.
13Kesheni, simameni imara katika imani, muwe hodari na wenye nguvu.
14Let all things ye do be done in love.
14Kila mfanyacho kifanyike kwa upendo.
15But I beseech you, brethren, (ye know the house of Stephanas, that it is the first-fruits of Achaia, and they have devoted themselves to the saints for service,)
15Ndugu, mnaifahamu jamaa ya Stefana; wao ni watu wa kwanza kabisa kuipokea imani ya Kikristo katika Akaya, na wamejitolea kuwatumikia watu wa Mungu. Ninawasihi ninyi ndugu zangu,
16that *ye* should also be subject to such, and to every one joined in the work and labouring.
16muufuate uongozi wa watu kama hao, na uongozi wa kila mtu afanyaye kazi na kutumikia pamoja nao.
17But I rejoice in the coming of Stephanas and Fortunatus and Achaicus; because *they* have supplied what was lacking on your part.
17Nafurahi sana kwamba Stefana, Fortunato na Akaiko wamefika; wamelijaza pengo lililokuwako kwa kutokuwako kwenu.
18For they have refreshed my spirit and yours: own therefore such.
18Wameiburudisha roho yangu na yenu pia. Kwa hiyo inafaa kuwakumbuka watu wa namna hii.
19The assemblies of Asia salute you. Aquila and Priscilla, with the assembly in their house, salute you much in [the] Lord.
19Makanisa yote ya Asia yanawasalimuni. Akula na Priskila pamoja na watu wote wa Mungu walio nyumbani mwao wanawasalimuni sana katika Bwana.
20All the brethren salute you. Salute one another with a holy kiss.
20Ndugu wote wanawasalimuni. Nanyi salimianeni kwa ishara ya mapendo ya Mungu.
21The salutation of [me] Paul with my own hand.
21Mimi Paulo nawasalimuni, nikiandika kwa mkono wangu mwenyewe.
22If any one love not the Lord [Jesus Christ] let him be Anathema Maranatha.
22Yeyote asiyempenda Bwana, na alaaniwe. MARANA THA--BWANA, njoo!
23The grace of the Lord Jesus Christ [be] with you.
23Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.
24My love [be] with you all in Christ Jesus. Amen.
24Mapendo yangu yawe kwenu katika kuungana na Kristo Yesu.