1I testify before God and Christ Jesus, who is about to judge living and dead, and by his appearing and his kingdom,
1Nakuamuru mbele ya Mungu, na mbele ya Kristo Yesu atakayewahukumu watu walio hai na wafu, na kwa sababu anakuja kutawala akiwa Mfalme:
2proclaim the word; be urgent in season [and] out of season, convict, rebuke, encourage, with all longsuffering and doctrine.
2hubiri huo ujumbe, sisitiza kuutangaza (iwe ni wakati wa kufaa au wakati usiofaa), karipia, onya na himiza watu ukiwafundisha kwa uvumilivu wote.
3For the time shall be when they will not bear sound teaching; but according to their own lusts will heap up to themselves teachers, having an itching ear;
3Utakuja wakati ambapo watu hawatasikiliza mafundisho ya kweli, ila watafuata tamaa zao wenyewe na kujikusanyia walimu tele watakaowaambia mambo yale tu ambayo masikio yao yako tayari kusikia.
4and they will turn away their ear from the truth, and will have turned aside to fables.
4Watakataa kuusikia ukweli, watageukia hadithi za uongo.
5But *thou*, be sober in all things, bear evils, do [the] work of an evangelist, fill up the full measure of thy ministry.
5Wewe, lakini, uwe macho katika kila hali; vumilia mateso, fanya kazi ya mhubiri wa Habari Njema, timiza kikamilifu utumishi wako.
6For *I* am already being poured out, and the time of my release is come.
6Kwa upande wangu mimi, niko karibu kabisa kutolewa dhabihu na wakati wa kufariki kwangu umefika.
7I have combated the good combat, I have finished the race, I have kept the faith.
7Nimefanya bidii katika mashindano, nimemaliza safari yote na imani nimeitunza.
8Henceforth the crown of righteousness is laid up for me, which the Lord, the righteous Judge, will render to me in that day; but not only to me, but also to all who love his appearing.
8Na sasa imebakia tu kupewa tuzo la ushindi kwa maisha ya uadilifu, tuzo ambalo Bwana Hakimu wa haki, atanipa mimi Siku ile na wala si mimi tu, ila na wale wote wanaotazamia kwa upendo kutokea kwake.
9Use diligence to come to me quickly;
9Fanya bidii kuja kwangu karibuni.
10for Demas has forsaken me, having loved the present age, and is gone to Thessalonica; Crescens to Galatia, Titus to Dalmatia.
10Dema ameupenda ulimwengu huu akaniacha na kwenda zake Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia, na Tito amekwenda Dalmatia.
11Luke alone is with me. Take Mark, and bring [him] with thyself, for he is serviceable to me for ministry.
11Luka peke yake ndiye aliye hapa pamoja nami. Mpate Marko uje naye, kwa maana ataweza kunisaidia katika kazi yangu.
12But Tychicus I have sent to Ephesus.
12Nilimtuma Tukiko kule Efeso.
13The cloak which I left behind [me] in Troas at Carpus's, bring when thou comest, and the books, especially the parchments.
13Utakapokuja niletee koti langu nililoacha kwa Karpo kule Troa; niletee pia vile vitabu, na hasa vile vilivyotengenezwa kwa ngozi.
14Alexander the smith did many evil things against me. The Lord will render to him according to his works.
14Yule sonara aitwaye Aleksanda amenitendea maovu mengi; Bwana atamlipa kufuatana na hayo matendo yake.
15Against whom be *thou* also on thy guard, for he has greatly withstood our words.
15Jihadhari naye kwa sababu aliupinga ujumbe wetu kwa ukali.
16At my first defence no man stood with me, but all deserted me. May it not be imputed to them.
16Wakati nilipojitetea kwa mara ya kwanza hakuna mtu aliyesimama upande wangu; wote waliniacha. Mungu asiwahesabie kosa hilo!
17But the Lord stood with [me], and gave me power, that through me the proclamation might be fully made, and all [those of] the nations should hear; and I was delivered out of the lion's mouth.
17Lakini, Bwana alikaa pamoja nami, akanipa nguvu, hata nikaweza kuutangaza ujumbe wote, watu wa mataifa wausikie; tena nikaokolewa katika hukumu ya kifo kama kinywani mwa simba.
18The Lord shall deliver me from every wicked work, and shall preserve [me] for his heavenly kingdom; to whom [be] glory for the ages of ages. Amen.
18Bwana ataniokoa na mambo yote maovu, na kunichukua salama mpaka katika Utawala wake wa mbinguni. Kwake uwe utukufu milele na milele! Amina.
19Salute Prisca and Aquila, and the house of Onesiphorus.
19Wasalimu Priska na Akula, pamoja na jamaa ya Onesiforo.
20Erastus remained in Corinth, but Trophimus I left behind in Miletus sick.
20Erasto alibaki Korintho, naye Trofimo nilimwacha Mileto kwa sababu alikuwa mgonjwa.
21Use diligence to come before winter. Eubulus salutes thee, and Pudens, and Linus, and Claudia, and the brethren all.
21Fanya bidii kuja kabla ya majira ya baridi. Ebulo, Pude, Lino na Klaudia wanakusalimu; vilevile ndugu wengine wote.
22The Lord Jesus Christ [be] with your spirit. Grace [be] with you.
22Bwana awe nawe rohoni mwako. Nawatakieni nyote neema.