1イエスが宮から出て行こうとしておられると、弟子たちは近寄ってきて、宮の建物にイエスの注意を促した。
1Yesu alitoka Hekaluni, na alipokuwa akienda zake, wanafunzi wake walimwendea, wakamwonyesha majengo ya Hekalu.
2そこでイエスは彼らにむかって言われた、「あなたがたは、これらすべてのものを見ないか。よく言っておく。その石一つでもくずされずに、そこに他の石の上に残ることもなくなるであろう」。
2Yesu akawaambia, "Sawa, mnaweza kuyatazama haya yote! Kweli nawaambieni, hakuna hata jiwe moja litakalosalia hapa juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa."
3またオリブ山ですわっておられると、弟子たちが、ひそかにみもとにきて言った、「どうぞお話しください。いつ、そんなことが起るのでしょうか。あなたがまたおいでになる時や、世の終りには、どんな前兆がありますか」。
3Yesu alipokuwa ameketi juu ya mlima wa Mizeituni, wanafunzi walimwendea faraghani, wakamwuliza, "Twambie mambo haya yatatukia lini? Ni ishara gani itakayoonyesha kuja kwako na mwisho wa nyakati?"
4そこでイエスは答えて言われた、「人に惑わされないように気をつけなさい。
4Yesu akawajibu, "Jihadharini msije mkadanganywa na mtu.
5多くの者がわたしの名を名のって現れ、自分がキリストだと言って、多くの人を惑わすであろう。
5Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: Mimi ndiye Kristo, nao watawapotosha watu wengi.
6また、戦争と戦争のうわさとを聞くであろう。注意していなさい、あわててはいけない。それは起らねばならないが、まだ終りではない。
6Mtasikia juu ya vita na fununu za vita; lakini msifadhaike, maana hayo hayana budi kutokea, lakini mwisho wenyewe ungali bado.
7民は民に、国は国に敵対して立ち上がるであろう。またあちこちに、ききんが起り、また地震があるであろう。
7Taifa moja litapigana na taifa lingine; ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine. Hapa na pale patakuwa na njaa na mitetemeko ya ardhi.
8しかし、すべてこれらは産みの苦しみの初めである。
8Yote hayo ni kama mwanzo wa maumivu ya kujifungua mtoto.
9そのとき人々は、あなたがたを苦しみにあわせ、また殺すであろう。またあなたがたは、わたしの名のゆえにすべての民に憎まれるであろう。
9"Kisha watawatoeni ili mteswe na kuuawa. Mataifa yote yatawachukieni kwa ajili ya jina langu.
10そのとき、多くの人がつまずき、また互に裏切り、憎み合うであろう。
10Tena, wengi wataiacha imani yao, watasalitiana na kuchukiana.
11また多くのにせ預言者が起って、多くの人を惑わすであろう。
11Watatokea manabii wengi wa uongo watakaowapotosha watu wengi.
12また不法がはびこるので、多くの人の愛が冷えるであろう。
12Kwa sababu ya ongezeko la uhalifu, upendo wa watu wengi utafifia.
13しかし、最後まで耐え忍ぶ者は救われる。
13Lakini atakayevumilia mpaka mwisho, ataokoka.
14そしてこの御国の福音は、すべての民に対してあかしをするために、全世界に宣べ伝えられるであろう。そしてそれから最後が来るのである。
14Ila, kabla ya mwisho kufika, hii Habari Njema ya Ufalme wa Mungu itahubiriwa ulimwenguni kote kama ushuhuda kwa mataifa yote.
15預言者ダニエルによって言われた荒らす憎むべき者が、聖なる場所に立つのを見たならば(読者よ、悟れ)、
15"Basi, mtakapoona Chukizo Haribifu lililonenwa na nabii Danieli limesimama mahali patakatifu, (msomaji na atambue maana yake),
16そのとき、ユダヤにいる人々は山へ逃げよ。
16hapo, walioko Yudea na wakimbilie milimani.
