1わたしたちの間に成就された出来事を、最初から親しく見た人々であって、
1Mheshimiwa Theofilo: Watu wengi wamejitahidi kuandika juu ya mambo yale yaliyotendeka kati yetu.
2御言に仕えた人々が伝えたとおり物語に書き連ねようと、多くの人が手を着けましたが、
2Waliandika kama tulivyoelezwa na wale walioyaona kwa macho yao tangu mwanzo, na waliotangaza ujumbe huo.
3テオピロ閣下よ、わたしもすべての事を初めから詳しく調べていますので、ここに、それを順序正しく書きつづって、閣下に献じることにしました。
3Inafaa nami pia, Mheshimiwa, baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote tangu mwanzo, nikuandikie kwa mpango,
4すでにお聞きになっている事が確実であることを、これによって十分に知っていただきたいためであります。
4ili nawe uweze kujionea mwenyewe ukweli wa mambo yale uliyofundishwa.
5ユダヤの王ヘロデの世に、アビヤの組の祭司で名をザカリヤという者がいた。その妻はアロン家の娘のひとりで、名をエリサベツといった。
5Wakati Herode alipokuwa mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani mmoja jina lake Zakaria, wa kikundi cha Abia. Mke wake alikuwa anaitwa Elisabeti, naye alikuwa wa ukoo wa kuhani Aroni.
6ふたりとも神のみまえに正しい人であって、主の戒めと定めとを、みな落度なく行っていた。
6Wote wawili walikuwa wanyofu mbele ya Mungu, wakiishi kwa kufuata amri na maagizo yote ya Bwana bila lawama.
7ところが、エリサベツは不妊の女であったため、彼らには子がなく、そしてふたりともすでに年老いていた。
7Lakini hawakuwa wamejaliwa watoto kwa vile Elisabeti alikuwa tasa, nao wote wawili walikuwa wazee sana.
8さてザカリヤは、その組が当番になり神のみまえに祭司の務をしていたとき、
8Siku moja, ilipokuwa zamu yake ya kutoa huduma ya ukuhani mbele ya Mungu,
9祭司職の慣例に従ってくじを引いたところ、主の聖所にはいって香をたくことになった。
9Zakariya alichaguliwa kwa kura, kama ilivyokuwa desturi, kuingia hekaluni ili afukize ubani.
10香をたいている間、多くの民衆はみな外で祈っていた。
10Watu, umati mkubwa, walikuwa wamekusanyika nje wanasali wakati huo wa kufukiza ubani.
11すると主の御使が現れて、香壇の右に立った。
11Malaika wa Bwana akamtokea humo ndani, akasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia ubani.
12ザカリヤはこれを見て、おじ惑い、恐怖の念に襲われた。
12Zakariya alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.
13そこで御使が彼に言った、「恐れるな、ザカリヤよ、あなたの祈が聞きいれられたのだ。あなたの妻エリサベツは男の子を産むであろう。その子をヨハネと名づけなさい。
13Lakini malaika akamwambia, "Zakariya, usiogope, kwa maana sala yako imesikilizwa, na Elisabeti mkeo atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohane.
14彼はあなたに喜びと楽しみとをもたらし、多くの人々もその誕生を喜ぶであろう。
14Utakuwa na furaha kubwa na watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
15彼は主のみまえに大いなる者となり、ぶどう酒や強い酒をいっさい飲まず、母の胎内にいる時からすでに聖霊に満たされており、
15Atakuwa mkuu mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kileo, atajazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
16そして、イスラエルの多くの子らを、主なる彼らの神に立ち帰らせるであろう。
16Atawaelekeza wengi wa watu wa Israeli kwa Bwana Mungu wao.
17彼はエリヤの霊と力とをもって、みまえに先立って行き、父の心を子に向けさせ、逆らう者に義人の思いを持たせて、整えられた民を主に備えるであろう」。
17Atamtangulia Bwana akiongozwa na nguvu na roho kama Eliya. Atawapatanisha kina baba na watoto wao; atawafanya wasiotii wawe na fikira za uadilifu, na hivyo amtayarishie Bwana watu wake."
18するとザカリヤは御使に言った、「どうしてそんな事が、わたしにわかるでしょうか。わたしは老人ですし、妻も年をとっています」。
18Zakariya akamwambia huyo malaika, "Ni kitu gani kitakachonihakikishia jambo hilo? Mimi ni mzee, hali kadhalika na mke wangu."
19御使が答えて言った、「わたしは神のみまえに立つガブリエルであって、この喜ばしい知らせをあなたに語り伝えるために、つかわされたものである。
19Malaika akamjibu, "Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele ya Mungu, na nimetumwa niseme nawe, nikuletee hii habari njema.
20時が来れば成就するわたしの言葉を信じなかったから、あなたはおしになり、この事の起る日まで、ものが言えなくなる」。
20Sikiliza, utakuwa bubu kwa sababu huyasadiki haya maneno yatakayotimia kwa wakati wake. Hutaweza kusema mpaka hayo niliyokuambia yatakapotimia."
21民衆はザカリヤを待っていたので、彼が聖所内で暇どっているのを不思議に思っていた。
21Wakati huo, wale watu walikuwa wanamngoja Zakariya huku wakishangaa juu ya kukawia kwake Hekaluni.
22ついに彼は出てきたが、物が言えなかったので、人々は彼が聖所内でまぼろしを見たのだと悟った。彼は彼らに合図をするだけで、引きつづき、おしのままでいた。
22Alipotoka nje, hakuweza kusema nao. Ikawa dhahiri kwao kwamba alikuwa ameona maono Hekaluni. Lakini akawa anawapa ishara kwa mikono, akabaki bubu.
23それから務の期日が終ったので、家に帰った。
23Zamu yake ya kuhudumu ilipokwisha, alirudi nyumbani.
24そののち、妻エリサベツはみごもり、五か月のあいだ引きこもっていたが、
24Baadaye Elisabeti mkewe akapata mimba. Akajificha nyumbani kwa muda wa miezi mitano, akisema:
25「主は、今わたしを心にかけてくださって、人々の間からわたしの恥を取り除くために、こうしてくださいました」と言った。
25"Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana; ameniangalia na kuniondolea aibu niliyokuwa nayo mbele ya watu."
26六か月目に、御使ガブリエルが、神からつかわされて、ナザレというガリラヤの町の一処女のもとにきた。
26Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya,
27この処女はダビデ家の出であるヨセフという人のいいなづけになっていて、名をマリヤといった。
27kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi.
28御使がマリヤのところにきて言った、「恵まれた女よ、おめでとう、主があなたと共におられます」。
28Malaika akamwendea, akamwambia, "Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe."
29この言葉にマリヤはひどく胸騒ぎがして、このあいさつはなんの事であろうかと、思いめぐらしていた。
29Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini?
30すると御使が言った、「恐れるな、マリヤよ、あなたは神から恵みをいただいているのです。
30Malaika akamwambia, "Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.
31見よ、あなたはみごもって男の子を産むでしょう。その子をイエスと名づけなさい。
31Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu.
32彼は大いなる者となり、いと高き者の子と、となえられるでしょう。そして、主なる神は彼に父ダビデの王座をお与えになり、
32Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake.
33彼はとこしえにヤコブの家を支配し、その支配は限りなく続くでしょう」。
33Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho."
34そこでマリヤは御使に言った、「どうして、そんな事があり得ましょうか。わたしにはまだ夫がありませんのに」。
34Maria akamjibu, "Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?"
35御使が答えて言った、「聖霊があなたに臨み、いと高き者の力があなたをおおうでしょう。それゆえに、生れ出る子は聖なるものであり、神の子と、となえられるでしょう。
35Malaika akamjibu, "Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu.
36あなたの親族エリサベツも老年ながら子を宿しています。不妊の女といわれていたのに、はや六か月になっています。
36Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa.
37神には、なんでもできないことはありません」。
37Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu."
38そこでマリヤが言った、「わたしは主のはしためです。お言葉どおりこの身に成りますように」。そして御使は彼女から離れて行った。
38Maria akasema, "Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema." Kisha yule malaika akaenda zake.
39そのころ、マリヤは立って、大急ぎで山里へむかいユダの町に行き、
39Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yuda.
40ザカリヤの家にはいってエリサベツにあいさつした。
40Huko, aliingia katika nyumba ya Zakariya, akamsalimu Elisabeti.
41エリサベツがマリヤのあいさつを聞いたとき、その子が胎内でおどった。エリサベツは聖霊に満たされ、
41Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifiu,
42声高く叫んで言った、「あなたは女の中で祝福されたかた、あなたの胎の実も祝福されています。
42akasema kwa sauti kubwa, "Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa.
43主の母上がわたしのところにきてくださるとは、なんという光栄でしょう。
43Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
44ごらんなさい。あなたのあいさつの声がわたしの耳にはいったとき、子供が胎内で喜びおどりました。
44Nakwambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
45主のお語りになったことが必ず成就すると信じた女は、なんとさいわいなことでしょう」。
45Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokwambia."
46するとマリヤは言った、「わたしの魂は主をあがめ、
46Naye Maria akasema,
47わたしの霊は救主なる神をたたえます。
47"Moyo wangu wamtukuza Bwana, roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.
48この卑しい女をさえ、心にかけてくださいました。今からのち代々の人々は、わたしをさいわいな女と言うでしょう、
48Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu. Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.
