Darby's Translation

Swahili: New Testament

Matthew

14

1At that time Herod the tetrarch heard of the fame of Jesus,
1Wakati huo, mtawala Herode alisikia sifa za Yesu.
2and said to his servants, This is John the baptist: *he* is risen from the dead, and because of this these works of power display their force in him.
2Basi, akawaambia watumishi wake, "Mtu huyu ni Yohane mbatizaji, amefufuka kutoka wafu; ndiyo maana nguvu za miujiza zinafanya kazi ndani yake."
3For Herod had seized John, and had bound him and put him in prison on account of Herodias the wife of Philip his brother.
3Herode ndiye aliyekuwa amemtia Yohane nguvuni, akamfunga minyororo na kumtia gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo, ndugu yake. Sababu hasa ni
4For John said to him, It is not lawful for thee to have her.
4kwamba alikuwa amemwambia Herode, "Si halali kwako kuishi na huyo mwanamke!"
5And [while] desiring to kill him, he feared the crowd, because they held him for a prophet.
5Herode alitaka kumwua Yohane, lakini aliogopa watu kwa sababu kwao Yohane alikuwa nabii.
6But when Herod's birthday was celebrated, the daughter of Herodias danced before them, and pleased Herod;
6Katika sherehe za sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode, binti ya Herodia alicheza mbele ya wageni. Herode alifurahiwa,
7whereupon he promised with oath to give her whatsoever she should ask.
7hata akaahidi kwa kiapo kumpa huyo msichana chochote atakachoomba.
8But she, being set on by her mother, says, Give me here upon a dish the head of John the baptist.
8Naye, huku akichochewa na mama yake, akaomba, "Nipe papahapa katika sinia kichwa cha Yohane mbatizaji."
9And the king was grieved; but on account of the oaths, and those lying at table with [him], he commanded [it] to be given.
9Mfalme alihuzunika, lakini kwa sababu ya kile kiapo chake na kwa sababu ya wale wageni karamuni, akaamuru apewe.
10And he sent and beheaded John in the prison;
10Basi, Herode akatuma mtu gerezani amkate kichwa Yohane.
11and his head was brought upon a dish, and was given to the damsel, and she carried [it] to her mother.
11Kichwa chake kikaletwa katika sinia, wakampa yule msichana, naye akampelekea mama yake.
12And his disciples came and took the body and buried it, and came and brought word to Jesus.
12Wanafunzi wa Yohane wakaja, wakauchukua mwili wake, wakauzika. Kisha wakaenda kumpasha habari Yesu.
13And Jesus, having heard it, went away thence by ship to a desert place apart. And the crowds having heard [of it] followed him on foot from the cities.
13Yesu alipopata habari hiyo, aliondoka mahali pale kwa mashua, akaenda mahali pa faragha peke yake. Lakini watu walipata habari, wakamfuata kwa miguu toka mijini.
14And going out he saw a great crowd, and was moved with compassion about them, and healed their infirm.
14Basi, aliposhuka pwani, aliona umati mkubwa wa watu, akawaonea huruma, akawaponya wagonjwa wao.
15But when even was come, his disciples came to him saying, The place is desert, and [much of] the [day] time already gone by; dismiss the crowds, that they may go into the villages and buy food for themselves.
15Kulipokuwa jioni, wanafunzi wake walimwendea wakamwambia, "Mahali hapa ni nyikani, na saa zimepita. Basi, uwaage watu ili waende vijijini wakajinunulie chakula."
16But Jesus said to them, They have no need to go: give *ye* them to eat.
16Yesu akawaambia, "Si lazima waende, wapeni ninyi chakula."
17But they say to him, We have not here save five loaves and two fishes.
17Lakini wao wakamwambia, "Tunayo mikate mitano tu na samaki wawili."
18And he said, Bring them here to me.
18Yesu akawaambia, "Nileteeni hapa."