17屋上にいる者は、家からものを取り出そうとして下におりるな。
17Aliye juu ya paa la nyumba yake asishuke kuchukua kitu nyumbani mwake.
18畑にいる者は、上着を取りにあとへもどるな。
18Aliye shambani asirudi nyuma kuchukua vazi lake.
19その日には、身重の女と乳飲み子をもつ女とは、不幸である。
19Ole wao kina mama waja wazito na wanaonyonyesha siku hizo!
20あなたがたの逃げるのが、冬または安息日にならないように祈れ。
20Ombeni ili kukimbia kwenu kusiwe siku za baridi au siku ya Sabato!
21その時には、世の初めから現在に至るまで、かつてなく今後もないような大きな患難が起るからである。
21Maana wakati huo kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka leo, wala haitapata kutokea tena.
22もしその期間が縮められないなら、救われる者はひとりもないであろう。しかし、選民のためには、その期間が縮められるであろう。
22Kama siku hizo hazingalipunguzwa, hakuna binadamu yeyote ambaye angeokoka; lakini siku hizo zitapunguzwa kwa ajili ya wale walioteuliwa.
23そのとき、だれかがあなたがたに『見よ、ここにキリストがいる』、また、『あそこにいる』と言っても、それを信じるな。
23"Basi, mtu akiwaambieni siku hizo: Kristo yuko hapa au Yuko pale, msimsadiki.
24にせキリストたちや、にせ預言者たちが起って、大いなるしるしと奇跡とを行い、できれば、選民をも惑わそうとするであろう。
24Maana watatokea kina Kristo wa uongo na manabii wa uongo. Watafanya ishara kubwa na maajabu ya kuweza kuwapotosha ikiwezekana hata wateule wa Mungu.
25見よ、あなたがたに前もって言っておく。
25Sikilizeni, nimekwisha kuwaonya kabla ya wakati.
26だから、人々が『見よ、彼は荒野にいる』と言っても、出て行くな。また『見よ、へやの中にいる』と言っても、信じるな。
26Basi, wakiwaambieni, Tazameni, yuko jangwani, msiende huko; au, Tazameni, amejificha ndani, msisadiki;
27ちょうど、いなずまが東から西にひらめき渡るように、人の子も現れるであろう。
27maana, kama vile umeme uangazavyo toka mashariki hadi magharibi, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Mtu.
28死体のあるところには、はげたかが集まるものである。
28Pale ulipo mzoga, ndipo watakapokusanyika tai.
29しかし、その時に起る患難の後、たちまち日は暗くなり、月はその光を放つことをやめ、星は空から落ち、天体は揺り動かされるであろう。
29"Mara baada ya dhiki ya siku hizo, jua litatiwa giza, mwezi hautaangaza, nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za mbingu zitatikiswa.
30そのとき、人の子のしるしが天に現れるであろう。またそのとき、地のすべての民族は嘆き、そして力と大いなる栄光とをもって、人の子が天の雲に乗って来るのを、人々は見るであろう。
30Kisha, ishara ya Mwana wa Mtu itaonekana angani, na hapo makabila yote duniani yatalalamika; watamwona Mwana wa Mtu akija juu ya mawingu ya angani mwenye nguvu na utukufu mwingi.
31また、彼は大いなるラッパの音と共に御使たちをつかわして、天のはてからはてに至るまで、四方からその選民を呼び集めるであろう。
31Naye atawatuma malaika wake wenye tarumbeta la kuvuma sana, nao watawakusanya wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, toka mwisho huu wa mbingu hadi mwisho huu.
32いちじくの木からこの譬を学びなさい。その枝が柔らかになり、葉が出るようになると、夏の近いことがわかる。
32"Kwa mtini jifunzeni mfano huu: Mara tu matawi yake yanapoanza kuwa laini na kuchanua majani, mnajua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
33そのように、すべてこれらのことを見たならば、人の子が戸口まで近づいていると知りなさい。
33Hali kadhalika nanyi mtakapoona mambo haya yote yakitendeka, jueni kwamba yuko karibu sana.
