Darby's Translation

Swahili: New Testament

Acts

12

1At that time Herod the king laid his hands on some of those of the assembly to do them hurt,
1Karibu wakati huohuo, mfalme Herode alianza kuwatesa baadhi ya Wakristo.
2and slew James, the brother of John, with the sword.
2Alimwua kwa upanga Yakobo ndugu yake Yohane.
3And seeing that it was pleasing to the Jews, he went on to take Peter also: (and they were the days of unleavened bread:)
3Alipoona kuwa kitendo hiki kiliwapendeza Wayahudi, aliendelea, akamkamata Petro. (Hiyo ilifanyika wakati wa sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu.)
4whom having seized he put in prison, having delivered him to four quaternions of soldiers to keep, purposing after the passover to bring him out to the people.
4Baada ya kutiwa nguvuni, Petro alifungwa gerezani, akawekwa chini ya ulinzi wa vikundi vinne vya askari wannewanne. Herode alikusudia kumtoa hadharani baada ya sikukuu ya Pasaka.
5Peter therefore was kept in the prison; but unceasing prayer was made by the assembly to God concerning him.
5Basi, Petro alipokuwa gerezani, kanisa lilikuwa linamwombea kwa Mungu kwa moyo.
6And when Herod was going to bring him forth, that night Peter was sleeping between two soldiers, bound with two chains, and guards before the door kept the prison.
6Usiku, kabla ya siku ile ambayo Herode angemtoa Petro hadharani, Petro alikuwa amelala kati ya askari wawili. Alikuwa amefungwa minyororo miwili, na walinzi walikuwa wanalinda lango la gereza.
7And lo, an angel of [the] Lord came there, and a light shone in the prison: and having smitten the side of Peter, he roused him up, saying, Rise up quickly. And his chains fell off his hands.
7Ghafla, malaika wa Bwana akasimama karibu naye na mwanga ukaangaza kile chumba cha gereza. Malaika akamgusa akisema, "Amka upesi!" Mara ile minyororo ikaanguka kutoka katika mikono yake.
8And the angel said to him, Gird thyself, and bind on thy sandals. And he did so. And he says to him, Cast thine upper garment about thee and follow me.
8Malaika akamwambia, "Jifunge mshipi wako, vaa viatu vyako." Akafanya hivyo. Kisha huyo malaika akamwambia, "Vaa koti lako, unifuate."
9And going forth he followed [him] and did not know that what was happening by means of the angel was real, but supposed he saw a vision.
9Petro akamfuata nje lakini hakujua kama hayo yaliyofanywa na huyo malaika yalikuwa ya kweli; alidhani alikuwa anaota ndoto.
10And having passed through a first and second guard, they came to the iron gate which leads into the city, which opened to them of itself; and going forth they went down one street, and immediately the angel left him.
10Walipita kituo cha kwanza cha ulinzi na cha pili, halafu wakafika kwenye mlango wa chuma wa kuingilia mjini. Huo mlango ukawafungukia wenyewe, nao wakatoka nje. Wakawa wanatembea katika barabara moja na mara yule malaika akamwacha Petro peke yake.
11And Peter, being come to himself, said, Now I know certainly that [the] Lord has sent forth his angel and has taken me out of the hand of Herod and all the expectation of the people of the Jews.
11Hapo ndipo Petro alipotambua yaliyotukia, akasema, "Sasa najua kwa hakika kwamba Bwana amemtuma malaika wake akaniokoa kutoka katika mkono wa Herode na kutoka katika mambo yale yote watu wa Israeli waliyotazamia."
12And having become clearly conscious [in himself], he came to the house of Mary, the mother of John who was surnamed Mark, where were many gathered together and praying.
12Alipotambua hivyo alikwenda moja kwa moja mpaka nyumbani kwa Maria mama yake Yohane aitwaye Marko. Humo watu wengi walikuwa wamekusanyika wakisali.
13And when he had knocked at the door of the entry, a maid came to listen, by name Rhoda;
13Petro alibisha mlango wa nje na mtumishi mmoja msichana aitwaye Roda, akaenda mlangoni kuitikia.
14and having recognised the voice of Peter, through joy did not open the entry, but running in, reported that Peter was standing before the entry.
14Huyo msichana aliitambua sauti ya Petro akafurahi mno, hata badala ya kuufungua ule mlango, akakimbilia ndani na kuwaambia kwamba Petro alikuwa amesimama nje mlangoni.
15And they said to her, Thou art mad. But she maintained that it was so. And they said, It is his angel.
15Wakamwambia yule msichana, "Una wazimu!" Lakini yeye akasisitiza kwamba ilikuwa kweli. Nao wakamwambia, "Huyo ni malaika wake."
16But Peter continued knocking: and having opened, they saw him and were astonished.
16Wakati huo Petro alikuwa anaendelea kupiga hodi. Mwishowe walifungua mlango, wakamwona, wakashangaa.
17And having made a sign to them with his hand to be silent, he related [to them] how the Lord had brought him out of prison; and he said, Report these things to James and to the brethren. And he went out and went to another place.
17Petro aliwaashiria kwa mkono wakae kimya, akawaeleza jinsi Bwana alivyomtoa gerezani. Kisha akawaambia watoe taarifa ya jambo hilo kwa Yakobo na wale ndugu wengine, halafu akatoka akaenda mahali pengine.
18And when it was day there was no small disturbance among the soldiers, what then was become of Peter.
18Kulipokucha, ulitokea wasiwasi mkubwa kati ya wale askari kuhusu yaliyokuwa yamempata Petro.
19And Herod having sought him and not found him, having examined the guards, commanded [them] to be executed. And he went down from Judaea to Caesarea and stayed [there].
19Herode aliamuru ufanywe msako lakini hawakuweza kumpata. Hivyo aliamuru wale askari wahojiwe, akatoa amri wauawe. Halafu akatoka huko Yudea akaenda Kaisarea ambako alikaa.
20And he was in bitter hostility with [the] Tyrians and Sidonians; but they came to him with one accord, and, having gained Blastus the king's chamberlain, sought peace, because their country was nourished by the king's.
20Herode alikasirishwa sana na watu wa Tiro na Sidoni. Lakini wao walimpelekea wajumbe. Nao wakafaulu kwanza kumpata Blasto awe upande wao. Blasto alikuwa msimamizi mkuu wa ikulu ya mfalme. Kisha, wakamwendea Herode wakamwomba kuwe na amani, kwa maana nchi yao ilitegemea nchi ya mfalme kwa chakula.
21And on a set day, clothed in royal apparel and sitting on the elevated seat [of honour], Herod made a public oration to them.
21Siku moja iliyochaguliwa, Herode akiwa amevaa mavazi rasmi na kuketi katika kiti cha kifalme aliwahutubia watu.
22And the people cried out, A god's voice and not a man's.
22Wale watu walimpigia kelele za shangwe wakisema, "Hii ni sauti ya mungu, si ya mtu."
23And immediately an angel of [the] Lord smote him, because he did not give the glory to God, and he expired, eaten of worms.
23Papo hapo malaika wa Bwana akamwangusha Herode chini kwa sababu hakumpa Mungu hizo sifa. Akaliwa na wadudu, akafa.
24But the word of God grew and spread itself.
24Neno la Mungu likazidi kuenea na kukua.
25And Barnabas and Saul returned from Jerusalem, having fulfilled the service [entrusted to them], taking also with them John, surnamed Mark.
25Baada ya Barnaba na Saulo kutekeleza shughuli zao, walitoka tena Yerusalemu wakamchukua Yohane aitwaye pia Marko.