Darby's Translation

Swahili: New Testament

John

7

1And after these things Jesus walked in Galilee, for he would not walk in Judaea, because the Jews sought to kill him.
1Baada ya hayo, Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya. Hakutaka kutembea mkoani Yudea kwa sababu viongozi wa Wayahudi walikuwa wanataka kumwua.
2Now the tabernacles, the feast of the Jews, was near.
2Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
3His brethren therefore said to him, Remove hence and go into Judaea, that thy disciples also may see thy works which thou doest;
3Basi ndugu zake wakamwambia, "Ondoka hapa uende Yudea ili wanafunzi wako wazione kazi unazozifanya.
4for no one does anything in secret and himself seeks to be [known] in public. If thou doest these things, manifest thyself to the world:
4Mtu hafanyi mambo kwa siri kama anataka kujulikana kwa watu. Maadam unafanya mambo haya, basi, jidhihirishe kwa ulimwengu."
5for neither did his brethren believe on him.
5(Hata ndugu zake hawakumwamini!)
6Jesus therefore says to them, My time is not yet come, but your time is always ready.
6Basi, Yesu akawaambia, "Wakati wangu ufaao haujafika bado. Lakini kwenu ninyi kila wakati unafaa.
7The world cannot hate you, but me it hates, because I bear witness concerning it that its works are evil.
7Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, lakini mimi wanichukia kwa sababu mimi nauambia wazi kwamba matendo yake ni maovu.
8Ye, go ye up to this feast. I go not up to this feast, for *my* time is not yet fulfilled.
8Ninyi nendeni kwenye sikukuu hiyo. Mimi siendi kwenye sikukuu hiyo, maana saa yangu ifaayo haijafika."
9Having said these things to them he abode in Galilee.
9Alisema hayo kisha akabaki huko Galilaya.
10But when his brethren had gone up, then he himself also went up to the feast, not openly, but as in secret.
10Baada ya ndugu zake kwenda kwenye sikukuu, Yesu naye alikwenda, lakini hakuenda kwa hadhara bali kwa siri.
11The Jews therefore sought him at the feast, and said, Where is he?
11Viongozi wa Wayahudi walikuwa wanamtafuta kwenye sikukuu hiyo; Wakauliza: "Yuko wapi?"
12And there was much murmuring concerning him among the crowds. Some said, He is [a] good [man]; others said, No; but he deceives the crowd.
12Kulikuwa na minong'ono mingi katika umati wa watu. Baadhi yao walisema, "Ni mtu mwema." Wengine walisema, "La! Anawapotosha watu."
13However, no one spoke openly concerning him on account of [their] fear of the Jews.
13Hata hivyo hakuna mtu aliyethubutu kusema, habari zake hadharani kwa kuwaogopa viongozi wa Wayahudi.
14But when it was now the middle of the feast, Jesus went up into the temple and taught.
14Sikukuu hiyo ilipofikia katikati, Yesu naye alikwenda Hekaluni, akaanza kufundisha.
15The Jews therefore wondered, saying, How knows this [man] letters, having never learned?
15Basi, Wayahudi wakashangaa na kusema "Mtu huyu amepataje elimu naye hakusoma shuleni?"
16Jesus therefore answered them and said, My doctrine is not mine, but [that] of him that has sent me.
16Hapo Yesu akawajibu, "Mafundisho ninayofundisha si yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
17If any one desire to practise his will, he shall know concerning the doctrine, whether it is of God, or [that] I speak from myself.
17Mtu anayependa kufanya yale anayotaka Mungu, atajua kama mafundisho yangu yametoka kwa Mungu, au mimi najisemea tu mwenyewe.
18He that speaks from himself seeks his own glory; but he that seeks the glory of him that has sent him, he is true, and unrighteousness is not in him.
18Yeye anayejisemea tu mwenyewe anatafuta sifa yake mwenyewe; lakini anayetafuta sifa ya yule aliyemtuma, huyo ni mwaminifu, na ndani yake hamna uovu wowote.
