Kabyle: New Testament

Swahili: New Testament

Colossians

1

1Nekk Bulus, amceggeɛ n Ɛisa Lmasiḥ s lebɣi n Sidi Ṛebbi akk-d gma-tneɣ Timuti,
1Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Timotheo,
2i watmaten yellan di temdint n Kulus, wid iteddun s ṣṣfa deg webrid n Lmasiḥ. Ṛṛeḥma ț-țalwit a wen-d-țțunefkent s ɣuṛ Ṛebbi Baba-tneɣ !
2tunawaandikia ninyi watu wa Mungu huko Kolosai, ndugu zetu waaminifu katika kuungana na Kristo. Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu.
3Nețḥemmid Sidi Ṛebbi Baba-s n Ssid-nneɣ Ɛisa Lmasiḥ yerna ndeɛɛu fell-awen ;
3Daima tunamshukuru Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, wakati tunapowaombea.
4axaṭer nesla s liman i tesɛam di Ɛisa Lmasiḥ d wamek i tḥemmlem agdud n Sidi Ṛebbi,
4Maana tumesikia juu ya imani yenu katika Kristo Yesu na juu ya upendo wenu kwa watu wote wa Mungu.
5ɣef ddemma n usirem i wen-ițțuheggan deg igenwan, asirem nni i wen-d-ițțuxebbṛen s wawal n tideț n lexbaṛ n lxiṛ.
5Wakati ujumbe ule wa kweli, yaani Habari Njema, ilipowafikieni kwa mara ya kwanza, mlipata kusikia juu ya lile tumaini linalopatikana kwake. Kwa sababu hiyo imani na upendo wenu vinategemea jambo lile mnalotumainia ambalo mmewekewa salama mbinguni.
6Lexbeṛ-agi n lxiṛ yewḍen armi d ɣuṛ-wen, yețnerni di ddunit meṛṛa ; akken daɣen i gețnerni deg-wen ula d kunwi seg wasmi i teslam yerna tessnem tideț ɣef ṛṛeḥma n Sidi Ṛebbi,
6Habari Njema inazidi kuzaa matunda na kuenea ulimwenguni kote kama vile ilivyofanya kwenu ninyi tangu siku ile mliposikia juu ya neema ya Mungu na kuitambua ilivyo kweli.
7akken i wen-ț-isselmed Ibafras, aṛfiq-nneɣ eɛzizen di leqdic ; nețța iqeddcen ɣef Lmasiḥ s wul yeṣfan,
7Mlijifunza juu ya neema ya Mungu kutoka kwa Epafra, mtumishi mwenzetu, ambaye ni mfanyakazi mwaminifu wa Kristo kwa niaba yetu.
8ixebbeṛ-aɣ-ed ɣef leḥmala s wayes i kkun-yeččuṛ Ṛṛuḥ iqedsen.
8Yeye alitupa habari za upendo wenu mliojaliwa na Roho.
9Daymi nezga ndeɛɛu fell-awen ɣer Sidi Ṛebbi seg wasmi nesla yis-wen, nessutur-as a wen-d-yefk amek ara tissinem akken ilaq lebɣi ines, s lɛeqliya d lefhama i d-ițțak Ṛṛuḥ iqedsen.
9Kwa sababu hiyo tumekuwa tukiwaombeeni daima tangu tulipopata habari zenu. Tunamwomba Mungu awajazeni ujuzi kamili wa mapenzi yake, awajazeni hekima yote na elimu iletwayo na Roho wake.
10S wakka, aț-țleḥḥum s tikli yebɣa Sidi Ṛebbi iwakken a s tɛeǧbem di kullec, a d-tefkem lfakya yelhan, yerna aț-țnernim di tmusni n Sidi Ṛebbi,
10Hapo mtaweza kuishi kama anavyotaka Bwana na kutenda daima yanayompendeza. Maisha yenu yatakuwa yenye matunda ya kila namna ya matendo mema na mtazidi kukua katika kumjua Mungu.
11Ndeɛɛu ɣer Ṛebbi akken a kkun-isseǧhed s tezmert-is tameqqrant iwakken aț-tṣebṛem i kullec alamma ț-țaggara.
11Mungu awajalieni nguvu kwa uwezo wake mtukufu ili mweze kustahimili kila kitu kwa uvumilivu.
12Ḥemmdet, cekkṛet s lfeṛḥ Sidi Ṛebbi Baba-tneɣ i wen-d-yefkan amur di lweṛt i d-ihegga i warraw n tafat.
12Na kwa furaha, mshukuruni Baba aliyewawezesha ninyi kuwa na sehemu yenu katika mambo yale Mungu aliyowawekea watu wake katika utawala wa mwanga.
13Ikkes-aɣ-d si tezmert n ṭṭlam, iwakken a ɣ-yessiweḍ ɣer tgelda n Mmi-s eɛzizen,
13Yeye alituokoa katika nguvu ya giza, akatuleta salama katika ufalme wa Mwanae mpenzi,
14s wayes nețwasellek yerna nesɛa leɛfu n ddnubat-nneɣ.
14ambaye kwa njia yake tunakombolewa, yaani dhambi zetu zinaondolewa.
15Lmasiḥ, d ṣṣifa n Sidi Ṛebbi ur nezmir a nwali, d nețța i d amezwaru n txelqit meṛṛa.
15Kristo ni mfano wa Mungu asiyeonekana; ni mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
16Yis i gețwaxleq wayen nețwali d wayen ur nețwali ara ama deg igenwan ama di lqaɛa, tigeldiwin d igelliden, lḥekmat akk-d tezmar yellan deg igenwan ; kullec yețwaxleq yis, kullec yețwaxleq i nețța.
