Darby's Translation

Swahili: New Testament

Mark

1

1Beginning of the glad tidings of Jesus Christ, Son of God;
1Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
2as it is written in [Isaiah] the prophet, Behold, *I* send my messenger before thy face, who shall prepare thy way.
2Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: "Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie; yeye atakutayarishia njia yako.
3Voice of one crying in the wilderness, Prepare the way of [the] Lord, make his paths straight.
3Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni mapito yake."
4There came John baptising in the wilderness, and preaching [the] baptism of repentance for remission of sins.
4Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba ni lazima watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
5And there went out to him all the district of Judaea, and all they of Jerusalem, and were baptised by him in the river Jordan, confessing their sins.
5Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
6And John was clothed in camel's hair, and a leathern girdle about his loins, and ate locusts and wild honey.
6Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
7And he preached, saying, There comes he that is mightier than I after me, the thong of whose sandals I am not fit to stoop down and unloose.
7Naye alihubiri akisema, "Baada yangu anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.
8*I* indeed have baptised you with water, but *he* shall baptise you with [the] Holy Spirit.
8Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu."
9And it came to pass in those days [that] Jesus came from Nazareth of Galilee, and was baptised by John at the Jordan.
9Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani.
10And straightway going up from the water, he saw the heavens parting asunder, and the Spirit, as a dove, descending upon him.
10Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa.
11And there came a voice out of the heavens: *Thou* art my beloved Son, in thee I have found my delight.
11Sauti ikasikika kutoka mbinguni: "Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe."
12And immediately the Spirit drives him out into the wilderness.
12Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani,
13And he was in the wilderness forty days tempted by Satan, and was with the wild beasts; and the angels ministered to him.
13akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamtumikia.
14But after John was delivered up, Jesus came into Galilee preaching the glad tidings of the kingdom of God,
14Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema,
15and saying, The time is fulfilled and the kingdom of God has drawn nigh; repent and believe in the glad tidings.
15"Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!"
16And walking by the sea of Galilee, he saw Simon, and Andrew, [Simon's] brother, casting out a net in the sea, for they were fishers.
16Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu.
17And Jesus said to them, Come after me, and I will make you become fishers of men;
17Yesu akawaambia, "Nifuateni nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu."
18and straightway leaving their trawl-nets they followed him.
18Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
19And going on thence a little, he saw James the [son] of Zebedee, and John his brother, and these [were] in the ship repairing the trawl-nets;
19Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
20and straightway he called them; and leaving their father Zebedee in the ship with the hired servants, they went away after him.
20Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
21And they go into Capernaum. And straightway on the sabbath he entered into the synagogue and taught.
21Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika Sunagogi, akaanza kufundisha.
22And they were astonished at his doctrine, for he taught them as having authority, and not as the scribes.
22Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama walimu wao wa Sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.
23And there was in their synagogue a man [possessed] by an unclean spirit, and he cried out
23Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu,
24saying, Eh! what have we to do with thee, Jesus, Nazarene? Art thou come to destroy us? I know thee who thou art, the holy one of God.
24akapaaza sauti, "Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: wewe ni Mtakatifu wa Mungu!"
25And Jesus rebuked him, saying, Hold thy peace and come out of him.
25Yesu akamkemea, "Nyamaza! Mtoke mtu huyu."
26And the unclean spirit, having torn him, and uttered a cry with a loud voice, came out of him.
26Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.
27And all were amazed, so that they questioned together among themselves, saying, What is this? what new doctrine is this? for with authority he commands even the unclean spirits, and they obey him.
27Watu wote wakashangaa, wakaulizana, "Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!"
28And his fame went out straightway into the whole region of Galilee around.
28Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika wilaya ya Galilaya.
29And straightway going out of the synagogue, they came with James and John into the house of Simon and Andrew.
29Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.
30And the mother-in-law of Simon lay in a fever. And straightway they speak to him about her.
30Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.
31And he went up to [her] and raised her up, having taken her by the hand, and straightway the fever left her, and she served them.
31Yesu akamwendea huyo mama, akamshika mkono, akamwinua. Na ile homa ikamwacha, akaanza kuwatumikia.
32But evening being come, when the sun had gone down, they brought to him all that were suffering, and those possessed by demons;
32Jioni, jua lilipokwisha tua, wakamletea Yesu wagonjwa wote na watu waliopagawa na pepo.
33and the whole city was gathered together at the door.
33Watu wote wa mji ule wakakusanyika nje ya mlango.
34And he healed many suffering from various diseases; and he cast out many demons, and did not suffer the demons to speak because they knew him.
34Naye Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa mbalimbali; aliwafukuza pepo wengi, lakini hakuwaruhusu kusema kitu maana walikuwa wanamjua yeye ni nani.
35And rising in the morning long before day, he went out and went away into a desert place, and there prayed.
35Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
36And Simon and those with him went after him:
36Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
37and having found him, they say to him, All seek thee.
37Walipomwona wakamwambia, "Kila mtu anakutafuta."
38And he says to them, Let us go elsewhere into the neighbouring country towns, that I may preach there also, for for this purpose am I come forth.
38Yesu akawaambia, "Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo."
39And he was preaching in their synagogues in the whole of Galilee, and casting out demons.
39Basi, akaenda kila mahali Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
40And there comes to him a leper, beseeching him, and falling on his knees to him, and saying to him, If thou wilt thou canst cleanse me.
40Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba, "Ukitaka, waweza kunitakasa!"
41But Jesus, moved with compassion, having stretched out his hand, touched him, and says to him, I will, be thou cleansed.
41Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, "Nataka, takasika!"
42And as he spoke straightway the leprosy left him, and he was cleansed.
42Mara ukoma ukamwacha mtu huyo, akatakasika.
43And having sharply charged him, he straightway sent him away,
43Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwonya vikali,
44and says to him, See thou say nothing to any one, but go, shew thyself to the priest, and offer for thy cleansing what Moses ordained, for a testimony to them.
44"Usimwambie mtu yeyote jambo hili, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani; kisha utoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona."
45But he, having gone forth, began to proclaim [it] much, and to spread the matter abroad, so that he could no longer enter openly into the city, but was without in desert places, and they came to him from every side.
45Lakini huyo mtu akaenda, akaanza kueneza habari hiyo kila mahali na kusema mambo mengi hata Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote waziwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande.