1I exhort therefore, first of all, that supplications, prayers, intercessions, thanksgivings be made for all men;
1Kwanza kabisa, basi naomba dua, sala, maombi na sala za shukrani zitolewe kwa Mungu kwa ajili ya watu wote,
2for kings and all that are in dignity, that we may lead a quiet and tranquil life in all piety and gravity;
2kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi maisha ya utulivu na amani pamoja na uchaji wa Mungu na mwenendo mwema.
3for this is good and acceptable before our Saviour God,
3Jambo hili ni jema na lampendeza Mungu Mwokozi wetu,
4who desires that all men should be saved and come to [the] knowledge of [the] truth.
4ambaye anataka watu wote waokolewe na wapate kuujua ukweli.
5For God is one, and [the] mediator of God and men one, [the] man Christ Jesus,
5Maana yuko Mungu mmoja, na pia yuko mmoja anayewapatanisha watu na Mungu, binadamu Kristo Yesu,
6who gave himself a ransom for all, the testimony [to be rendered] in its own times;
6ambaye alijitoa mwenyewe kuwakomboa watu wote. Huo ulikuwa uthibitisho, wakati ufaao ulipowadia.
7to which *I* have been appointed a herald and apostle, (I speak [the] truth, I do not lie,) a teacher of [the] nations in faith and truth.
7Kwa sababu hiyo mimi nilitumwa niwe mtume na mwalimu wa watu wa mataifa, niutangaze ujumbe wa imani na ukweli. Nasema ukweli; sisemi uongo!
8I will therefore that the men pray in every place, lifting up pious hands, without wrath or reasoning.
8Basi, popote mnapokutana kufanya ibada nataka wanaume wasali, watu waliojitolea kweli na ambao wanaweza kuinua mikono yao wakisali bila hasira wala ubishi.
9In like manner also that the women in decent deportment and dress adorn themselves with modesty and discretion, not with plaited [hair] and gold, or pearls, or costly clothing,
9Hali kadhalika, nawataka wanawake wawe wanyofu na wenye busara kuhusu mavazi yao; wavae sawasawa na si kwa urembo wa mitindo ya kusuka nywele, kujipamba kwa dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
10but, what becomes women making profession of the fear of God, by good works.
10bali kwa matendo mema kama iwapasavyo wanawake wamchao Mungu.
11Let a woman learn in quietness in all subjection;
11Wanawake wanapaswa kukaa kimya na kuwa wanyenyekevu wakati wa kujifunza.
12but I do not suffer a woman to teach nor to exercise authority over man, but to be in quietness;
12Mimi simruhusu mwanamke amfundishe au amtawale mwanamume; anapaswa kukaa kimya.
13for Adam was formed first, then Eve:
13Maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa.
14and Adam was not deceived; but the woman, having been deceived, was in transgression.
14Na wala si Adamu aliyedanganywa; bali mwanamke ndiye aliyedanganywa, akaivunja sheria ya Mungu.
15But she shall be preserved in childbearing, if they continue in faith and love and holiness with discretion.
15Hata hivyo, mwanamke ataokolewa kwa kupata watoto, kama akidumu katika imani, upendo, utakatifu na unyofu.