19Has not Moses given you the law, and no one of you practises the law? Why do ye seek to kill me?
19Je, Mose hakuwapeni Sheria? Hata hivyo, hakuna hata mmoja wenu anayeishika Sheria. Kwa nini mnataka kuniua?"
20The crowd answered [and said], Thou hast a demon: who seeks to kill thee?
20Hapo watu wakamjibu, "Una wazimu wewe! Nani anataka kukuua?"
21Jesus answered and said to them, I have done one work, and ye all wonder.
21Yesu akawajibu, "Kuna jambo moja nililofanya, nanyi mnalistaajabia.
22Therefore Moses gave you circumcision (not that it is of Moses, but of the fathers), and ye circumcise a man on sabbath.
22Mose aliwapeni ile desturi ya kutahiri. (Si kwamba desturi hiyo ilitoka kwa Mose, bali ilitoka kwa mababu). Sasa ninyi humtahiri mtu hata siku ya Sabato.
23If a man receives circumcision on sabbath, that the law of Moses may not be violated, are ye angry with me because I have made a man entirely sound on sabbath?
23Ikiwa basi, mtu hutahiriwa hata siku ya Sabato kusudi Sheria ya Mose isivunjwe, mbona mnanikasirikia kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya Sabato?
24Judge not according to sight, but judge righteous judgment.
24Msihukumu mambo kwa nje tu; toeni hukumu ya haki."
25Some therefore of those of Jerusalem said, Is not this he whom they seek to kill?
25Baadhi ya watu wa Yerusalemu walisema, "Je, yule mtu wanayemtafuta wamuue si huyu?
26and behold, he speaks openly, and they say nothing to him. Have the rulers then indeed recognised that this is the Christ?
26Tazameni sasa! Anawaonya hadharani, wala hakuna mtu anayemwambia hata neno. Je, yawezekana kuwa viongozi wametambua kweli kwamba huyu ndiye Kristo?
27But [as to] this [man] we know whence he is. Now [as to] the Christ, when he comes, no one knows whence he is.
27Kristo atakapokuja hakuna mtu atakayejua mahali alikotoka, lakini sisi tunajua alikotoka mtu huyu!"
28Jesus therefore cried out in the temple, teaching and saying, Ye both know me and ye know whence I am; and I am not come of myself, but he that sent me is true, whom ye do not know.
28Basi, Yesu alipokuwa anafundisha Hekaluni alipaaza sauti na kusema, "Ati mnanijua; hata nilikotoka mnakujua! Hata hivyo, sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe; ila yeye aliyenituma mimi ni wa kweli, nanyi hamumjui.
29I know him, because I am from him, and *he* has sent me.
29Lakini mimi namjua kwa sababu nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma."
30They sought therefore to take him; and no one laid his hand upon him, because his hour had not yet come.
30Basi, watu wakataka kumtia nguvuni, lakini hakuna mtu aliyethubutu kumkamata kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
31But many of the crowd believed on him, and said, Will the Christ, when he comes, do more signs than those which this [man] has done?
31Wengi katika ule umati wa watu walimwamini, wakasema, "Je, Kristo akija atafanya ishara kubwa zaidi kuliko alizozifanya huyu?"
32The Pharisees heard the crowd murmuring these things concerning him, and the Pharisees and the chief priests sent officers that they might take him.
32Mafarisayo waliwasikia watu wakinong'ona maneno hayo juu ya Yesu. Basi, wao pamoja na makuhani wakuu wakawatuma walinzi wamtie nguvuni.
33Jesus therefore said, Yet a little while I am with you, and I go to him that has sent me.
33Yesu akasema, "Bado niko nanyi kwa muda mfupi, kisha nitamwendea yule aliyenituma.
34Ye shall seek me and shall not find [me], and where I am ye cannot come.
34Mtanitafuta lakini hamtaniona, maana pale nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika."
35The Jews therefore said to one another, Where is he about to go that we shall not find him? Is he about to go to the dispersion among the Greeks, and teach the Greeks?
