French 1910

Swahili: New Testament

1 Thessalonians

5

1Pour ce qui est des temps et des moments, vous n'avez pas besoin, frères, qu'on vous en écrive.
1Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.
2Car vous savez bien vous-mêmes que le jour du Seigneur viendra comme un voleur dans la nuit.
2Maana ninyi wenyewe mwajua kwamba Siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajavyo usiku.
3Quand les hommes diront: Paix et sûreté! alors une ruine soudaine les surprendra, comme les douleurs de l'enfantement surprennent la femme enceinte, et ils n'échapperont point.
3Watu watakapokuwa wanasema: "Kila kitu ni shwari na salama" ndipo uharibifu utakapowaangukia ghafla! Mambo hayo yatatukia ghafla kama uchungu wa uzazi unavyomjia mama anayejifungua, wala watu hawataweza kuepukana nayo.
4Mais vous, frères, vous n'êtes pas dans les ténèbres, pour que ce jour vous surprenne comme un voleur;
4Lakini ninyi ndugu, hamko gizani, na siku hiyo haipaswi kuwajieni ghafla kama vile mwizi.
5vous êtes tous des enfants de la lumière et des enfants du jour. Nous ne sommes point de la nuit ni des ténèbres.
5Ninyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.
6Ne dormons donc point comme les autres, mais veillons et soyons sobres.
6Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.
7Car ceux qui dorment dorment la nuit, et ceux qui s'enivrent s'enivrent la nuit.
7Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.
8Mais nous qui sommes du jour, soyons sobres, ayant revêtu la cuirasse de la foi et de la charité, et ayant pour casque l'espérance du salut.
8Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.
9Car Dieu ne nous a pas destinés à la colère, mais à l'acquisition du salut par notre Seigneur Jésus-Christ,
9Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
10qui est mort pour nous, afin que, soit que nous veillions, soit que nous dormions, nous vivions ensemble avec lui.
10ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.
11C'est pourquoi exhortez-vous réciproquement, et édifiez-vous les uns les autres, comme en réalité vous le faites.
11Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana ninyi kwa ninyi kama mnavyofanya sasa.
12Nous vous prions, frères, d'avoir de la considération pour ceux qui travaillent parmi vous, qui vous dirigent dans le Seigneur, et qui vous exhortent.
12Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.
13Ayez pour eux beaucoup d'affection, à cause de leur oeuvre. Soyez en paix entre vous.
13Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa sababu ya kazi wanayofanya. Muwe na amani kati yenu.
14Nous vous en prions aussi, frères, avertissez ceux qui vivent dans le désordre, consolez ceux qui sont abattus, supportez les faibles, usez de patience envers tous.
14Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.
15Prenez garde que personne ne rende à autrui le mal pour le mal; mais poursuivez toujours le bien, soit entre vous, soit envers tous.
15Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.
16Soyez toujours joyeux.
16Furahini daima,
17Priez sans cesse.
17salini kila wakati
18Rendez grâces en toutes choses, car c'est à votre égard la volonté de Dieu en Jésus-Christ.
18na muwe na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.
19N'éteignez pas l'Esprit.
19Msimpinge Roho Mtakatifu;
20Ne méprisez pas les prophéties.
20msidharau unabii.
21Mais examinez toutes choses; retenez ce qui est bon;
21Pimeni kila kitu: zingatieni kilicho chema,
22abstenez-vous de toute espèce de mal.
22na epukeni kila aina ya uovu.
23Que le Dieu de paix vous sanctifie lui-même tout entiers, et que tout votre être, l'esprit, l'âme et le corps, soit conservé irrépréhensible, lors de l'avènement de notre Seigneur Jésus-Christ!
23Mungu anayetupatia amani awafanye ninyi watakatifu kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu--roho, mioyo na miili yenu--mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
24Celui qui vous a appelés est fidèle, et c'est lui qui le fera.
24Yeye anayewaita ninyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.
25Frères, priez pour nous.
25Ndugu, tuombeeni na sisi pia.
26Saluez tous les frères par un saint baiser.
26Wasalimuni ndugu wote kwa ishara ya upendo.
27Je vous en conjure par le Seigneur, que cette lettre soit lue à tous les frères.
27Nawahimizeni kwa jina la Bwana muwasomee ndugu zetu wote barua hii.
28Que la grâce de notre Seigneur Jésus-Christ soit avec vous!
28Tunawatakieni neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.