34よく聞いておきなさい。これらの事が、ことごとく起るまでは、この時代は滅びることがない。
34Nawaambieni kweli, kizazi hiki hakitapita kabla ya mambo hayo yote kutukia.
35天地は滅びるであろう。しかしわたしの言葉は滅びることがない。
35Naam, mbingu na dunia zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
36その日、その時は、だれも知らない。天の御使たちも、また子も知らない、ただ父だけが知っておられる。
36"Lakini, juu ya siku au saa hiyo, hakuna mtu ajuaye itakuja lini; wala malaika wa mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake ndiye ajuaye.
37人の子の現れるのも、ちょうどノアの時のようであろう。
37Kwa maana kama ilivyokuwa nyakati za Noa, ndivyo itakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Mtu.
38すなわち、洪水の出る前、ノアが箱舟にはいる日まで、人々は食い、飲み、めとり、とつぎなどしていた。
38Maana nyakati hizo, kabla ya gharika kuu, watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka Noa alipoingia ndani ya ile safina.
39そして洪水が襲ってきて、いっさいのものをさらって行くまで、彼らは気がつかなかった。人の子の現れるのも、そのようであろう。
39Hawakujua kuna nini mpaka ile gharika ilipotokea, ikawakumba wote. Ndivyo itakavyokuwa wakati Mwana wa Mtu atakapokuja.
40そのとき、ふたりの者が畑にいると、ひとりは取り去られ、ひとりは取り残されるであろう。
40Wakati huo watu wawili watakuwa shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.
41ふたりの女がうすをひいていると、ひとりは取り去られ、ひとりは残されるであろう。
41Kina mama wawili watakuwa wanasaga nafaka, mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.
42だから、目をさましていなさい。いつの日にあなたがたの主がこられるのか、あなたがたには、わからないからである。
42Basi, kesheni, kwa maana hamjui siku atakayokuja Bwana wenu.
43このことをわきまえているがよい。家の主人は、盗賊がいつごろ来るかわかっているなら、目をさましていて、自分の家に押し入ることを許さないであろう。
43Lakini kumbukeni jambo hili: kama mwenye nyumba angejua siku mwizi atakapofika, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
44だから、あなたがたも用意をしていなさい。思いがけない時に人の子が来るからである。
44Kwa hiyo, nanyi pia muwe tayari, kwa maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia."
45主人がその家の僕たちの上に立てて、時に応じて食物をそなえさせる忠実な思慮深い僕は、いったい、だれであろう。
45Yesu akaendelea kusema, "Ni nani basi mtumishi mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watu wake, awape chakula kwa wakati wake?
46主人が帰ってきたとき、そのようにつとめているのを見られる僕は、さいわいである。
46Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakapokuja atamkuta akifanya hivyo.
47よく言っておくが、主人は彼を立てて自分の全財産を管理させるであろう。
47Kweli nawaambieni, atamweka mtumishi huyo aisimamie mali yake yote.
48もしそれが悪い僕であって、自分の主人は帰りがおそいと心の中で思い、
48Lakini kama mtumishi mbaya akijisemea moyoni: Bwana wangu anakawia kurudi,
49その僕仲間をたたきはじめ、また酒飲み仲間と一緒に食べたり飲んだりしているなら、
49kisha akaanza kuwapiga watumishi wenzake, akaanza kula na kunywa pamoja na walevi,
50その僕の主人は思いがけない日、気がつかない時に帰ってきて、彼を厳罰に処し、偽善者たちと同じ目にあわせるであろう。彼はそこで泣き叫んだり、歯がみをしたりするであろう。
50bwana wake atakuja siku asiyoitazamia na saa asiyoijua.
51彼を厳罰に処し、偽善者たちと同じ目にあわせるであろう。彼はそこで泣き叫んだり、歯がみをしたりするであろう。
51Atamkatilia mbali na kumweka kundi moja na wanafiki. Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.