1What then [is] the superiority of the Jew? or what the profit of circumcision?
1Basi, Myahudi ana nini zaidi kuliko watu wengine? Au kutahiriwa kuna faida gani?
2Much every way: and first, indeed, that to them were entrusted the oracles of God.
2Naam, iko faida kwa kila upande. Kwanza, Mungu aliwakabidhi Wayahudi ujumbe wake.
3For what? if some have not believed, shall their unbelief make the faith of God of none effect?
3Lakini itakuwaje iwapo baadhi yao hawakuwa waaminifu? Je, jambo hilo litaondoa uaminifu wa Mungu?
4Far be the thought: but let God be true, and every man false; according as it is written, So that thou shouldest be justified in thy words, and shouldest overcome when thou art in judgment.
4Hata kidogo! Mungu hubaki mwaminifu daima, ingawaje kila binadamu ni mwongo. Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Kila usemapo, maneno yako ni ya haki; na katika hukumu, wewe hushinda."
5But if our unrighteousness commend God's righteousness, what shall we say? Is God unrighteous who inflicts wrath? I speak according to man.
5Lakini, ikiwa uovu wetu unathibitisha kwamba Mungu anatenda kwa haki, tutasema nini? Je, tutasema kwamba anakosa haki akituadhibu? (Hapa naongea kibinadamu).
6Far be the thought: since how shall God judge the world?
6Hata kidogo! Ingekuwa hivyo, Mungu angewezaje kuuhukumu ulimwengu?
7For if the truth of God, in my lie, has more abounded to his glory, why yet am *I* also judged as a sinner?
7Labda utasema: "Ikiwa ukosefu wa uaminifu kwa upande wangu unamdhihirisha Mungu kuwa mwaminifu zaidi na hivyo kumpatia utukufu, basi singepaswa kuhukumiwa kuwa mwenye dhambi!"
8and not, according as we are injuriously charged, and according as some affirm that we say, Let us practise evil things, that good ones may come? whose judgment is just.
8Ni sawa na kusema: tufanye maovu ili tupate mema! Ndivyo wengine walivyotukashifu kwa kutushtaki kwamba tumefundisha hivyo. Watahukumiwa wanavyostahili!
9What then? are we better? No, in no wise: for we have before charged both Jews and Greeks with being all under sin:
9Tuseme nini, basi? Je, sisi Wayahudi ni bora zaidi kuliko wengine? Hata kidogo! Kwa maana nimekwisha bainisha hapo mwanzoni kwamba Wayahudi na watu wa mataifa mengine wote wako chini ya utawala wa dhambi.
10according as it is written, There is not a righteous [man], not even one;
10Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Hakuna hata mmoja aliye mwadilifu!
11there is not the [man] that understands, there is not one that seeks after God.
11Hakuna mtu anayeelewa, wala anayemtafuta Mungu.
12All have gone out of the way, they have together become unprofitable; there is not one that practises goodness, there is not so much as one:
12Wote wamepotoka wote wamekosa; hakuna atendaye mema, hakuna hata mmoja.
13their throat is an open sepulchre; with their tongues they have used deceit; asps' poison [is] under their lips:
13Makoo yao ni kama kaburi wazi, ndimi zao zimejaa udanganyifu, midomoni mwao mwatoka maneno yenye sumu kama ya nyoka.
14whose mouth is full of cursing and bitterness;
14Vinywa vyao vimejaa laana chungu.
15swift their feet to shed blood;
15Miguu yao iko mbioni kumwaga damu,
16ruin and misery [are] in their ways,
16popote waendapo husababisha maafa na mateso;
17and way of peace they have not known:
17njia ya amani hawaijui.
18there is no fear of God before their eyes.
18Hawajali kabisa kumcha Mungu."
19Now we know that whatever the things the law says, it speaks to those under the law, that every mouth may be stopped, and all the world be under judgment to God.
19Tunajua kwamba Sheria huwahusu walio chini ya Sheria hiyo, hata hawawezi kuwa na kisingizio chochote, na ulimwengu wote uko chini ya hukumu ya Mungu.
20Wherefore by works of law no flesh shall be justified before him; for by law [is] knowledge of sin.
20Maana hakuna binadamu yeyote anayekubaliwa kuwa mwadilifu mbele yake Mungu kwa kuishika Sheria; kazi ya Sheria ni kumwonyesha tu mtu kwamba ametenda dhambi.
21But now without law righteousness of God is manifested, borne witness to by the law and the prophets;
21Lakini sasa, njia ya Mungu ya kuwakubali watu kuwa waadilifu imekwisha dhihirishwa, tena bila kutegemea Sheria. Sheria na manabii hushuhudia jambo hili.
22righteousness of God by faith of Jesus Christ towards all, and upon all those who believe: for there is no difference;
22Mungu huwakubali watu kuwa waadilifu kwa njia ya imani yao kwa Yesu Kristo; Mungu hufanya hivyo kwa wote wanaoamini; hakuna ubaguzi wowote.
23for all have sinned, and come short of the glory of God;
23Watu wote wametenda dhambi na wametindikiwa utukufu wa Mungu.
24being justified freely by his grace through the redemption which [is] in Christ Jesus;
24Lakini kwa zawadi ya neema ya Mungu, watu wote hukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya Yesu Kristo anayewakomboa.
25whom God has set forth a mercy-seat, through faith in his blood, for [the] shewing forth of his righteousness, in respect of the passing by the sins that had taken place before, through the forbearance of God;
25Mungu alimtoa Yesu kusudi, kwa damu yake, awe njia ya kuwaondolea watu dhambi zao kwa imani yao kwake. Alifanya hivyo ili apate kuonyesha kwamba yeye ni mwadilifu. Hapo zamani Mungu alikuwa mvumilivu bila kuzijali dhambi za watu;
26for [the] shewing forth of his righteousness in the present time, so that he should be just, and justify him that is of [the] faith of Jesus.
26lakini sasa, wakati huu, anazikabili dhambi za watu apate kuonyesha uadilifu wake. Kwa namna hiyo Mungu mwenyewe huonyesha kwamba yeye ni mwadilifu na kwamba humkubali kuwa mwadilifu mtu yeyote anayemwamini Yesu.
27Where then [is] boasting? It has been excluded. By what law? of works? Nay, but by law of faith;
27Basi, tunaweza kujivunia nini? Hakuna! Kwa nini? Je, kwa sababu ya kutimiza Sheria? La! Bali kwa sababu tunaamini.
28for we reckon that a man is justified by faith, without works of law.
28Maana mtu hukubaliwa kuwa mwadilifu kwa imani, wala si kwa kutimiza matakwa ya Sheria.
29Is [God] the God of Jews only? is he not of [the] nations also? Yea, of nations also:
29Au je, Mungu nu Mungu wa Wayahudi tu, ama pia wa watu wa mataifa mengine? Naam, wa mataifa mengine pia.
30since indeed [it is] one God who shall justify [the] circumcision on the principle of faith, and uncircumcision by faith.
30Mungu ni mmoja, naye atawakubali Wayahudi kuwa waadilifu kwa imani yao, na watu wa mataifa mengine pia kwa imani yao.
31Do we then make void law by faith? Far be the thought: [no,] but we establish law.
31Je, tunaitumia imani kuibatilisha Sheria? Hata kidogo; bali tunaipa Sheria thamani yake kamili.