1For the law, having a shadow of the coming good things, not the image itself of the things, can never, by the same sacrifices which they offer continually yearly, perfect those who approach.
1Sheria ya Wayahudi si picha kamili ya mambo yale halisi: ni kivuli tu cha mema yanayokuja. Dhabihu zilezile hutolewa daima, mwaka baada ya mwaka. Sheria yawezaje, basi, kwa njia ya dhabihu hizo, kuwafanya wale wanaoabudu wawe wakamilifu?
2Since, would they not indeed have ceased being offered, on account of the worshippers once purged having no longer any conscience of sins?
2Kama hao watu wanaomwabudu Mungu wangekuwa wametakaswa dhambi zao kweli, hawangejisikia tena kuwa na dhambi, na dhabihu hizo zote zingekoma.
3But in these [there is] a calling to mind of sins yearly.
3Lakini dhabihu hizo hufanyika kila mwaka kuwakumbusha watu dhambi zao.
4For blood of bulls and goats [is] incapable of taking away sins.
4Maana damu ya fahali na mbuzi haiwezi kamwe kuondoa dhambi.
5Wherefore coming into the world he says, Sacrifice and offering thou willedst not; but thou hast prepared me a body.
5Ndiyo maana Kristo alipokuwa anakuja ulimwenguni, alimwambia Mungu: "Hukutaka dhabihu wala sadaka, lakini umenitayarishia mwili.
6Thou tookest no pleasure in burnt-offerings and sacrifices for sin.
6Sadaka za kuteketezwa au za kuondoa dhambi hazikupendezi.
7Then I said, Lo, I come (in [the] roll of the book it is written of me) to do, O God, thy will.
7Hapo nikasema: Niko hapa ee Mungu, tayari kufanya mapenzi yako kama ilivyoandikwa juu yangu katika kitabu cha Sheria."
8Above, saying Sacrifices and offerings and burnt-offerings and sacrifices for sin thou willedst not, neither tookest pleasure in (which are offered according to the law);
8Kwanza alisema: "Hutaki, wala hupendezwi na dhabihu na sadaka, sadaka za kuteketezwa na za kuondoa dhambi." Alisema hivyo ingawa sadaka hizi zote hutolewa kufuatana na Sheria.
9then he said, Lo, I come to do thy will. He takes away the first that he may establish the second;
9Kisha akasema: "Niko hapa, ee Mungu, tayari kufanya mapenzi yako." Hivyo Mungu alibatilisha dhabihu za zamani na mahali pake akaweka dhabihu nyingine moja.
10by which will we have been sanctified through the offering of the body of Jesus Christ once for all.
10Kwa kuwa Yesu Kristo alitimiza mapenzi ya Mungu, sisi tunatakaswa dhambi zetu kwa ile dhabihu ya mwili wake aliyotoa mara moja tu, ikatosha.
11And every priest stands daily ministering, and offering often the same sacrifices, which can never take away sins.
11Kila kuhani Myahudi humhudumia Mungu kila siku, akitoa dhabibu zilezile mara nyingi, dhabibu ambazo haziwezi kuondoa dhambi.
12But *he*, having offered one sacrifice for sins, sat down in perpetuity at [the] right hand of God,
12Lakini Kristo alitoa dhabihu moja tu kwa ajili ya dhambi, dhabihu ifaayo milele, kisha akaketi upande wa kulia wa Mungu.
13waiting from henceforth until his enemies be set [for the] footstool of his feet.
13Huko anangoja mpaka adui zake watakapowekwa kama kibao chini ya miguu yake.
14For by one offering he has perfected in perpetuity the sanctified.
14Basi, kwa dhabihu yake moja tu, amewafanya kuwa wakamilifu milele wale wanaotakaswa dhambi zao.
15And the Holy Spirit also bears us witness [of it]; for after what was said:
15Naye Roho Mtakatifu anatupa ushahidi wake. Kwanza anasema:
16This [is] the covenant which I will establish towards them after those days, saith [the] Lord: Giving my laws into their hearts, I will write them also in their understandings;
16"Hili ndilo agano nitakalofanya nao, katika siku zijazo, asema Bwana: Nitaweka sheria zangu mioyoni mwao, na kuziandika akilini mwao."
17and their sins and their lawlessnesses I will never remember any more.
17Kisha akaongeza kusema: "Sitakumbuka tena dhambi zao, wala vitendo vyao vya uhalifu."
18But where there [is] remission of these, [there is] no longer a sacrifice for sin.
18Basi, dhambi zikisha ondolewa, hakutakuwa na haja tena ya kutoa dhabihu za kuondoa dhambi.
19Having therefore, brethren, boldness for entering into the [holy of] holies by the blood of Jesus,
19Basi, ndugu, kwa damu ya Yesu tunapewa moyo thabiti wa kuingia Mahali Patakatifu.
