Darby's Translation

Swahili: New Testament

Luke

6

1And it came to pass on [the] second-first sabbath, that he went through cornfields, and his disciples were plucking the ears and eating [them], rubbing [them] in their hands.
1Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano, na wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakaondoa punje zake kwa mikono, wakala.
2But some of the Pharisees said to them, Why do ye what is not lawful to do on the sabbath?
2Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, "Mbona mnafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato?"
3And Jesus answering said to them, Have ye not read so much as this, what David did when he hungered, he and those who were with him,
3Yesu akawajibu, "Je, hamjasoma jinsi alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
4how he entered into the house of God and took the shewbread and ate, and gave to those also who were with him, which it is not lawful that [any] eat, unless the priests alone?
4Yeye aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akachukua ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu, akala na kuwapa wenzake. Kisheria, ni makuhani tu peke yao ndio walioruhusiwa kula mikate hiyo."
5And he said to them, The Son of man is Lord of the sabbath also.
5Hivyo akawaambia, "Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato."
6And it came to pass on another sabbath also that he entered into the synagogue and taught; and there was a man there, and his right hand was withered.
6Siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia katika sunagogi, akafundisha. Mle ndani mlikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
7And the scribes and the Pharisees were watching if he would heal on the sabbath, that they might find something of which to accuse him.
7Walimu wa Sheria na Mafarisayo walitaka kupata kisingizio cha kumshtaki Yesu na hivyo wakawa wanangojea waone kama angemponya mtu siku ya Sabato.
8But *he* knew their thoughts, and said to the man who had the withered hand, Get up, and stand in the midst. And having risen up he stood [there].
8Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, "Inuka, simama katikati." Yule mtu akaenda akasimama katikati.
9Jesus therefore said to them, I will ask you if it is lawful on the sabbath to do good, or to do evil? to save life, or to destroy [it]?
9Kisha Yesu akawaambia, "Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?"
10And having looked around on them all, he said to him, Stretch out thy hand. And he did [so] and his hand was restored as the other.
10Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, "Nyosha mkono wako." Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.
11But *they* were filled with madness, and they spoke together among themselves what they should do to Jesus.
11Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.
12And it came to pass in those days that he went out into the mountain to pray, and he spent the night in prayer to God.
12Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akimwomba Mungu.
13And when it was day he called his disciples, and having chosen out twelve from them, whom also he named apostles:
13Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume:
14Simon, to whom also he gave the name of Peter, and Andrew his brother, [and] James and John, [and] Philip and Bartholomew,
14Simoni (ambaye Yesu alimpa jina Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo na Yohane, Filipo na Bartholomayo,
15[and] Matthew and Thomas, James the [son] of Alphaeus and Simon who was called Zealot,
15Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo na Simoni (aliyeitwa Zelote),
16[and] Judas [brother] of James, and Judas Iscariote, who was also [his] betrayer;
16Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.
17and having descended with them, he stood on a level place, and a crowd of his disciples, and a great multitude of the people from all Judaea and Jerusalem, and the sea coast of Tyre and Sidon, who came to hear him, and to be healed of their diseases;
17Baada ya kushuka mlimani pamoja na mitume, Yesu alisimama mahali palipokuwa tambarare. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati wa watu waliotoka pande zote za Yudea na Yerusalemu na pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walifika kumsikiliza Yesu na kuponywa magonjwa yao.
18and those that were beset by unclean spirits were healed.
18Aliwaponya pia wote waliokuwa wanasumbuliwa na pepo wachafu.
19And all the crowd sought to touch him, for power went out from him and healed all.
19Watu wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa inatoka ndani yake na kuwaponya wote.
20And *he*, lifting up his eyes upon his disciples, said, Blessed [are] ye poor, for yours is the kingdom of God.
20Yesu akawageukia wanafunzi wake, akasema: "Heri ninyi mlio maskini, maana Ufalme wa Mungu ni wenu.
21Blessed ye that hunger now, for ye shall be filled. Blessed ye that weep now, for ye shall laugh.
21Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
22Blessed are ye when men shall hate you, and when they shall separate you [from them], and shall reproach [you], and cast out your name as wicked, for the Son of man's sake:
22"Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
23rejoice in that day and leap for joy, for behold, your reward is great in the heaven, for after this manner did their fathers act toward the prophets.
23Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
24But woe to you rich, for ye have received your consolation.
24Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
25Woe to you that are filled, for ye shall hunger. Woe to you who laugh now, for ye shall mourn and weep.
25Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
26Woe, when all men speak well of you, for after this manner did their fathers to the false prophets.
26Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
27But to you that hear I say, Love your enemies; do good to those that hate you;
27"Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
28bless those that curse you; pray for those who use you despitefully.
28Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
29To him that smites thee on the cheek, offer also the other; and from him that would take away thy garment, forbid not thy body-coat also.
29Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
30To every one that asks of thee, give; and from him that takes away what is thine, ask it not back.
30Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
31And as ye wish that men should do to you, do *ye* also to them in like manner.
31Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.
32And if ye love those that love you, what thank is it to you? for even sinners love those that love them.
32"Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda ninyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.
33And if ye do good to those that do good to you, what thank is it to you? for even sinners do the same.
33Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo!
34And if ye lend to those from whom ye hope to receive, what thank is it to you? [for] even sinners lend to sinners that they may receive the like.
34Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!
35But love your enemies, and do good, and lend, hoping for nothing in return, and your reward shall be great, and ye shall be sons of [the] Highest; for *he* is good to the unthankful and wicked.
35Ila nyinyi wapendeni adui zenu, na kuwatendea mema; kopesheni bila kutazamia malipo, na tuzo lenu litakuwa kubwa, nanyi mtakuwa watoto wa Mungu aliye juu. Kwa maana yeye ni mwema kwa wale wasio na shukrani na walio wabaya.
36Be ye therefore merciful, even as your Father also is merciful.
36Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.
37And judge not, and ye shall not be judged; condemn not, and ye shall not be condemned. Remit, and it shall be remitted to you.
37"Msiwahukumu wengine, nanyi hamtahukumiwa; msiwalaumu wengine, nanyi hamtalaumiwa; wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
38Give, and it shall be given to you; good measure, pressed down, and shaken together, and running over, shall be given into your bosom: for with the same measure with which ye mete it shall be measured to you again.
38Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu."
39And he spoke also a parable to them: Can a blind [man] lead a blind [man]? shall not both fall into [the] ditch?
39Akawaambia mfano huu: "Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwenzake? La! Wote wataanguka shimoni.
40The disciple is not above his teacher, but every one that is perfected shall be as his teacher.
40Mwanafunzi hamshindi mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi akisha hitimu huwa kama mwalimu wake.
41But why lookest thou on the mote which is in the eye of thy brother, but perceivest not the beam which is in thine own eye?
41Unawezaje kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwenzio, usione boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
42or how canst thou say to thy brother, Brother, allow [me], I will cast out the mote that is in thine eye, thyself not seeing the beam that is in thine eye? Hypocrite, cast out first the beam out of thine eye, and then thou shalt see clear to cast out the mote which is in the eye of thy brother.
42Au, unawezaje kumwambia mwenzako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi katika jicho lako, na huku huioni boriti iliyoko katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, na hivyo utaona sawasawa kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilicho katika jicho la ndugu yako.
43For there is no good tree which produces corrupt fruit, nor a corrupt tree which produces good fruit;
43"Mti mwema hauzai matunda mabaya, wala mti mbaya hauzai matunda mazuri.
44for every tree is known by its own fruit, for figs are not gathered from thorns, nor grapes vintaged from a bramble.
44Watu huutambua mti kutokana na matunda yake. Ni wazi kwamba watu hawachumi tini katika michongoma, wala hawachumi zabibu katika mbigili.
45The good man, out of the good treasure of his heart, brings forth good; and the wicked [man] out of the wicked, brings forth what is wicked: for out of the abundance of the heart his mouth speaks.
45Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka katika hazina bora iliyo moyoni mwake; na mtu mbaya hutoa yaliyo mabaya katika hazina mbaya iliyo moyoni mwake, kwa maana mtu huongea kutokana na yale yaliyojaa moyoni mwake.
46And why call ye me, Lord, Lord, and do not the things that I say?
46"Mbona mwaniita Bwana, Bwana, na huku hamtimizi yale ninayosema?
47Every one that comes to me, and hears my words and does them, I will shew you to whom he is like.
47Nitawapeni mfano unaofaa kuonyesha alivyo yeyote yule anayekuja kwangu, akasikia maneno yangu na kuyatimiza:
48He is like a man building a house, who dug and went deep, and laid a foundation on the rock; but a great rain coming, the stream broke upon that house, and could not shake it, for it had been founded on the rock.
48Huyo anafanana na mtu ajengaye nyumba, ambaye amechimba chini na kuweka msingi wake juu ya mwamba; kukatokea mafuriko ya mto, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa imara.
49And he that has heard and not done, is like a man who has built a house on the ground without [a] foundation, on which the stream broke, and immediately it fell, and the breach of that house was great.
49Lakini yeyote anayesikia maneno yangu lakini asifanye chochote, huyo anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo, bila msingi. Mafuriko ya mto yakatokea, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, ikaanguka na kuharibika kabisa!"