Darby's Translation

Swahili: New Testament

Ephesians

3

1For this reason *I* Paul, prisoner of the Christ Jesus for you nations,
1Kutokana na hayo, mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu, namwomba Mungu.
2(if indeed ye have heard of the administration of the grace of God which has been given to me towards you,
2Bila shaka mmekwisha sikia kwamba Mungu, kwa neema yake, alinikabidhi kazi hii niifanye kwa faida yenu.
3that by revelation the mystery has been made known to me, (according as I have written before briefly,
3Mimi nilijulishwa kwa njia ya ufunuo mpango wake uliofichika. (Nimeandika kwa ufupi juu ya jambo hili,
4by which, in reading it, ye can understand my intelligence in the mystery of the Christ,)
4nanyi mkiyasoma maneno yangu mtaweza kujua jinsi ninavyoielewa siri hiyo ya Kristo.)
5which in other generations has not been made known to the sons of men, as it has now been revealed to his holy apostles and prophets in [the power of the] Spirit,
5Zamani watu hawakujulishwa siri hiyo; lakini sasa Mungu amewajulisha mitume na manabii wake watakatifu kwa njia ya Roho.
6that [they who are of] the nations should be joint heirs, and a joint body, and joint partakers of [his] promise in Christ Jesus by the glad tidings;
6Siri yenyewe ni hii: kwa njia ya Habari Njema watu wa mataifa mengine wanapata sehemu yao pamoja na Wayahudi katika zile baraka za Mungu; wao ni viungo vya mwili uleule, na wanashiriki ahadi ileile aliyofanya Mungu kwa njia ya Kristo Yesu.
7of which I am become minister according to the gift of the grace of God given to me, according to the working of his power.
7Mimi nimefanywa kuwa mtumishi wa Habari Njema kwa neema ya pekee aliyonijalia Mungu kwa uwezo wake mkuu.
8To me, less than the least of all saints, has this grace been given, to announce among the nations the glad tidings of the unsearchable riches of the Christ,
8Mimi ni mdogo kuliko watu wote wa Mungu; lakini amenijalia neema yake, ili niwahubirie watu wa mataifa utajiri wake Kristo usiopimika,
9and to enlighten all [with the knowledge of] what is the administration of the mystery hidden throughout the ages in God, who has created all things,
9tena niwaangazie watu wote waone jinsi mpango wa Mungu uliofichika unavyotekelezwa. Mungu aliye Muumba wa vitu vyote alificha siri hiyo yake tangu milele,
10in order that now to the principalities and authorities in the heavenlies might be made known through the assembly the all-various wisdom of God,
10kusudi, sasa kwa njia ya kanisa, wakuu na wenye enzi wa mbinguni wapate kuitambua hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi.
11according to [the] purpose of the ages, which he purposed in Christ Jesus our Lord,
11Mungu alifanya jambo hilo kufuatana na azimio lake la milele ambalo amelifanya kwa njia ya Kristo Bwana wetu.
12in whom we have boldness and access in confidence by the faith of him.
12Basi, katika kuungana na Kristo, na kwa njia ya imani katika Kristo, sisi tunathubutu kumkaribia Mungu kwa uhodari.
13Wherefore I beseech [you] not to faint through my tribulations for you, which is your glory.
13Kwa hiyo, nawaombeni msife moyo kwa sababu ya mateso ninayopata kwa ajili yenu, maana hayo ni kwa ajili ya utukufu wenu.
14For this reason I bow my knees to the Father [of our Lord Jesus Christ],
14Kwa sababu hiyo, nampigia magoti Baba,
15of whom every family in [the] heavens and on earth is named,
15aliye asili ya jamaa zote duniani na mbinguni.
16in order that he may give you according to the riches of his glory, to be strengthened with power by his Spirit in the inner man;
16Namwomba Mungu, kadiri ya utajiri wa utukufu wake, awajalieni kwa uwezo wa Roho wake, nguvu ya kuwa imara ndani yenu,
17that the Christ may dwell, through faith, in your hearts, being rooted and founded in love,
17naye Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani. Namwomba mpate kuwa na mzizi na msingi katika mapendo
18in order that ye may be fully able to apprehend with all the saints what [is] the breadth and length and depth and height;
18kusudi muweze kufahamu pamoja na watu wote wa Mungu jinsi upendo wa Kristo ueneavyo kwa mapana na marefu, kwa kimo na kina.
19and to know the love of the Christ which surpasses knowledge; that ye may be filled [even] to all the fulness of God.
19Naam, mpate kujua upendo wa Kristo upitao elimu yote, mjazwe kabisa utimilifu wote wa Mungu.
20But to him that is able to do far exceedingly above all which we ask or think, according to the power which works in us,
20Kwake yeye ambaye kwa nguvu yake ifanyayo kazi ndani yetu, aweza kufanya mambo makuu zaidi ya yale tuwezayo kuomba au kufikiria;
21to him be glory in the assembly in Christ Jesus unto all generations of the age of ages. Amen).
21kwake Mungu uwe utukufu katika kanisa na katika Kristo Yesu, nyakati zote, milele na milele! Amina.