1And he entered again into the synagogue; and there was there a man having his hand dried up.
1Yesu aliingia tena katika sunagogi na mle ndani mlikuwa na mtu aliyekuwa na mkono uliopooza.
2And they watched him if he would heal him on the sabbath, that they might accuse him.
2Humo baadhi ya watu walimngojea amponye mtu huyo siku ya sabato ili wapate kumshtaki.
3And he says to the man who had his hand dried up, Rise up [and come] into the midst.
3Yesu akamwambia huyo mtu aliyekuwa na mkono uliopooza, "Njoo hapa katikati."
4And he says to them, Is it lawful on the sabbath to do good or to do evil, to save life or to kill? But they were silent.
4Kisha, akawauliza, "Je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuua?" Lakini wao hawakusema neno.
5And looking round upon them with anger, distressed at the hardening of their heart, he says to the man, Stretch out thy hand. And he stretched [it] out, and his hand was restored.
5Hapo akawatazama wote kwa hasira, akaona huzuni kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao. Kisha akamwambia huyo mtu, "Nyosha mkono wako!" Naye akaunyosha mkono wake, ukawa mzima tena.
6And the Pharisees going out straightway with the Herodians took counsel against him, how they might destroy him.
6Mara Mafarisayo wakatoka nje, wakafanya shauri pamoja na watu wa kikundi cha Herode jinsi ya kumwangamiza Yesu.
7And Jesus withdrew with his disciples to the sea; and a great multitude from Galilee followed him, and from Judaea,
7Yesu aliondoka hapo pamoja na wanafunzi wake, akaenda kando ya ziwa, na umati wa watu ukamfuata. Watu hao walikuwa wametoka Yerusalemu, Yudea,
8and from Jerusalem, and from Idumaea and beyond the Jordan; and they of around Tyre and Sidon, a great multitude, having heard what things he did, came to him.
8Idumea, ng'ambo ya mto Yordani, Tiro na Sidoni. Watu hao wengi walimwendea Yesu kwa sababu ya kusikia mambo mengi aliyokuwa ameyatenda.
9And he spoke to his disciples, in order that a little ship should wait upon him on account of the crowd, that they might not press upon him.
9Yesu akawaambia wanafunzi wake wamtayarishie mashua moja, ili umati wa watu usije ukamsonga.
10For he healed many, so that they beset him that they might touch him, as many as had plagues.
10Alikuwa amewaponya watu wengi, na wagonjwa wote wakawa wanamsonga ili wapate kumgusa.
11And the unclean spirits, when they beheld him, fell down before him, and cried saying, *Thou* art the Son of God.
11Na watu waliokuwa wamepagawa na pepo wachafu walipomwona, walijitupa chini mbele yake na kupaaza sauti, "Wewe ni Mwana wa Mungu!"
12And he rebuked them much, that they might not make him manifest.
12Lakini Yesu akawaamuru kwa ukali wasimjulishe kwa watu.
13And he goes up into the mountain, and calls whom he himself would, and they went to him.
13Yesu alipanda kilimani, akawaita wale aliowataka. Basi, wakamwendea,
14And he appointed twelve that they might be with him, and that he might send them to preach,
14naye akawateua watu kumi na wawili ambao aliwaita mitume, wakae naye, awatume kuhubiri
15and to have power [to heal diseases, and] to cast out demons.
15na wawe na mamlaka ya kuwafukuza pepo.
16And he gave to Simon the surname of Peter;
16Basi, hao kumi na wawili walioteuliwa ndio hawa: Simoni (ambaye Yesu alimpa jina, Petro),
17and James the [son] of Zebedee, and John the brother of James, and he gave them the surname of Boanerges, that is, Sons of thunder;
17Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo (Yesu aliwapa hawa ndugu wawili jina Boanerge, maana yake "wanangurumo"),
18and Andrew, and Philip, and Bartholomew, and Matthew, and Thomas, and James the [son] of Alphaeus, and Thaddaeus, and Simon the Cananaean,
18Andrea na Filipo, Batholomayo, Mathayo, Thoma, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkanani na
19and Judas Iscariote, who also delivered him up. And they come to [the] house.