20the new and living way which he has dedicated for us through the veil, that is, his flesh,
20Yeye ametufungulia njia mpya na yenye uzima kupitia lile pazia, yaani kwa njia ya mwili wake mwenyewe.
21and [having] a great priest over the house of God,
21Basi, tunaye kuhani maarufu aliye na mamlaka juu ya nyumba ya Mungu.
22let us approach with a true heart, in full assurance of faith, sprinkled as to our hearts from a wicked conscience, and washed as to our body with pure water.
22Kwa hiyo tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu na imani timilifu, kwa mioyo iliyotakaswa dhamiri mbaya, na kwa miili iliyosafishwa kwa maji safi.
23Let us hold fast the confession of the hope unwavering, (for he [is] faithful who has promised;)
23Tushikilie imara tumaini lile tunalokiri, maana Mungu aliyefanya ahadi zake ni mwaminifu.
24and let us consider one another for provoking to love and good works;
24Tujitahidi kushughulikiana kwa ajili ya kuongezeana bidii ya kupendana na kutenda mema.
25not forsaking the assembling of ourselves together, as the custom [is] with some; but encouraging [one another], and by so much the more as ye see the day drawing near.
25Tusiache ile desturi ya kukutana pamoja, kama vile wengine wanavyofanya. Bali tunapaswa kusaidiana kwani, kama mwonavyo, Siku ile ya Bwana inakaribia.
26For where we sin wilfully after receiving the knowledge of the truth, there no longer remains any sacrifice for sins,
26Maana, tukiendelea kutenda dhambi makusudi baada ya kufahamu ukweli, hakuna dhabihu iwezayo kutolewa tena kwa ajili ya kuondoa dhambi.
27but a certain fearful expectation of judgment, and heat of fire about to devour the adversaries.
27Linalobaki ni kungojea tu kwa hofu hukumu ya Mungu na moto mkali utakaowaangamiza wote wanaompinga.
28Any one that has disregarded Moses' law dies without mercy on [the testimony of] two or three witnesses:
28Mtu yeyote asiyeitii Sheria ya Mose, huuawa bila ya huruma kukiwa na ushahidi wa watu wawili au watatu.
29of how much worse punishment, think ye, shall he be judged worthy who has trodden under foot the Son of God, and esteemed the blood of the covenant, whereby he has been sanctified, common, and has insulted the Spirit of grace?
29Je, mtu yule anayempuuza Mwana wa Mungu na kuidharau damu ya agano la Mungu iliyomtakasa, mtu anayemtukana Roho wa Mungu, anastahili kupata adhabu kali ya namna gani?
30For we know him that said, To me [belongs] vengeance; *I* will recompense, saith the Lord: and again, The Lord shall judge his people.
30Maana tunamfahamu yule aliyesema, "Mimi nitalipiza kisasi, mimi nitalipiza," na ambaye alisema pia, "Bwana atawahukumu watu wake."
31[It is] a fearful thing falling into [the] hands of [the] living God.
31Kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai ni jambo la kutisha mno!
32But call to mind the earlier days in which, having been enlightened, ye endured much conflict of sufferings;
32Kumbukeni yaliyotokea siku zile za kwanza mlipoangaziwa mwanga wa Mungu. Ingawa siku zile mlipatwa na mateso mengi, ninyi mlistahimili.
33on the one hand, when ye were made a spectacle both in reproaches and afflictions; and on the other, when ye became partakers with those who were passing through them.
33Mara nyingine mlitukanwa na kufedheheshwa hadharani; mara nyingine mlikuwa radhi kuungana na wale walioteswa namna hiyohiyo.
34For ye both sympathised with prisoners and accepted with joy the plunder of your goods, knowing that ye have for yourselves a better substance, and an abiding one.
34Mlishiriki mateso ya wafungwa, na mliponyang'anywa mali yenu mlistahimili kwa furaha, maana mlijua kwamba mnayo mali bora zaidi na ya kudumu milele.
35Cast not away therefore your confidence, which has great recompense.
35Basi, msipoteze uhodari wenu, maana utawapatieni tuzo kubwa.
36For ye have need of endurance in order that, having done the will of God, ye may receive the promise.
36Mnahitaji kuwa na uvumilivu, ili mweze kufanya anayotaka Mungu na kupokea kile alichoahidi.
37For yet a very little while he that comes will come, and will not delay.
37Maana kama yasemavyo Maandiko: "Bado kidogo tu, na yule anayekuja, atakuja, wala hatakawia.
38But the just shall live by faith; and, if he draw back, my soul does not take pleasure in him.
38Lakini mtu wangu aliye mwadilifu ataamini na kuishi; walakini akirudi nyuma, mimi sitapendezwa naye."
39But *we* are not drawers back to perdition, but of faith to saving [the] soul.
39Basi, sisi hatumo miongoni mwa wale wanaorudi nyuma na kupotea, ila sisi tunaamini na tunaokolewa.