Darby's Translation

Swahili: New Testament

1 Thessalonians

5

1But concerning the times and the seasons, brethren, ye have no need that ye should be written to,
1Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.
2for ye know perfectly well yourselves, that the day of [the] Lord so comes as a thief by night.
2Maana ninyi wenyewe mwajua kwamba Siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajavyo usiku.
3When they may say, Peace and safety, then sudden destruction comes upon them, as travail upon her that is with child; and they shall in no wise escape.
3Watu watakapokuwa wanasema: "Kila kitu ni shwari na salama" ndipo uharibifu utakapowaangukia ghafla! Mambo hayo yatatukia ghafla kama uchungu wa uzazi unavyomjia mama anayejifungua, wala watu hawataweza kuepukana nayo.
4But *ye*, brethren, are not in darkness, that the day should overtake you as a thief:
4Lakini ninyi ndugu, hamko gizani, na siku hiyo haipaswi kuwajieni ghafla kama vile mwizi.
5for all *ye* are sons of light and sons of day; we are not of night nor of darkness.
5Ninyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.
6So then do not let us sleep as the rest do, but let us watch and be sober;
6Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.
7for they that sleep sleep by night, and they that drink drink by night;
7Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.
8but *we* being of [the] day, let us be sober, putting on [the] breastplate of faith and love, and as helmet [the] hope of salvation;
8Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.
9because God has not set us for wrath, but for obtaining salvation through our Lord Jesus Christ,
9Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
10who has died for us, that whether we may be watching or sleep, we may live together with him.
10ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.
11Wherefore encourage one another, and build up each one the other, even as also ye do.
11Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana ninyi kwa ninyi kama mnavyofanya sasa.
12But we beg you, brethren, to know those who labour among you, and take the lead among you in [the] Lord, and admonish you,
12Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.
13and to regard them exceedingly in love on account of their work. Be in peace among yourselves.
13Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa sababu ya kazi wanayofanya. Muwe na amani kati yenu.
14But we exhort you, brethren, admonish the disorderly, comfort the faint-hearted, sustain the weak, be patient towards all.
14Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.
15See that no one render to any evil for evil, but pursue always what is good towards one another and towards all;
15Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.
16rejoice always;
16Furahini daima,
17pray unceasingly;
17salini kila wakati
18in everything give thanks, for this is [the] will of God in Christ Jesus towards you;
18na muwe na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.
19quench not the Spirit;
19Msimpinge Roho Mtakatifu;
20do not lightly esteem prophecies;
20msidharau unabii.
21but prove all things, hold fast the right;
21Pimeni kila kitu: zingatieni kilicho chema,
22hold aloof from every form of wickedness.
22na epukeni kila aina ya uovu.
23Now the God of peace himself sanctify you wholly: and your whole spirit, and soul, and body be preserved blameless at the coming of our Lord Jesus Christ.
23Mungu anayetupatia amani awafanye ninyi watakatifu kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu--roho, mioyo na miili yenu--mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
24He [is] faithful who calls you, who will also perform [it].
24Yeye anayewaita ninyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.
25Brethren, pray for us.
25Ndugu, tuombeeni na sisi pia.
26Greet all the brethren with a holy kiss.
26Wasalimuni ndugu wote kwa ishara ya upendo.
27I adjure you by the Lord that the letter be read to all the [holy] brethren.
27Nawahimizeni kwa jina la Bwana muwasomee ndugu zetu wote barua hii.
28The grace of our Lord Jesus Christ [be] with you.
28Tunawatakieni neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.