19And having commanded the crowds to recline upon the grass, having taken the five loaves and the two fishes, he looked up to heaven, and blessed: and having broken the loaves, he gave [them] to the disciples, and the disciples [gave them] to the crowds.
19Akawaamuru watu waketi katika nyasi. Kisha akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akamshukuru Mungu. Halafu akaimega hiyo mikate, akawapa wanafunzi wake, nao wakawapa watu.
20And all ate and were filled, and they took up what was over and above of fragments twelve hand-baskets full.
20Watu wote wakala, wakashiba. Kisha wanafunzi wakakusanya mabaki, wakajaza vikapu kumi na viwili.
21But those that had eaten were about five thousand men, besides women and children.
21Jumla ya waliokula ilikuwa wanaume wapatao elfu tano, bila kuhesabu wanawake na watoto.
22And immediately he compelled the disciples to go on board ship, and to go on before him to the other side, until he should have dismissed the crowds.
22Mara, Yesu akawaamuru wanafunzi wake wapande mashua, wamtangulie ng'ambo ya ziwa wakati yeye anawaaga watu.
23And having dismissed the crowds, he went up into the mountain apart to pray. And when even was come, he was alone there,
23Baada ya kuwaaga, alipanda mlimani peke yake kusali. Ilipokuwa jioni, yeye alikuwa huko peke yake,
24but the ship was already in the middle of the sea tossed by the waves, for the wind was contrary.
24na wakati huo ile mashua ilikwishafika karibu katikati ya ziwa, lakini ilikuwa inakwenda mrama kwa sababu upepo ulikuwa unaipinga.
25But in the fourth watch of the night he went off to them, walking on the sea.
25Usiku, karibu na mapambazuko, Yesu aliwaendea wanafunzi akitembea juu ya maji.
26And the disciples, seeing him walking on the sea, were troubled, saying, It is an apparition. And they cried out through fear.
26Wanafunzi wake walipomwona akitembea juu ya maji waliingiwa na hofu, wakasema, "Ni mzimu!" Wakapiga kelele kwa hofu.
27But Jesus immediately spoke to them, saying, Take courage; it is *I*: be not afraid.
27Mara, Yesu akasema nao, "Tulieni, ni mimi. Msiogope!"
28And Peter answering him said, Lord, if it be *thou*, command me to come to thee upon the waters.
28Petro akamwambia, "Bwana, ikiwa ni wewe kweli, amuru nitembee juu ya maji nije kwako."
29And he said, Come. And Peter, having descended from the ship, walked upon the waters to go to Jesus.
29Yesu akasema, "Haya, njoo." Basi, Petro akashuka kutoka ile mashua, akatembea juu ya maji, akamwendea Yesu.
30But seeing the wind strong he was afraid; and beginning to sink he cried out, saying, Lord, save me.
30Lakini alipouona ule upepo, aliogopa, akaanza kuzama; akalia kwa sauti, "Bwana, niokoe!"
31And immediately Jesus stretched out his hand and caught hold of him, and says to him, O thou of little faith, why didst thou doubt?
31Hapo, Yesu akaunyosha mkono wake, akamshika na kumwambia, "Ewe mwenye imani haba! Kwa nini uliona shaka?"
32And when they had gone up into the ship, the wind fell.
32Basi, wakapanda mashuani, na upepo ukatulia.
33But those in the ship came and did homage to him, saying, Truly thou art God's Son.
33Wote waliokuwa ndani ya mashua walimsujudia, wakasema, "Hakika wewe ni Mwana wa Mungu."
34And having crossed over they came to the land of Gennesaret.
34Walivuka ziwa, wakafika nchi ya Genesareti.
35And when the men of that place recognised him, they sent to that whole country around, and they brought to him all that were ill,
35Watu wa huko walipomtambua, wakaeneza habari pote katika sehemu hizo. Basi, wakamletea Yesu wagonjwa wote,
36and besought him that they might only touch the hem of his garment; and as many as touched were made thoroughly well.
36wakamwomba awaruhusu waguse tu pindo la vazi lake; wote waliomgusa walipona.