Darby's Translation

Swahili: New Testament

John

4

1When therefore the Lord knew that the Pharisees had heard that Jesus makes and baptises more disciples than John
1Mafarisayo walisikia kwamba Yesu alikuwa anabatiza na kuwapata wanafunzi wengi kuliko Yohane.
2(however, Jesus himself did not baptise, but his disciples),
2(Lakini ukweli ni kwamba Yesu hakuwa anabatiza ila wanafunzi wake.)
3he left Judaea and went away again unto Galilee.
3Basi, Yesu aliposikia hayo, alitoka Yudea akarudi Galilaya;
4And he must needs pass through Samaria.
4na katika safari hiyo ilimbidi apitie Samaria.
5He comes therefore to a city of Samaria called Sychar, near to the land which Jacob gave to his son Joseph.
5Basi, akafika Sukari, mji mmoja wa Samaria, karibu na shamba ambalo Yakobo alikuwa amempa mwanawe, Yosefu.
6Now a fountain of Jacob's was there; Jesus therefore, being wearied with the way he had come, sat just as he was at the fountain. It was about the sixth hour.
6Mahali hapo palikuwa na kisima cha Yakobo, naye Yesu, kutokana na uchovu wa safari, akaketi kando ya kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
7A woman comes out of Samaria to draw water. Jesus says to her, Give me to drink
7Basi, mwanamke mmoja Msamaria akafika kuteka maji. Yesu akamwambia, "Nipatie maji ninywe."
8(for his disciples had gone away into the city that they might buy provisions).
8(Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)
9The Samaritan woman therefore says to him, How dost thou, being a Jew, ask to drink of me who am a Samaritan woman? for Jews have no intercourse with Samaritans.
9Lakini huyo mwanamke akamwambia, "Wewe ni Myahudi; mimi ni mwanamke Msamaria! Unawezaje kuniomba maji?" (Wayahudi hawakuwa na ushirikiano na Wasamaria katika matumizi ya vitu.)
10Jesus answered and said to her, If thou knewest the gift of God, and who it is that says to thee, Give me to drink, thou wouldest have asked of him, and he would have given thee living water.
10Yesu akamjibu, "Kama tu ungalijua zawadi ya Mungu na ni nani anayekwambia: Nipatie maji ninywe, ungalikwisha mwomba, naye angekupa maji yaliyo hai."
11The woman says to him, Sir, thou hast nothing to draw with, and the well is deep: whence then hast thou the living water?
11Huyo mama akasema, "Mheshimiwa, wewe huna chombo cha kutekea maji, nacho kisima ni kirefu; utapata wapi maji yaliyo hai?
12Art thou greater than our father Jacob, who gave us the well, and drank of it himself, and his sons, and his cattle?
12Au, labda wewe wajifanya mkuu kuliko babu yetu Yakobo? Yeye alitupa sisi kisima hiki; na yeye mwenyewe, watoto wake na mifugo yake walikunywa maji ya kisima hiki."
13Jesus answered and said to her, Every one who drinks of this water shall thirst again;
13Yesu akamjibu, "Kila anayekunywa maji haya ataona kiu tena.
14but whosoever drinks of the water which I shall give him shall never thirst for ever, but the water which I shall give him shall become in him a fountain of water, springing up into eternal life.
14Lakini atakayekunywa maji nitakayompa mimi, hataona kiu milele. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji ya uzima na kumpatia uzima wa milele."
15The woman says to him, Sir, give me this water, that I may not thirst nor come here to draw.
15Huyo mwanamke akamwambia, "Mheshimiwa, nipe maji hayo ili nisione kiu tena; nisije tena mpaka hapa kuteka maji."
16Jesus says to her, Go, call thy husband, and come here.
16Yesu akamwambia, "Nenda ukamwite mumeo uje naye hapa."
17The woman answered and said, I have not a husband. Jesus says to her, Thou hast well said, I have not a husband;
17Huyo mwanamke akamwambia, "Mimi sina mume." Yesu akamwambia, "Umesema kweli, kwamba huna mume.
18for thou hast had five husbands, and he whom now thou hast is not thy husband: this thou hast spoken truly.
