Darby's Translation

Swahili: New Testament

Galatians

1

1Paul, apostle, not from men nor through man, but through Jesus Christ, and God [the] Father who raised him from among [the] dead,
1Mimi Paulo mtume,
2and all the brethren with me, to the assemblies of Galatia.
2na ndugu wote walio pamoja nami, tunayaandikia makanisa yaliyoko Galatia. Mimi nimepata kuwa mtume si kutokana na mamlaka ya binadamu, wala si kwa nguvu ya mtu, bali kwa uwezo wa Yesu Kristo na wa Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka wafu.
3Grace to you, and peace, from God [the] Father, and our Lord Jesus Christ,
3Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
4who gave himself for our sins, so that he should deliver us out of the present evil world, according to the will of our God and Father;
4Kristo alijitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na mapenzi ya Mungu wetu na Baba, ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu mbaya wa sasa.
5to whom [be] glory to the ages of ages. Amen.
5Kwake yeye uwe utukufu milele! Amina.
6I wonder that ye thus quickly change, from him that called you in Christ's grace, to a different gospel,
6Nashangaa kwamba muda mfupi tu umepita, nanyi mnamwasi yule aliyewaita kwa neema ya Kristo, mkafuata Habari Njema ya namna nyingine.
7which is not another [one]; but there are some that trouble you, and desire to pervert the glad tidings of the Christ.
7Lakini hakuna "Habari Njema" nyingine. Ukweli ni kwamba wako watu wanaowavurugeni, watu wanaotaka kuipotosha Habari Njema ya Kristo.
8But if even *we* or an angel out of heaven announce as glad tidings to you [anything] besides what we have announced as glad tidings to you, let him be accursed.
8Lakini, hata kama mmoja wetu au malaika kutoka mbinguni, atawahubirieni Habari Njema tofauti na ile tuliyowahubirieni sisi, basi huyo na alaaniwe!
9As we have said before, now also again I say, If any one announce to you as glad tidings [anything] besides what ye have received, let him be accursed.
9Tulikwisha sema, na sasa nasema tena: kama mtu yeyote anawahubirieni Habari Njema ya aina nyingine, tofauti na ile mliyokwisha pokea, huyo na alaaniwe!
10For do I now seek to satisfy men or God? or do I seek to please men? If I were yet pleasing men, I were not Christ's bondman.
10Sasa nataka kibali cha nani: cha binadamu, ama cha Mungu? Au je, nataka kuwapendeza watu? Kama ningefanya hivyo, mimi singekuwa kamwe mtumishi wa Kristo.
11But I let you know, brethren, [as to] the glad tidings which were announced by me, that they are not according to man.
11Ndugu, napenda mfahamu kwamba ile Habari Njema niliyoihubiri si ujumbe wa kibinadamu.
12For neither did I receive them from man, neither was I taught [them], but by revelation of Jesus Christ.
12Wala mimi sikuipokea kutoka kwa binadamu, wala sikufundishwa na mtu. Yesu Kristo mwenyewe ndiye aliyenifunulia.
13For ye have heard [what was] my conversation formerly in Judaism, that I excessively persecuted the assembly of God, and ravaged it;
13Bila shaka mlikwisha sikia jinsi nilivyokuwa ninaishi zamani kwa kuzingatia dini ya Kiyahudi, na jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kupita kiasi na kutaka kuliharibu kabisa.
14and advanced in Judaism beyond many [my] contemporaries in my nation, being exceedingly zealous of the doctrines of my fathers.
14Naam, mimi niliwashinda wengi wa wananchi wenzangu wa rika langu katika kuizingatia dini ya Kiyahudi, nikajitahidi sana kuyashika mapokeo ya wazee wetu.
15But when God, who set me apart [even] from my mother's womb, and called [me] by his grace,
15Lakini Mungu, kwa neema yake, alikuwa ameniteua hata kabla sijazaliwa, akaniita nimtumikie.
16was pleased to reveal his Son in me, that I may announce him as glad tidings among the nations, immediately I took not counsel with flesh and blood,
16Mara tu alipoamua kunifunulia Mwanae kusudi niihubiri Habari Njema yake kwa watu wa mataifa mengine, bila kutafuta maoni ya binadamu,
17nor went I up to Jerusalem to those [who were] apostles before me; but I went to Arabia, and again returned to Damascus.
17na bila kwenda kwanza Yerusalemu kwa wale waliopata kuwa mitume kabla yangu, nilikwenda kwanza Arabia, kisha nikarudi tena Damasko.
18Then after three years I went up to Jerusalem to make acquaintance with Peter, and I remained with him fifteen days;
18Ilikuwa tu baada ya miaka mitatu, ndipo nilipokwenda Yerusalemu kuonana na Kefa; nilikaa kwake siku kumi na tano.
19but I saw none other of the apostles, but James the brother of the Lord.
19Lakini sikuwaona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
20Now what I write to you, behold, before God, I do not lie.
20Haya ninayowaandikieni, Mungu anajua; sisemi uongo.
21Then I came into the regions of Syria and Cilicia.
21Baadaye nilikwenda katika tarafa za Siria na Kilikia.
22But I was unknown personally to the assemblies of Judaea which [are] in Christ;
22Wakati huo, mimi binafsi sikujulikana kwa jumuiya za Wakristo kule Yudea.
23only they were hearing that he who persecuted us formerly now announces the glad tidings of the faith which formerly he ravaged:
23Walichokuwa wanajua ni kile tu walichosikia: "Mtu yule aliyekuwa akitutesa hapo awali, sasa anaihubiri imani ileile aliyokuwa anajaribu kuiangamiza."
24and they glorified God in me.
24Basi, wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.