1But a certain man in Caesarea, -- by name Cornelius, a centurion of the band called Italic,
1Kulikuwa na mtu mmoja huko Kaisarea aitwaye Kornelio, Jemadari wa kikosi kimoja kiitwacho "Kikosi cha Italia."
2pious, and fearing God with all his house, [both] giving much alms to the people, and supplicating God continually,
2Alikuwa mtu mwema; naye pamoja na jamaa yake yote walimcha Mungu; alikuwa anafanya mengi kusaidia maskini wa Kiyahudi na alikuwa anasali daima.
3-- saw plainly in a vision, about the ninth hour of the day, an angel of God coming unto him, and saying to him, Cornelius.
3Yapata saa tisa mchana, aliona dhahiri katika maono malaika wa Mungu akiingia ndani na kumwambia, "Kornelio!"
4But he, having fixed his eyes upon him, and become full of fear, said, What is it, Lord? And he said to him, Thy prayers and thine alms have gone up for a memorial before God.
4Kornelio alimkodolea macho huyo malaika kwa hofu, akamwambia, "Kuna nini Mheshimiwa?" Huyo malaika akamwambia, "Mungu amezipokea sala na sadaka zako kwa maskini.
5And now send men to Joppa and fetch Simon, who is surnamed Peter.
5Sasa, watume watu Yopa wakamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petro.
6He lodges with a certain Simon, a tanner, whose house is by the sea.
6Yeye yumo nyumbani kwa Simoni mtengenezaji wa ngozi ambaye nyumba yake iko karibu na bahari."
7And when the angel who was speaking to him had departed, having called two of his household and a pious soldier of those who were constantly with him,
7Huyo malaika aliyesema hayo alipokwisha kwenda zake, Kornelio aliwaita watumishi wawili wa nyumbani na mmoja wa askari zake ambaye alikuwa mcha Mungu,
8and related all things to them, he sent them to Joppa.
8akawaeleza yote yaliyotukia, akawatuma Yopa.
9And on the morrow, as these were journeying and drawing near to the city, Peter went up on the house to pray, about the sixth hour.
9Kesho yake, hao watu watatu wakiwa bado safarini, lakini karibu kufika Yopa, Petro alipanda juu ya paa la nyumba yapata saa sita mchana ili kusali.
10And he became hungry and desired to eat. But as they were making ready an ecstasy came upon him:
10Aliona njaa, akatamani kupata chakula. Chakula kilipokuwa kinatayarishwa, alipatwa na usingizi mzito akaona maono.
11and he beholds the heaven opened, and a certain vessel descending, as a great sheet, [bound] by [the] four corners [and] let down to the earth;
11Aliona mbingu zimefunguliwa na kitu kama shuka kubwa inateremshwa chini ikiwa imeshikwa pembe zake nne.
12in which were all the quadrupeds and creeping things of the earth, and the fowls of the heaven.
12Ndani ya shuka hiyo kulikuwa na kila aina ya wanyama: wanyama wenye miguu minne, wanyama watambaao na ndege wa angani.
13And there was a voice to him, Rise, Peter, slay and eat.
13Akasikia sauti ikimwambia: "Petro, amka uchinje, ule!"
14And Peter said, In no wise, Lord; for I have never eaten anything common or unclean.
14Petro akajibu, "La, Bwana; mimi sijaonja kamwe chochote ambacho ni najisi au kichafu."
15And [there was] a voice again the second time to him, What God has cleansed, do not *thou* make common.
15Ile sauti ikasikika tena ikimwambia: "Usiviite najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa!"
16And this took place thrice, and the vessel was straightway taken up into heaven.
16Jambo hili lilifanyika mara tatu, kisha ile shuka ikarudishwa juu mbinguni.
17And as Peter doubted in himself what the vision which he had seen might mean, behold also the men who were sent by Cornelius, having sought out the house of Simon, stood at the gate,
17Petro alipokuwa bado anashangaa juu ya maana ya hilo maono alilokuwa ameliona, wale watu waliotumwa na Kornelio, baada ya kuigundua nyumba ya Simoni, walifika mlangoni,
18and having called [some one], they inquired if Simon who was surnamed Peter was lodged there.
18Wakaita kwa sauti: "Je, kuna mgeni humu aitwaye Simoni Petro?"