18Maana umekuwa na waume watano, na huyo unayeishi naye sasa si mume wako. Hapo umesema kweli."
19The woman says to him, Sir, I see that thou art a prophet.
19Huyo Mwanamke akamwambia, "Mheshimiwa, naona ya kuwa wewe u nabii.
20Our fathers worshipped in this mountain, and ye say that in Jerusalem is the place where one must worship.
20Babu zetu waliabudu juu ya mlima huu, lakini ninyi mwasema kwamba mahali pa kumwabudu Mungu ni kule Yerusalemu."
21Jesus says to her, Woman, believe me, [the] hour is coming when ye shall neither in this mountain nor in Jerusalem worship the Father.
21Yesu akamwambia, "Niamini; wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba juu ya mlima huu, wala kule Yerusalemu.
22Ye worship ye know not what; we worship what we know, for salvation is of the Jews.
22Ninyi Wasamaria mnamwabudu yule msiyemjua, lakini sisi tunamjua huyo tunayemwabudu, kwa maana wokovu unatoka kwa Wayahudi.
23But [the] hour is coming and now is, when the true worshippers shall worship the Father in spirit and truth; for also the Father seeks such as his worshippers.
23Lakini wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wanaoabudu kweli, watamwabudu Baba kwa nguvu ya Roho; watu wanaomwabudu hivyo ndio Baba anaotaka.
24God [is] a spirit; and they who worship him must worship [him] in spirit and truth.
24Mungu ni Roho, na watu wataweza tu kumwabudu kweli kwa nguvu ya Roho wake."
25The woman says to him, I know that Messias is coming, who is called Christ; when *he* comes he will tell us all things.
25Huyo mama akamwambia, "Najua kwamba Masiha, aitwaye Kristo, anakuja. Atakapokuja atatujulisha kila kitu."
26Jesus says to her, I who speak to thee am [he].
26Yesu akamwambia, "Mimi ninayesema nawe, ndiye."
27And upon this came his disciples, and wondered that he spoke with a woman; yet no one said, What seekest thou? or, Why speakest thou with her?
27Hapo wanafunzi wake wakarudi, wakastaajabu sana kuona anaongea na mwanamke. Lakini hakuna mtu aliyesema: "Unataka nini?" au, "Kwa nini unaongea na mwanamke?"
28The woman then left her waterpot and went away into the city, and says to the men,
28Huyo mama akauacha mtungi wake pale, akaenda mjini na kuwaambia watu,
29Come, see a man who told me all things I had ever done: is not he the Christ?
29"Njoni mkamwone mtu aliyeniambia mambo yote niliyotenda! Je, yawezekana kuwa yeye ndiye Kristo?"
30They went out of the city and came to him.
30Watu wakatoka mjini, wakamwendea Yesu.
31But meanwhile the disciples asked him saying, Rabbi, eat.
31Wakati huohuo wanafunzi wake walikuwa wanamsihi Yesu: "Mwalimu, ule chakula."
32But he said to them, I have food to eat which ye do not know.
32Lakini Yesu akawaambia, "Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi."
33The disciples therefore said to one another, Has any one brought him [anything] to eat?
33Wanafunzi wake wakaulizana, "Je, kuna mtu aliyemletea chakula?"
34Jesus says to them, My food is that I should do the will of him that has sent me, and that I should finish his work.
34Yesu akawaambia, "Chakula changu ni kufanya anachotaka yule aliyenituma na kuitimiza kazi yake.
35Do not ye say, that there are yet four months and the harvest comes? Behold, I say to you, Lift up your eyes and behold the fields, for they are already white to harvest.
35Ninyi mwasema: Bado miezi minne tu, na wakati wa mavuno utafika! Lakini mimi nawaambieni, yatazameni mashamba; mazao yako tayari kuvunwa.
36He that reaps receives wages and gathers fruit unto life eternal, that both he that sows and he that reaps may rejoice together.
36Mvunaji anapata mshahara wake, na anakusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele; hivyo mpandaji na mvunaji watafurahi pamoja.
37For in this is [verified] the true saying, It is one who sows and another who reaps.
37Kwa sababu hiyo msemo huu ni kweli: Mmoja hupanda na mwingine huvuna.