16Maana kwa njia yake vitu vyote viliumbwa duniani na mbinguni, vitu vinavyoonekana na visivyoonekana: wenye enzi, watawala, wakuu na wenye mamlaka. Vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake.
17Yella-d uqbel a d-yețwaxleq kra yellan, d nețța i d lsas n txelqit,
17Kristo alikuwako kabla ya vitu vyote; kwa kuungana naye, vyote vyadumu mahali pake.
18d aqeṛṛuy n tejmaɛt n imasiḥiyen yellan d lǧețța-s. Yella si tazwara, d nețța i d amenzu i d-iḥyan si ger lmegtin iwakken ad yili d amezwaru di kullec.
18Yeye ni kichwa cha mwili wake, yaani kanisa; yeye ni chanzo cha uhai wa huo mwili. Yeye ndiye mwanzo, mzaliwa wa kwanza aliyefufuliwa kutoka wafu, ili awe na nafasi ya kwanza katika vitu vyote.
19Axaṭer Sidi Ṛebbi yufa lfeṛḥ-is s lekmal di Mmi-s,
19Maana Mungu alipenda utimilifu wote uwe ndani yake.
20s Lmasiḥ i gemṣalaḥ akk-d txelqit, yessers-ed lehna ama di lqaɛa ama deg igenwan s idammen n Mmi-s yuzzlen ɣef wumidag.
20Kwa njia yake Mungu alivipatanisha naye vitu vyote naam, viumbe vyote mbinguni na duniania; alileta amani kwa damu ya Kristo msalabani.
21Kunwi yellan zik-nni d ibeṛṛaniyen, d iɛdawen n Sidi Ṛebbi s ixemmimen-nwen d yir lecɣal nwen
21Hapo kwanza ninyi pia mlikuwa mbali na Mungu na mlikuwa adui zake kwa sababu ya fikira zenu na matendo yenu maovu.
22Tura issemṣaleḥ-ikkun yid-es s lmut n Mmi-s iwakken a d-tbanem zdat-es teṣfam, mbla lɛib.
22Lakini sasa, kwa kifo cha Mwanae aliyeishi hapa duniani, Mungu amewapatanisha naye, kusudi awalete mbele yake mkiwa watakatifu, safi na bila lawama.
23Ma yella teṭṭfem di liman-nwen s tideț, ma yella tbeddem, tṛeṣṣam. Ɣuṛ-wat aț-țțwexxṛem ɣef wusirem i wen-d-yewwi lexbaṛ n lxiṛ iwumi teslam, lexbaṛ-agi n lxiṛ i gețțubeccṛen i yemdanen n ddunit meṛṛa, i ɣef uɣaleɣ nekk d aqeddac.
23Mnapaswa, lakini kuendelea kuwa imara na thabiti katika imani hiyo, na msikubali kusukumwa mbali na tumaini lile mlilopata wakati mlipoisikia Habari Njema. Mimi Paulo nimekuwa mtumishi wa hiyo Habari Njema ambayo imekwisha hubiriwa kila kiumbe duniani.
24Tura feṛḥeɣ aṭas imi nɛețțabeɣ fell-awen, axaṭer țkemmileɣ ayen ixuṣṣen i leɛtab n Lmasiḥ ɣef ddemma n imasiḥiyen meṛṛa, yellan d lǧețța-s, i ɣef uɣaleɣ d aqeddac.
24Na sasa nafurahi kuteseka kwa ajili yenu, maana kwa mateso yangu hapa duniani, nasaidia kukamilisha kile kilichopungua bado katika mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, yaani kanisa.
25Iceggeɛ-iyi-d Sidi Ṛebbi iwakken a wen-d-beccṛeɣ awal-is s lekmal.
25Nami nimefanywa kuwa mtumishi wa kanisa kufuatana na mpango wake Mungu ambao alinikabidhi kwa faida yenu. Mpango wenyewe ni kuutangaza kwa ukamilifu ujumbe wake,
26Lbaḍna yeffren si zik, si lǧil ɣer lǧil, ibeggen-iț-id tura i wid yellan d ayla-s.
26ambao ni siri aliyowaficha binadamu wote tangu milele, lakini sasa amewajulisha watu wake.
27Yebɣa a d-yesken ccan n lbaḍna agi ifazen i leǧnas nniḍen ur nelli ara n wat Isṛail, iwakken ad walin Lmasiḥ deg-wen, nețța yellan d lsas n lɛaḍima i ɣer nessaram.
27Mpango wa Mungu ni kuwajulisha watu wake siri hii kuu na tukufu ambayo ni kwa ajili ya watu wote. Na, siri yenyewe ndiyo hii: Kristo yuko ndani yenu, na jambo hilo lamaanisha kwamba ninyi mtaushiriki utukufu wa Mungu.
28D Lmasiḥ agi i nețbecciṛ i yemdanen, nețweṣṣi-ten, nesselmad iten s tmusni d leɛqel, iwakken yal amdan ad innekmal di Lmasiḥ zdat Sidi Ṛebbi.
28Kwa sababu hiyo tunamhubiri Kristo kwa watu wote; tunawaonya na kuwafundisha wote kwa hekima yote, ili tuweze kumleta kila mmoja mbele ya Mungu akiwa amekomaa katika kuungana na Kristo.
29Ɣef wayagi i qeddceɣ s tezmert n Lmasiḥ yellan deg-i.
29Kwa madhumuni hayo mimi nafanya kazi na kujitahidi nikiitumia nguvu kuu ya Kristo ifanyayo kazi ndani yangu.