35Viongozi wa Wayahudi wakasema wao kwa wao, "Mtu huyu atakwenda wapi ambapo hatutaweza kumpata? Atakwenda kwa Wayahudi waliotawanyika kati ya Wagiriki, na kuwafundisha Wagiriki?
36What word is this which he said, Ye shall seek me and shall not find [me]; and where I am ye cannot come?
36Ana maana gani anaposema: Mtanitafuta lakini hamtanipata, na mahali nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika?"
37In the last, the great day of the feast, Jesus stood and cried saying, If any one thirst, let him come to me and drink.
37Siku ya mwisho ya sikukuu hiyo ilikuwa siku maalum. Yesu alisimama, akasema kwa sauti kubwa, "Aliye na kiu na aje kwangu anywe.
38He that believes on me, as the scripture has said, out of his belly shall flow rivers of living water.
38Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: Anayeniamini mimi, mito ya maji yenye uzima itatiririka kutoka moyoni mwake!"
39But this he said concerning the Spirit, which they that believed on him were about to receive; for [the] Spirit was not yet, because Jesus had not yet been glorified.
39(Alisema hayo kumhusu Roho ambaye wale waliomwamini yeye watampokea. Wakati huo Roho alikuwa hajafika kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.)
40[Some] out of the crowd therefore, having heard this word, said, This is truly the prophet.
40Baadhi ya watu katika ule umati walisikia maneno hayo, wakasema, "Kweli mtu huyu ndiye yule nabii!"
41Others said, This is the Christ. Others said, Does then the Christ come out of Galilee?
41Wengine wakasema, "Huyu ndiye Kristo!" Lakini wengine walisema, "Je, yawezekana Kristo akatoka Galilaya?
42Has not the scripture said that the Christ comes of the seed of David, and from the village of Bethlehem, where David was?
42Maandiko Matakatifu yasemaje? Yanasema: Kristo atatoka katika ukoo wa Daudi, na atazaliwa Bethlehemu, mji wa Daudi!"
43There was a division therefore in the crowd on account of him.
43Basi, kukatokea mafarakano juu yake katika ule umati wa watu.
44But some of them desired to take him, but no one laid hands upon him.
44Baadhi ya watu walitaka kumtia nguvuni lakini hakuna aliyejaribu kumkamata.
45The officers therefore came to the chief priests and Pharisees, and they said to them, Why have ye not brought him?
45Kisha wale walinzi wakarudi kwa makuhani wakuu na Mafarisayo; nao wakawauliza, "Kwa nini hamkumleta?"
46The officers answered, Never man spoke thus, as this man [speaks].
46Walinzi wakawajibu, "Hakuna mtu aliyepata kamwe kusema kama asemavyo mtu huyu!"
47The Pharisees therefore answered them, Are ye also deceived?
47Mafarisayo wakawauliza, "Je, nanyi pia mmedanganyika?
48Has any one of the rulers believed on him, or of the Pharisees?
48Je, mmekwisha mwona hata mmoja wa viongozi wa watu, au mmoja wa Mafarisayo aliyemwamini?
49But this crowd, which does not know the law, are accursed.
49Lakini umati huu haujui Sheria ya Mose; umelaaniwa!"
50Nicodemus says to them (being one of themselves),
50Mmoja wao alikuwa Nikodemo ambaye hapo awali alikuwa amemwendea Yesu. Basi, yeye akawaambia,
51Does our law judge a man before it have first heard from himself, and know what he does?
51"Je, Sheria yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza na kujua anafanya nini?"
52They answered and said to him, Art thou also of Galilee? Search and look, that no prophet arises out of Galilee.
52Nao wakamjibu, "Je, wewe pia umetoka Galilaya? Haya, kayachunguze Maandiko Matakatifu nawe utaona kwamba Galilaya hakutoki kamwe nabii!"
53And every one went to his home.
53Basi, wote wakaondoka, kila mtu akaenda zake;