38I have sent you to reap that on which ye have not laboured; others have laboured, and ye have entered into their labours.
38Mimi nimewatuma mkavune mavuno ambayo hamkuyatolea jasho, wengine walifanya kazi, lakini ninyi mnafaidika kutokana na jasho lao."
39But many of the Samaritans of that city believed on him because of the word of the woman who bore witness, He told me all things that I had ever done.
39Wasamaria wengi wa kijiji kile waliamini kwa sababu ya maneno aliyosema huyo mama: "Ameniambia mambo yote niliyofanya."
40When therefore the Samaritans came to him they asked him to abide with them, and he abode there two days.
40Wasamaria walimwendea Yesu wakamwomba akae nao; naye akakaa hapo siku mbili.
41And more a great deal believed on account of his word;
41Watu wengi zaidi walimwamini kwa sababu ya ujumbe wake.
42and they said to the woman, [It is] no longer on account of thy saying that we believe, for we have heard him ourselves, and we know that this is indeed the Saviour of the world.
42Wakamwambia yule mama, "Sisi hatuamini tu kwa sababu ya maneno yako; sisi wenyewe tumesikia, na tunajua kwamba huyu ndiye kweli Mwokozi wa ulimwengu."
43But after the two days he went forth thence and went away into Galilee,
43Baada ya siku mbili Yesu aliondoka hapo, akaenda Galilaya.
44for Jesus himself bore witness that a prophet has no honour in his own country.
44Maana Yesu mwenyewe alisema waziwazi kwamba, "Nabii hapati heshima katika nchi yake."
45When therefore he came into Galilee, the Galileans received him, having seen all that he had done in Jerusalem during the feast, for they also went to the feast.
45Basi, alipofika Galilaya, Wagalilaya wengi walimkaribisha. Maana nao pia walikuwa kwenye sikukuu ya Pasaka, wakayaona mambo yote Yesu aliyotenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu hiyo.
46He came therefore again to Cana of Galilee, where he made the water wine. And there was a certain courtier in Capernaum whose son was sick.
46Yesu alifika tena huko mjini Kana, mkoani Galilaya, mahali alipogeuza maji kuwa divai. Kulikuwa na ofisa mmoja aliyekuwa na mtoto mgonjwa huko Kafarnaumu.
47He, having heard that Jesus had come out of Judaea into Galilee, went to him and asked [him] that he would come down and heal his son, for he was about to die.
47Basi, huyo ofisa aliposikia kuwa Yesu alikuwa ametoka Yudea na kufika Galilaya, alimwendea akamwomba aende kumponya mtoto wake aliyekuwa mgonjwa mahututi.
48Jesus therefore said to him, Unless ye see signs and wonders ye will not believe.
48Yesu akamwambia, "Msipoona ishara na maajabu hamtaamini!"
49The courtier says to him, Sir, come down ere my child die.
49Huyo ofisa akamwambia, "Mheshimiwa, tafadhali twende kabla mwanangu hajafa."
50Jesus says to him, Go, thy son lives. And the man believed the word which Jesus said to him, and went his way.
50Yesu akamwambia, "Nenda tu, mwanao yu mzima." Huyo mtu akaamini maneno ya Yesu, akaenda zake.
51But already, as he was going down, his servants met him and brought [him] word saying, Thy child lives.
51Alipokuwa bado njiani, watumishi wake walikutana naye, wakamwambia kwamba mwanawe alikuwa mzima.
52He inquired therefore from them the hour at which he got better. And they said to him, Yesterday at the seventh hour the fever left him.
52Naye akawauliza saa mtoto alipopata nafuu; nao wakamwambia, "Jana saa saba mchana, homa ilimwacha."
53The father therefore knew that [it was] in that hour in which Jesus said to him, Thy son lives; and he believed, himself and his whole house.
53Huyo baba akakumbuka kwamba ilikuwa ni saa ileile ambapo Yesu alimwambia: "Mwanao yu mzima." Basi, yeye akaamini pamoja na jamaa yake yote.
54This second sign again did Jesus, being come out of Judaea into Galilee.
54Hii ilikuwa ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipokuwa anatoka Yudea kwenda Galilaya.