Darby's Translation

Swahili: New Testament

Mark

5

1And they came to the other side of the sea, to the country of the Gadarenes.
1Basi, wakafika katika nchi ya Wagerase, ng'ambo ya ziwa.
2And immediately on his going out of the ship there met him out of the tombs a man possessed by an unclean spirit,
2Mara tu Yesu aliposhuka mashuani, mtu mmoja aliyepagawa na pepo mchafu alitoka makaburini, akakutana naye.
3who had his dwelling in the tombs; and no one was able to bind him, not even with chains;
3Mtu huyo alikuwa akiishi makaburini wala hakuna mtu aliyeweza tena kumfunga kwa minyororo.
4because he had been often bound with fetters and chains, and the chains had been torn asunder by him, and the fetters were shattered; and no one was able to subdue him.
4Mara nyingi walimfunga kwa pingu na minyororo lakini kila mara aliweza kuikata hiyo minyororo na kuzivunja hizo pingu, wala hakuna mtu aliyeweza kumzuia.
5And continually night and day, in the tombs and in the mountains, he was crying and cutting himself with stones.
5Mchana na usiku alikaa makaburini na milimani akipaaza sauti na kujikatakata kwa mawe.
6But seeing Jesus from afar off, he ran and did him homage,
6Alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia, akamwinamia
7and crying with a loud voice he says, What have I to do with thee, Jesus, Son of the Most High God? I adjure thee by God, torment me not.
7akisema kwa sauti kubwa, "Una shauri gani nami, wewe Yesu Mwana wa Mungu aliye juu? Kwa jina la Mungu, nakusihi usinitese!"
8For he said to him, Come forth, unclean spirit, out of the man.
8(Alisema hivyo kwa kuwa Yesu alikuwa amemwambia, "Pepo mchafu, mtoke mtu huyu.")
9And he asked him, What is thy name? And he says to him, Legion is my name, because we are many.
9Basi, Yesu akamwuliza, "Jina lako nani?" Naye akajibu, "Jina langu ni Jeshi, maana sisi tu wengi."
10And he besought him much that he would not send them away out of the country.
10Kisha akamsihi Yesu asiwafukuze hao pepo katika nchi ile.
11Now there was there just at the mountain a great herd of swine feeding;
11Kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe malishoni kwenye mteremko wa mlima.
12and they besought him, saying, Send us into the swine that we may enter into them.
12Basi, hao pepo wakamsihi, "Utupeleke kwa hao nguruwe, tuwaingie."
13And Jesus [immediately] allowed them. And the unclean spirits going out entered into the swine, and the herd rushed down the steep slope, into the sea (about two thousand), and were choked in the sea.
13Naye akawaruhusu. Basi, hao pepo wachafu wakatoka, wakawaingia wale nguruwe. Kundi lote la nguruwe wapatao elfu mbili likaporomoka kwenye ule mteremko mkali mpaka ziwani, likatumbukia majini.
14And those that were feeding them fled and reported it in the city and in the country. And they went out to see what it was that had taken place.
14Wachungaji wa hao nguruwe walikimbia, wakatangaza jambo hilo mjini na mashambani. Watu wakafika kuona yaliyotukia.
15And they come to Jesus, and they see the possessed of demons sitting [and] clothed and sensible, [him] that had had the legion: and they were afraid.
15Wakamwendea Yesu, wakamwona na mtu yuleyule aliyekuwa amepagawa na jeshi la pepo ameketi chini, amevaa nguo na ana akili yake sawa, wakaogopa.
16And they that had seen [it] related to them how it had happened to the [man] possessed by demons, and concerning the swine.
16Watu walishuhudia tukio hilo wakaeleza wengine mambo yaliyompata huyo mtu aliyekuwa amepagawa na pepo na juu ya wale nguruwe.
17And they began to beg him to depart from their coasts.
17Basi, wakaanza kumwomba aondoke katika nchi yao.
18And as he went on board ship, the man that had been possessed by demons besought him that he might be with him.
18Yesu alipokuwa anapanda mashuani, yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo akamwomba amruhusu kwenda naye.
19And he suffered him not, but says to him, Go to thine home to thine own people, and tell them how great things the Lord has done for thee, and has had mercy on thee.
19Lakini Yesu akamkatalia. Badala yake akamwambia, "Nenda nyumbani kwa jamaa yako, ukawaambie mambo yote Bwana aliyokutendea na jinsi alivyokuonea huruma."
20And he went away and began to proclaim in the Decapolis how great things Jesus had done for him; and all wondered.
20Basi, huyo mtu akaenda, akaanza kutangaza huko Dekapoli mambo yote Yesu aliyomtendea; watu wote wakashangaa.
21And Jesus having passed over in the ship again to the other side, a great crowd gathered to him; and he was by the sea.
21Yesu alivukia tena upande wa pili wa ziwa kwa mashua. Umati mkubwa wa watu ukakusanyika mbele yake, naye akawa amesimama kando ya ziwa.
22And [behold] there comes one of the rulers of the synagogue, by name Jairus, and seeing him, falls down at his feet;
