1But I myself, Paul, entreat you by the meekness and gentleness of the Christ, who, as to appearance, [when present] [am] mean among you, but absent am bold towards you;
1Mimi Paulo mwenyewe ambaye naonekana kuwa mpole nikiwa pamoja nanyi, lakini mkali wakati nikiwa mbali nanyi, nawasihini kwa huruma na wema wake Kristo.
2but I beseech that present I may not be bold with the confidence with which I think to be daring towards some who think of us as walking according to flesh.
2Nawaombeni msinisababishe kuwa mkali wakati nitakapokuja, maana nina hakika naweza kuwa mkali kwa wote wale wanaotudhania kwamba tunaishi kidunia.
3For walking in flesh, we do not war according to flesh.
3Kweli tunaishi duniani, lakini hatupigani vita kidunia.
4For the arms of our warfare [are] not fleshly, but powerful according to God to [the] overthrow of strongholds;
4Maana, silaha tunazotumia katika vita vyetu si silaha za kidunia, ila ni nguvu za Mungu zenye kuharibu ngome zote. Tunaharibu hoja zote za uongo,
5overthrowing reasonings and every high thing that lifts itself up against the knowledge of God, and leading captive every thought into the obedience of the Christ;
5na kubomoa kila kizuizi cha majivuno kilichowekwa kuipinga elimu ya Mungu; tunaziteka fikira zote na kuzifanya zimtii Kristo.
6and having in readiness to avenge all disobedience when your obedience shall have been fulfilled.
6Mkisha kuwa wakamilifu katika kutii, sisi tuko tayari kuadhibu kila namna ya kutotii.
7Do ye look at what concerns appearance? If any one has confidence in himself that he is of Christ, let him think this again in himself, that even as he [is] of Christ, so also [are] we.
7Ninyi hutazama mambo kwa nje tu. Je, yupo mtu yeyote anayedhani kwamba yeye ni wa Kristo? Sawa! Basi, afikirie vilevile kwamba sisi pia ni wa Kristo kama yeye alivyo wa Kristo.
8For and if I should boast even somewhat more abundantly of our authority, which the Lord has given [to us] for building up and not for your overthrowing, I shall not be put to shame;
8Hata kama nimezidi katika kujivuna kwangu juu ya ule uwezo aliotupa--uwezo wa kuwajenga na sio wa kubomoa--hata hivyo sijutii hata kidogo.
9that I may not seem as if I was frightening you by letters:
9Sipendi mfikiri kwamba nataka kuwatisha ninyi kwa barua zangu.
10because his letters, he says, [are] weighty and strong, but his presence in the body weak, and his speech naught.
10Mtu anaweza kusema: "Barua za Paulo ni kali na zenye maneno mazito, lakini yeye mwenyewe anapokuwa pamoja nasi ni mtu dhaifu, na hata anapoongea maneno yake ni kama si kitu."
11Let such a one think this, that such as we are in word by letters [when] absent, such also present in deed.
11Mtu asemaye hivyo heri akumbuke kwamba hakuna tofauti ya yale tunayoandika katika barua wakati tuko mbali, na yale tutakayofanya wakati tutakapokuwa nanyi.
12For we dare not class ourselves or compare ourselves with some who commend themselves; but these, measuring themselves by themselves, and comparing themselves with themselves, are not intelligent.
12Kwa vyovyote hatungethubutu kujiweka au kujilinganisha na wale watu wanaojisifia wenyewe. Watu wenye kujifanya wao kuwa kipimo cha kujipimia, na watu wanaojilinganisha wenyewe kwa wenyewe, ni wapumbavu.
13Now *we* will not boast out of measure, but according to the measure of the rule which the God of measure has apportioned to us, to reach to you also.
13Lakini sisi hatutajivuna kupita kiasi; kujivuna huko kutabaki katika kile kipimo cha kazi aliyotukabidhi Mungu, kazi ambayo tunaifanya pia kwenu.
14For we do not, as not reaching to you, overstretch ourselves, (for we have come to you also in the glad tidings of the Christ;)
14Na kwa vile ninyi mu katika mipaka hiyo, hatukuipita tulipokuja kwenu, tukiwaleteeni Habari Njema juu ya Kristo.
15not boasting out of measure in other people's labours, but having hope, your faith increasing, to be enlarged amongst you, according to our rule, yet more abundantly
15Basi, hatujivunii kazi waliyofanya wengine zaidi ya kipimo tulichopewa; ila tunatumaini kwamba imani yenu itazidi miongoni mwenu kufuatana na kipimo alichotuwekea Mungu.
16to announce the glad tidings to that [which is] beyond you, not to be boasting in another's rule of things made ready to hand.
16Hapo tutaweza kuihubiri Habari Njema katika nchi nyingine, mbali nanyi; na haitakuwa shauri la kujivunia kazi waliyofanya watu wengine mahali pengine.
17But he that boasts, let him boast in the Lord.
17Lakini kama yasemavyo Maandiko: "Mwenye kuona fahari na aone fahari juu ya alichofanya Bwana."
18For not *he* that commends himself is approved, but whom the Lord commends.
18Anayekubaliwa si yule anayejisifu mwenyewe, bali yule anayesifiwa na Bwana.