19But as Peter continued pondering over the vision, the Spirit said to him, Behold, three men seek thee;
19Petro alikuwa bado anajaribu kuelewa lile maono, na hapo Roho akamwambia, "Sikiliza! kuna watu watatu hapa, wanakutafuta.
20but rise up, go down, and go with them, nothing doubting, because *I* have sent them.
20Shuka upesi na wala usisite kwenda pamoja nao kwa maana ni mimi niliyewatuma."
21And Peter going down to the men said, Behold, *I* am he whom ye seek: what is the cause for which ye come?
21Basi, Petro akateremka chini, akawaambia hao watu, "Mimi ndiye mnayemtafuta. Kwa nini mmekuja?"
22And they said, Cornelius, a centurion, a righteous man, and fearing God, and borne witness to by the whole nation of the Jews, has been divinely instructed by a holy angel to send for thee to his house, and hear words from thee.
22Wao wakamjibu, "Jemadari Kornelio ambaye ni mtu mwema, mcha Mungu na mwenye kuheshimika mbele ya Wayahudi wote ametutuma. Aliambiwa na malaika mtakatifu akualike nyumbani kwake ili asikilize chochote ulicho nacho cha kusema."
23Having therefore invited them in, he lodged them. And on the morrow, rising up he went away with them, and certain of the brethren from Joppa went with him.
23Petro akawaalika ndani, akawapa mahali pa kulala usiku ule. Kesho yake, Petro alianza safari pamoja nao, na baadhi ya ndugu wa huko Yopa walifuatana naye.
24And on the morrow they came to Caesarea. But Cornelius was looking for them, having called together his kinsmen and [his] intimate friends.
24Siku ya pili yake, walifika Kaisarea na huko Kornelio alikuwa anawangojea pamoja na jamaa na marafiki aliokuwa amewaalika.
25And when Peter was now coming in, Cornelius met him, and falling down did [him] homage.
25Petro alipokuwa anaingia, Kornelio alitoka nje kumlaki, akapiga magoti mbele yake na kuinama chini kabisa.
26But Peter made him rise, saying, Rise up: *I* myself also am a man.
26Lakini Petro alimwinua, akamwambia, "Simama, kwa maana mimi ni binadamu tu."
27And he went in, talking with him, and found many gathered together.
27Petro aliendelea kuongea na Kornelio wakiwa wanaingia nyumbani ambamo aliwakuta watu wengi wamekusanyika.
28And he said to them, *Ye* know how it is unlawful for a Jew to be joined or come to one of a strange race, and to *me* God has shewn to call no man common or unclean.
28Petro akawaambia, "Ninyi wenyewe mnajua kwamba Myahudi yeyote amekatazwa na Sheria yake ya dini kushirikiana na watu wa mataifa mengine. Lakini Mungu amenijulisha nisimfikirie mtu yeyote kuwa najisi au mchafu.
29Wherefore also, having been sent for, I came without saying anything against it. I inquire therefore for what reason ye have sent for me.
29Kwa sababu hiyo, mliponiita nimekuja bila kusita. Basi, nawaulizeni: kwa nini mmeniita?"
30And Cornelius said, Four days ago I had been [fasting] unto this hour, and the ninth [I was] praying in my house, and lo, a man stood before me in bright clothing,
30Kornelio akasema, "Siku tatu zilizopita saa kama hii, saa tisa alasiri, nilikuwa nikisali chumbani mwangu. Ghafla, mtu aliyekuwa amevaa mavazi yenye kun'gaa alisimama mbele yangu,
31and said, Cornelius, thy prayer has been heard, and thy alms have come in remembrance before God.
31akasema: Kornelio! Sala yako na sadaka zako kwa maskini vimekubaliwa na Mungu.
32Send therefore to Joppa and fetch Simon, who is surnamed Peter; he lodges in the house of Simon, a tanner, by the sea [who when he is come will speak to thee].
32Mtume mtu Yopa akamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petroi; yuko nyumbani kwa Simoni mtengenezaji wa ngozi karibu na bahari.
33Immediately therefore I sent to thee, and *thou* hast well done in coming. Now therefore *we* are all present before God to hear all things that are commanded thee of God.