22Hapo akaja mmojawapo wa maofisa wa sunagogi, jina lake Yairo. Alipomwona Yesu, akajitupa mbele ya miguu yake,
23and he besought him much, saying, My little daughter is at extremity; [I pray] that thou shouldest come and lay thy hands upon her so that she may be healed, and may live.
23akamsihi akisema, "Binti yangu mdogo ni mgonjwa karibu kufa. Twende tafadhali, ukamwekee mikono yako, apate kupona na kuishi."
24And he went with him, and a large crowd followed him and pressed on him.
24Basi, Yesu akaondoka pamoja naye. Watu wengi sana wakamfuata, wakawa wanamsonga kila upande.
25And a certain woman who had had a flux of blood twelve years,
25Mmojawapo alikuwa mwanamke mwenye ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili.
26and had suffered much under many physicians, and had spent everything she had and had found no advantage from it, but had rather got worse,
26Mwanamke huyo alikuwa amekwisha sumbuka sana kuwaendea waganga wengi. Na ingawa alikuwa amekwisha tumia mali yake yote, hakupata nafuu bali hali yake ilizidi kuwa mbaya.
27having heard concerning Jesus, came in the crowd behind and touched his clothes;
27Alikuwa amesikia habari za Yesu, na hivyo akaupenya msongamano wa watu kutoka nyuma, akagusa vazi lake.
28for she said, If I shall touch but his clothes I shall be healed.
28Alifanya hivyo, maana alijisemea, "Nikigusa tu vazi lake, nitapona."
29And immediately her fountain of blood was dried up, and she knew in her body that she was cured from the scourge.
29Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, akajisikia mwilini mwake kwamba ameponywa ugonjwa wake.
30And immediately Jesus, knowing in himself the power that had gone out of him, turning round in the crowd said, Who has touched my clothes?
30Yesu alitambua mara kwamba nguvu imemtoka. Basi akaugeukia ule umati wa watu, akauliza, "Nani aliyegusa mavazi yangu?"
31And his disciples said to him, Thou seest the crowd pressing on thee, and sayest thou, Who touched me?
31Wanafunzi wake wakamjibu, "Unaona jinsi watu wanavyokusonga; mbona wauliza nani aliyekugusa?"
32And he looked round about to see her who had done this.
32Lakini Yesu akaendelea kutazama amwone huyo aliyefanya hivyo.
33But the woman, frightened and trembling, knowing what had taken place in her, came and fell down before him, and told him all the truth.
33Hapo huyo mwanamke, akifahamu yaliyompata, akajitokeza akitetemeka kwa hofu, akajitupa chini mbele ya Yesu na kusema ukweli wote.
34And he said to her, Daughter, thy faith has healed thee; go in peace, and be well of thy scourge.
34Yesu akamwambia, "Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako."
35While he was yet speaking, they come from the ruler of the synagogue's [house], saying, Thy daughter has died, why troublest thou the teacher any further?
35Yesu alipokuwa bado anaongea, watu walifika kutoka nyumbani kwa yule ofisa wa sunagogi, wakamwambia, "Binti yako amekwisha kufa. Ya nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?"
36But Jesus [immediately], having heard the word spoken, says to the ruler of the synagogue, Fear not; only believe.
36Lakini, bila kujali walichosema, Yesu akamwambia mkuu wa sunagogi, "Usiogope, amini tu."
37And he suffered no one to accompany him save Peter and James, and John the brother of James.
37Wala hakumruhusu mtu yeyote kufuatana naye ila Petro, Yakobo na Yohane nduguye Yakobo.
38And he comes to the house of the ruler of the synagogue, and sees the tumult, and people weeping and wailing greatly.
38Wakafika nyumbani kwa ofisa wa sunagogi naye Yesu akasikia makelele, kilio na maombolezo mengi.
39And entering in he says to them, Why do ye make a tumult and weep? the child has not died, but sleeps.
39Akaingia ndani, akawaambia, "Mbona mnapiga kelele na kulia? Msichana hakufa, amelala tu."
40And they derided him. But he, having put [them] all out, takes with [him] the father of the child, and the mother, and those that were with him, and enters in where the child was lying.
40Lakini wao wakamcheka. Basi, akawaondoa wote nje, akawachukua baba na mama ya huyo msichana na wale wanafunzi wake, wakaingia chumbani alimokuwa huyo msichana.
41And having laid hold of the hand of the child, he says to her, Talitha koumi, which is, interpreted, Damsel, I say to thee, Arise.
41Kisha akamshika mkono, akamwambia, "Talitha, kumi," maana yake, "Msichana, nakwambia, amka!"
42And immediately the damsel arose and walked, for she was twelve years old. And they were astonished with great astonishment.
42Mara msichana akasimama, akaanza kutembea. (Alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili.) Hapo watu wakashangaa kupita kiasi.
43And he charged them much that no one should know this; and he desired that [something] should be given her to eat.
43Yesu akawakataza sana wasimjulishe mtu jambo hilo. Kisha akawaambia wampe huyo msichana chakula.