49力あるかたが、わたしに大きな事をしてくださったからです。そのみ名はきよく、
49Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu, jina lake ni takatifu.
50そのあわれみは、代々限りなく主をかしこみ恐れる者に及びます。
50Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi.
51主はみ腕をもって力をふるい、心の思いのおごり高ぶる者を追い散らし、
51Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
52権力ある者を王座から引きおろし、卑しい者を引き上げ、
52amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.
53飢えている者を良いもので飽かせ、富んでいる者を空腹のまま帰らせなさいます。
53Wenye njaa amewashibisha mema, matajiri amewaacha waende mikono mitupu.
54主は、あわれみをお忘れにならず、その僕イスラエルを助けてくださいました、
54Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.
55わたしたちの父祖アブラハムとその子孫とをとこしえにあわれむと約束なさったとおりに」。
55Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele."
56マリヤは、エリサベツのところに三か月ほど滞在してから、家に帰った。
56Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.
57さてエリサベツは月が満ちて、男の子を産んだ。
57Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.
58近所の人々や親族は、主が大きなあわれみを彼女におかけになったことを聞いて、共どもに喜んだ。
58Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.
59八日目になったので、幼な子に割礼をするために人々がきて、父の名にちなんでザカリヤという名にしようとした。
59Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakariya.
60ところが、母親は、「いいえ、ヨハネという名にしなくてはいけません」と言った。
60Lakini mama yake akasema, "La, sivyo, bali ataitwa Yohane."
61人々は、「あなたの親族の中には、そういう名のついた者は、ひとりもいません」と彼女に言った。
61Wakamwambia, "Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?"
62そして父親に、どんな名にしたいのですかと、合図で尋ねた。
62Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.
63ザカリヤは書板を持ってこさせて、それに「その名はヨハネ」と書いたので、みんなの者は不思議に思った。
63Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: "Yohane ndilo jina lake." Wote wakastaajabu.
64すると、立ちどころにザカリヤの口が開けて舌がゆるみ、語り出して神をほめたたえた。
64Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
65近所の人々はみな恐れをいだき、またユダヤの山里の至るところに、これらの事がことごとく語り伝えられたので、
65Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.
66聞く者たちは皆それを心に留めて、「この子は、いったい、どんな者になるだろう」と語り合った。主のみ手が彼と共にあった。
66Wote waliosikia mambo hayo waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: "Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?" Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.
67父ザカリヤは聖霊に満たされ、預言して言った、
67Zakariya, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka ujumbe wa Mungu:
68「主なるイスラエルの神は、ほむべきかな。神はその民を顧みてこれをあがない、
68"Asifiwe Bwana Mungu wa Israeli, kwani amekuja kuwasaidia na kuwakomboa watu wake.
69わたしたちのために救の角を僕ダビデの家にお立てになった。
69Ametupatia Mwokozi shujaa, mzawa wa Daudi mtumishi wake.
70古くから、聖なる預言者たちの口によってお語りになったように、
70Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu,
71わたしたちを敵から、またすべてわたしたちを憎む者の手から、救い出すためである。
71kwamba atatuokoa mikononi mwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72こうして、神はわたしたちの父祖たちにあわれみをかけ、その聖なる契約、
72Alisema atawahurumia wazee wetu, na kukumbuka agano lake takatifu.
73すなわち、父祖アブラハムにお立てになった誓いをおぼえて、
73Kiapo alichomwapia Abrahamu baba yetu, ni kwamba atatujalia sisi
74わたしたちを敵の手から救い出し、
74tukombolewe kutoka adui zetu, tupate kumtumikia bila hofu,
75生きている限り、きよく正しく、みまえに恐れなく仕えさせてくださるのである。
75kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu.
76幼な子よ、あなたは、いと高き者の預言者と呼ばれるであろう。主のみまえに先立って行き、その道を備え、
76Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu, utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;
77罪のゆるしによる救をその民に知らせるのであるから。
77kuwatangazia watu kwamba wataokolewa kwa kuondolewa dhambi zao.
78これはわたしたちの神のあわれみ深いみこころによる。また、そのあわれみによって、日の光が上からわたしたちに臨み、
78Mungu wetu ni mpole na mwenye huruma. Atasababisha pambazuko angavu la ukombozi litujie kutoka juu,
79暗黒と死の陰とに住む者を照し、わたしたちの足を平和の道へ導くであろう」。幼な子は成長し、その霊も強くなり、そしてイスラエルに現れる日まで、荒野にいた。
79na kuwaangazia wote wanaokaa katika giza kuu la kifo, aongoze hatua zetu katika njia ya amani."
80幼な子は成長し、その霊も強くなり、そしてイスラエルに現れる日まで、荒野にいた。
80Mtoto akakua, akapata nguvu rohoni. Alikaa jangwani mpaka alipojionyesha rasmi kwa watu wa Israeli.