1But I have judged this with myself, not to come back to you in grief.
1Basi nimeamua nisiwatembelee tena kuwatia huzuni.
2For if *I* grieve you, who also [is] it that gladdens me, if not he that is grieved through me?
2Maana nikiwahuzunisha ninyi, basi, ni nani atakayenifariji? Ni walewale niliowahuzunisha!
3And I have written this very [letter] [to you], that coming I may not have grief from those from whom I ought to have joy; trusting in you all that my joy is [that] of you all.
3Ndiyo maana niliwaandikia--sikutaka kuja kwenu na kuhuzunishwa na ninyi ambao ndio mngepaswa kuwa furaha yangu. Nina hakika kwamba, mimi nikifurahi, ninyi nyote pia mnafurahi.
4For out of much tribulation and distress of heart I wrote to you, with many tears; not that ye may be grieved, but that ye may know the love which I have very abundantly towards you.
4Nilipowaandikia hapo awali katika hali ya huzuni na sikitiko moyoni na kwa machozi mengi, haikuwa kwa ajili ya kuwahuzunisha ninyi, bali kwa ajili ya kuwaonyesheni kwamba nawapenda mno.
5But if any one has grieved, he has grieved, not me, but in part (that I may not overcharge [you]) all of you.
5Ikiwa kuna mtu aliyemhuzunisha mwingine, hakunihuzunisha mimi--ila amewahuzunisha ninyi nyote, na sipendi kuwa mkali zaidi.
6Sufficient to such a one [is] this rebuke which [has been inflicted] by the many;
6Adhabu aliyokwisha pata kutoka kwa wengi wenu inamtosha.
7so that on the contrary ye should rather shew grace and encourage, lest perhaps such a one should be swallowed up with excessive grief.
7Iliyobakia ni afadhali kwenu kumsamehe mtu huyo na kumpa moyo ili asije akahuzunika mno na kukata tamaa kabisa.
8Wherefore I exhort you to assure him of [your] love.
8Kwa hiyo nawasihi: mwonyesheni kwamba mnampenda.
9For to this end also I have written, that I might know, by putting you to the test, if as to everything ye are obedient.
9Madhumuni yangu kuandika ile barua yalikuwa kutaka kujua kama mko tayari kutii katika kila jambo.
10But to whom ye forgive anything, *I* also; for I also, what I have forgiven, if I have forgiven anything, [it is] for your sakes in [the] person of Christ;
10Mkimsamehe mtu, nami pia ninamsamehe. Maana ninaposamehe--kama kweli ninacho cha kusamehe--nasamehe mbele ya Kristo kwa ajili yenu,
11that we might not have Satan get an advantage against us, for we are not ignorant of *his* thoughts.
11ili tusimpe nafasi Shetani atudanganye; maana twaijua mipango yake ilivyo.
12Now when I came to Troas for the [publication of the] glad tidings of the Christ, a door also being opened to me in [the] Lord,
12Nilipofika Troa kuhubiri Habari Njema ya Kristo, nilikuta mlango u wazi kwa ajili ya kazi ya Bwana.
13I had no rest in my spirit at not finding Titus my brother; but bidding them adieu, I came away to Macedonia.
13Lakini nilifadhaika sana kwa kutomkuta ndugu yetu Tito. Ndiyo maana niliwaaga wote pale nikaenda Makedonia.
14But thanks [be] to God, who always leads us in triumph in the Christ, and makes manifest the odour of his knowledge through us in every place.
14Lakini, shukrani kwa Mungu anayetuongoza daima katika msafara wa ushindi wa Kristo. Yeye hutufanya tuueneze ukweli wa Kristo kama harufu nzuri, kila mahali.
15For we are a sweet odour of Christ to God, in the saved and in those that perish:
15Maana sisi ni kama harufu nzuri ya ubani ambayo Kristo anamtolea Mungu, harufu nzuri inayofikia wote wanaookolewa na wanaopotea.
16to the one an odour from death unto death, but to the others an odour from life unto life; and who [is] sufficient for these things?
16Kwa wale wanaopotea, harufu hiyo ni kifo; lakini kwa wale wanaookolewa, harufu hiyo ni uhai. Nani basi, awezaye kushiriki katika kazi ya namna hiyo?
17For we do not, as the many, make a trade of the word of God; but as of sincerity, but as of God, before God, we speak in Christ.
17Sisi si kama wengine ambao hufanya biashara na ujumbe wa Mungu; sisi tunahubiri kwa unyofu mbele ya Mungu, kama watu tuliotumwa na Mungu, tukiwa tumeungana na Kristo.