1For the rest, brethren, pray for us, that the word of the Lord may run and be glorified, even as also with you;
1Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili ujumbe wa Bwana uzidi kuenea upesi na kupokelewa kwa heshima kama vile ulivyo kati yenu.
2and that we may be delivered from bad and evil men, for faith [is] not [the portion] of all.
2Ombeni pia ili Mungu atuokoe na watu wapotovu na waovu, maana si wote wanaoamini ujumbe huu.
3But the Lord is faithful, who shall establish you and keep [you] from evil.
3Lakini Bwana ni mwaminifu. Yeye atawaimarisheni na kuwalinda salama na yule Mwovu.
4But we trust in the Lord as to you, that the things which we enjoin, ye both do and will do.
4Naye Bwana anatupatia tumaini kubwa juu yenu, na hatuna shaka kwamba mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaambieni.
5But the Lord direct your hearts into the love of God, and into the patience of the Christ.
5Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika uvumilivu tunaopewa na Kristo.
6Now we enjoin you, brethren, in the name of our Lord Jesus Christ, that ye withdraw from every brother walking disorderly and not according to the instruction which he received from us.
6Ndugu, tunawaamuru kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, mjiepushe na ndugu wote walio wavivu na ambao hawafuati maagizo tuliyowapa.
7For ye know yourselves how ye ought to imitate us, because we have not walked disorderly among you;
7Ninyi wenyewe mnajua kwamba mnapaswa kufuata mfano wetu. Sisi tulipokuwa nanyi hatukuwa wavivu;
8nor have we eaten bread from any one without cost; but in toil and hardship working night and day not to be chargeable to any one of you:
8hatukula chakula kwa mtu yeyote bila ya kumlipa. Tulifanya kazi kwa bidii na taabu mchana na usiku ili tusiwe mzigo kwa mtu yeyote kati yenu.
9not that we have not the right, but that we might give ourselves as an example to you, in order to your imitating us.
9Tulifanya hivyo si kwa kuwa hatuna haki ya kutaka msaada wenu, ila kwa sababu tunataka kuwapeni mfano.
10For also when we were with you we enjoined you this, that if any man does not like to work, neither let him eat.
10Tulipokuwa pamoja nanyi tulikuwa tukiwaambieni, "Mtu asiyefanya kazi, asile."
11For we hear that [there are] some walking among you disorderly, not working at all, but busybodies.
11Tunasema mambo hayo kwa sababu tumesikia kwamba wako baadhi yenu ambao ni wavivu na ambao hawafanyi chochote, isipokuwa tu kujiingiza katika mambo ya watu wengine.
12Now such we enjoin and exhort in [the] Lord Jesus Christ, that working quietly they eat their own bread.
12Kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo tunawaamuru na kuwaonya watu hao wawe na nidhamu na kufanya kazi ili wajipatie maslahi yao wenyewe.
13But *ye*, brethren, do not faint in well-doing.
13Lakini ninyi ndugu, msichoke kutenda mema.
14But if any one obey not our word by the letter, mark that man, and do not keep company with him, that he may be ashamed of himself;
14Huenda kwamba huko kuna mtu ambaye hatautii huu ujumbe tunaowapelekeeni katika barua hii. Ikiwa hivyo, basi, mfichueni mtu huyo na msiwe na uhusiano wowote naye kusudi aone aibu.
15and do not esteem him as an enemy, but admonish [him] as a brother.
15Lakini msimtendee mtu huyo kama adui, bali mwonyeni kama ndugu.
16But the Lord of peace himself give you peace continually in every way. The Lord [be] with you all.
16Bwana mwenyewe ndiye chanzo cha amani, awajalieni amani siku zote kwa kila namna. Bwana awe nanyi nyote.
17The salutation by the hand of me, Paul, which is [the] mark in every letter; so I write.
17Kwa mkono wangu mwenyewe naandika hivi: Salamu kutoka kwa Paulo! Hivi ndivyo ninavyotia sahihi kila barua; ndivyo ninavyoandika.
18The grace of our Lord Jesus Christ [be] with you all.
18Tunawatakieni nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.