Darby's Translation

Swahili: New Testament

1 Corinthians

3

1And *I*, brethren, have not been able to speak to you as to spiritual, but as to fleshly; as to babes in Christ.
1Ndugu, mimi sikuweza kusema nanyi kama watu mlio na huyo Roho. Nilipaswa kusema nanyi kama watu wa kidunia, kama watoto wachanga katika maisha ya Kikristo.
2I have given you milk to drink, not meat, for ye have not yet been able, nor indeed are ye yet able;
2Ilinibidi kuwalisheni kwa maziwa, na si kwa chakula kigumu, kwani hamkuwa tayari kukipokea. Hata sasa hamko tayari.
3for ye are yet carnal. For whereas [there are] among you emulation and strife, are ye not carnal, and walk according to man?
3Maana bado mu watu wa kidunia. Je, si kweli kwamba bado uko wivu na magombano kati yenu? Mambo hayo yanaonyesha wazi kwamba ninyi bado ni watu wa kidunia, mnaishi mtindo wa kidunia.
4For when one says, *I* am of Paul, and another, *I* of Apollos, are ye not men?
4Mmoja wenu anaposema, "Mimi ni wa Paulo", na mwingine, "Mimi ni wa Apolo", je, hiyo haionyeshi kwamba mnaishi bado kama watu wa dunia hii tu?
5Who then is Apollos, and who Paul? Ministering servants, through whom ye have believed, and as the Lord has given to each.
5Apolo ni nani? na Paulo ni nani? Sisi ni watumishi tu ambao tuliwaleteeni ninyi imani. Kila mmoja wetu anafanya kazi aliyopewa na Bwana.
6*I* have planted; Apollos watered; but God has given the increase.
6Mimi nilipanda mbegu, Apolo akamwagilia maji; lakini aliyeiotesha mbegu ni Mungu.
7So that neither the planter is anything, nor the waterer; but God the giver of the increase.
7Wa maana si yule aliyepanda mbegu, au yule aliyemwagilia maji; wa maana ni Mungu aliyeiwezesha mbegu kuota.
8But the planter and the waterer are one; but each shall receive his own reward according to his own labour.
8Yule aliyepanda na yule aliyemwagilia maji wote ni sawa, ingawa kila mmoja atapokea tuzo lake kufuatana na jitihada yake mwenyewe.
9For we are God's fellow-workmen; ye are God's husbandry, God's building.
9Maana sisi ni ndugu, wafanyakazi pamoja na Mungu; na ninyi ni shamba lake; ninyi ni jengo lake.
10According to the grace of God which has been given to me, as a wise architect, I have laid the foundation, but another builds upon it. But let each see how he builds upon it.
10Kwa msaada wa neema aliyonipa Mungu, nimefaulu, kama mwashi stadi mwenye busara, kuweka msingi ambao juu yake mtu mwingine anajenga. Basi, kila mmoja awe mwangalifu jinsi anavyojenga juu yake.
11For other foundation can no man lay besides that which [is] laid, which is Jesus Christ.
11Hakuna mtu awezaye kuweka msingi mwingine badala ya ule uliokwisha wekwa, yaani Yesu Kristo.
12Now if any one build upon [this] foundation, gold, silver, precious stones, wood, grass, straw,
12Juu ya msingi huo mtu anaweza kujenga kwa dhahabu, fedha au mawe ya thamani; anaweza kutumia miti, majani au nyasi.
13the work of each shall be made manifest; for the day shall declare [it], because it is revealed in fire; and the fire shall try the work of each what it is.
13Iwe iwavyo, ubora wa kazi ya kila mmoja utaonekana wakati Siku ile ya Kristo itakapoifichua. Maana, Siku hiyo itatokea na moto, na huo moto utaipima na kuonyesha ubora wake.
14If the work of any one which he has built upon [the foundation] shall abide, he shall receive a reward.
14Ikiwa alichojenga mtu juu ya huo msingi kitaustahimili huo moto, atapokea tuzo;
15If the work of any one shall be consumed, he shall suffer loss, but *he* shall be saved, but so as through [the] fire.
15lakini kama alichojenga kitaunguzwa, basi, atapoteza tuzo lake; lakini yeye mwenyewe ataokolewa kana kwamba ameponyoka kutoka motoni.
16Do ye not know that ye are [the] temple of God, and [that] the Spirit of God dwells in you?
16Je, hamjui kwamba ninyi ni hekalu la Mungu, na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
17If any one corrupt the temple of God, *him* shall God destroy; for the temple of God is holy, and such are *ye*.
17Basi, mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu; maana hekalu la Mungu ni takatifu, na hekalu hilo ni ninyi wenyewe.
18Let no one deceive himself: if any one thinks himself to be wise among you in this world, let him become foolish, that he may be wise.
18Msijidanganye! Mtu yeyote miongoni mwenu akijidhania mwenye hekima mtindo wa kidunia, heri awe mjinga kusudi apate kuwa na hekima ya kweli.
19For the wisdom of this world is foolishness with God; for it is written, He who takes the wise in their craftiness.
19Maana, hekima ya kidunia ni upumbavu mbele ya Mungu. Kwani Maandiko Matakatifu yasema: "Mungu huwanasa wenye hekima katika ujanja wao."
20And again, [The] Lord knows the reasonings of the wise that they are vain.
20Na tena: "Bwana ajua kwamba mawazo ya wenye hekima hayafai."
21So that let no one boast in men; for all things are yours.
21Basi, mtu asijivunie watu. Maana kila kitu ni chenu.
22Whether Paul, or Apollos, or Cephas, or [the] world, or life, or death, or things present, or things coming, all are yours;
22Paulo, Apolo na Kefa, ulimwengu, maisha na kifo; mambo ya sasa na ya baadaye, yote ni yenu.
23and *ye* [are] Christ's, and Christ [is] God's.
23Lakini ninyi ni wa Kristo naye Kristo ni wa Mungu.