33Kwa hiyo nilikutumia ujumbe bila kuchelewa, nawe umefanya vyema kuja. Sasa, sisi tuko mbele ya Mungu, kusikiliza chochote ambacho bwana amekuamuru kusema."
34And Peter opening his mouth said, Of a truth I perceive that God is no respecter of persons,
34Hapo Petro akaanza kusema: "Sasa nimetambua kwamba hakika Mungu hana ubaguzi.
35but in every nation he that fears him and works righteousness is acceptable to him.
35Mtu wa taifa lolote anayemcha Mungu na kutenda haki anapokelewa naye.
36The word which he sent to the sons of Israel, preaching peace by Jesus Christ, (*he* is Lord of all things,)
36Huu ndio ule ujumbe Mungu alioupeleka kwa watu wa Israeli, akitangaza Habari Njema iletayo amani kwa njia ya Yesu Kristo ambaye ni Bwana wa wote.
37*ye* know; the testimony which has spread through the whole of Judaea, beginning from Galilee after the baptism which John preached --
37Ninyi mnajua jambo lililotukia katika nchi yote ya Wayahudi kuanzia Galilaya baada ya ule ubatizo aliohubiri Yohane.
38Jesus who [was] of Nazareth: how God anointed him with [the] Holy Spirit and with power; who went through [all quarters] doing good, and healing all that were under the power of the devil, because God was with him.
38Mnajua Yesu wa Nazareti na jinsi Mungu alivyomteua kwa kummiminia Roho Mtakatifu na nguvu. Mungu alikuwa pamoja naye; yeye alikwenda huko na huko akitenda mema na kuwaponya wote waliokuwa wamevamiwa na Ibilisi.
39*We* also [are] witnesses of all things which he did both in the country of the Jews and in Jerusalem; whom they also slew, having hanged him on a cross.
39Sisi ni mashahidi wa mambo yote aliyotenda katika nchi ya Wayahudi na katika Yerusalemu. Walimuua kwa kumtundika msalabani;
40This [man] God raised up the third day and gave him to be openly seen,
40lakini Mungu alimfufua siku ya tatu, akamfanya aonekane
41not of all the people, but of witnesses who were chosen before of God, *us* who have eaten and drunk with him after he arose from among [the] dead.
41si kwa watu wote ila kwa wale Mungu aliokwisha wachagua wawe mashahidi wake, yaani sisi tuliokula na kunywa pamoja naye baada ya kufufuka kwake kutoka wafu.
42And he commanded us to preach to the people, and to testify that *he* it is who was determinately appointed of God [to be] judge of living and dead.
42Alituamuru kuihubiri Habari Njema kwa watu wote na kushuhudia kwamba yeye ndiye aliyeteuliwa na Mungu awe Mwamuzi wa wazima na wafu.
43To him all the prophets bear witness that every one that believes on him will receive through his name remission of sins.
43Manabii wote waliongea juu yake kwamba kila mtu atakayemwamini atasamehewa dhambi zake zote kwa jina lake."
44While Peter was yet speaking these words the Holy Spirit fell upon all those who were hearing the word.
44Wakati Petro alipokuwa bado anasema maneno hayo, Roho Mtakatifu aliwashukia wote waliokuwa wanasikiliza ujumbe huo.
45And the faithful of the circumcision were astonished, as many as came with Peter, that upon the nations also the gift of the Holy Spirit was poured out:
45Wale Wayahudi waumini waliokuja pamoja na Petro kutoka Yopa walishangaa kuona kuwa Mungu aliwamiminia zawadi ya Roho Mtakatifu watu wa mataifa mengine pia;
46for they heard them speaking with tongues and magnifying God. Then Peter answered,
46maana waliwasikia wakiongea kwa lugha mbalimbali wakimtukuza Mungu. Hapo Petro akasema,
47Can any one forbid water that these should not be baptised, who have received the Holy Spirit as we also [did]?
47"Watu hawa wamempokea Roho Mtakatifu kama sisi wenyewe tulivyompokea. Je, kuna yeyote atakayeweza kuwazuia wasibatizwe kwa maji?"
48And he commanded them to be baptised in the name of the Lord. Then they begged him to stay some days.
48Basi, akaamuru wabatizwe kwa jina la Yesu Kristo. Kisha wakamwomba akae nao kwa siku chache.