19Yuda Iskarioti ambaye alimsaliti Yesu.
20And again a crowd comes together, so that they cannot even eat bread.
20Kisha Yesu alikwenda nyumbani. Umati wa watu ukakusanyika tena, hata Yesu na wafuasi wake wasiweze kupata nafasi ya kula chakula.
21And his relatives having heard [of it] went out to lay hold on him, for they said, He is out of his mind.
21Basi, watu wa jamaa yake walipopata habari hiyo wakatoka kwenda kumchukua maana walikuwa wanasema kwamba amepatwa na wazimu.
22And the scribes who had come down from Jerusalem said, He has Beelzebub, and, By the prince of the demons he casts out demons.
22Nao walimu wa Sheria waliokuwa wametoka Yerusalemu, wakasema, "Ana Beelzebuli! Tena, anawafukuza pepo kwa nguvu ya mkuu wa pepo."
23And having called them to [him], he said to them in parables, How can Satan cast out Satan?
23Hapo Yesu akawaita, akawaambia kwa mifano, "Shetani anawezaje kumfukuza Shetani?
24And if a kingdom has become divided against itself, that kingdom cannot subsist.
24Ikiwa utawala mmoja umegawanyika makundimakundi yanayopigana, utawala huo hauwezi kudumu.
25And if a house has become divided against itself, that house cannot subsist.
25Tena, ikiwa jamaa moja imegawanyika makundimakundi yanayopingana, jamaa hiyo itaangamia.
26And if Satan rise up against himself, and is divided, he cannot subsist, but has an end.
26Ikiwa basi, utawala wa Shetani umegawanyika vikundivikundi hauwezi kudumu, bali utaangamia kabisa.
27But no one can, having entered into his house, plunder the goods of the strong [man] unless he first bind the strong [man], and then he will plunder his house.
27"Hakuna mtu awezaye kuivamia nyumba ya mtu mwenye nguvu na kumnyang'anya mali yake, isipokuwa kwanza amemfunga huyo mtu mwenye nguvu; hapo ndipo atakapoweza kumnyang'anya mali yake.
28Verily I say unto you, that all sins shall be forgiven to the sons of men, and all the injurious speeches [with] which they may speak injuriously;
28"Kweli nawaambieni, watu watasamehewa dhambi zao zote na kufuru zao zote;
29but whosoever shall speak injuriously against the Holy Spirit, to eternity has no forgiveness; but lies under the guilt of an everlasting sin;
29lakini anayesema mabaya dhidi ya Roho Mtakatifu, hatasamehewa kamwe; ana hatia ya dhambi ya milele."
30-- because they said, He has an unclean spirit.
30(Yesu alisema hivyo kwa sababu walikuwa wanasema, "Ana pepo mchafu.")
31And his brethren and his mother come, and standing without sent to him calling him.
31Mama yake Yesu na ndugu zake walifika hapo, wakasimama nje, wakampelekea ujumbe kutaka kumwona.
32And a crowd sat around him. And they said to him, Behold, thy mother and thy brethren seek thee without.
32Umati wa watu ulikuwa umekaa hapo kumzunguka. Basi, wakamwambia, "Mama yako na ndugu zako wako nje, wanataka kukuona."
33And he answered them, saying, Who is my mother or my brethren?
33Yesu akawaambia, "Mama yangu na ndugu zangu ni kina nani?"
34And looking around in a circuit at those that were sitting around him, he says, Behold my mother and my brethren:
34Hapo akawatazama watu waliokuwa wamemzunguka, akasema, "Tazameni! Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu.
35for whosoever shall do the will of God, *he* is my brother, and sister, and mother.
35Mtu yeyote anayefanya anayotaka Mungu, huyo ndiye kaka yangu, dada yangu na mama yangu."