1Malxisadeq-agi yella d agellid n Salem, d lmuqeddem n Sidi Ṛebbi ɛlayen. D nețța i gemmugren Sidna Ibṛahim mi d-yuɣal seg umenɣi i deg yeɣleb igelliden nniḍen, iwakken a t-ibarek.
1Melkisedeki alikuwa mfalme wa Salemu, na kuhani wa Mungu Mkuu. Abrahamu alipokuwa anarudi kutoka vitani ambako aliwaua wafalme, Melkisedeki alikutana naye akambariki,
2I nețța i gefka Sidna Ibṛahim amur wis ɛecṛa n wayen akk i d-yerbeḥ seg umenɣi. Malxisadeq lmeɛna n yisem-is « agellid n lḥeqq », yețțusemma daɣen agellid n Salem yeɛni « agellid n lehna ».
2naye Abrahamu akampa sehemu ya kumi ya vitu vyote alivyokuwa navyo. (Maana ya kwanza ya jina hili Melkisedeki ni "Mfalme wa Uadilifu"; na, kwa vile yeye alikuwa mfalme wa Salemu, jina lake pia lina maana ya "Mfalme wa Amani.")
3Ur neẓri ara anwa i d baba-s neɣ anta i d yemma-s, ur nessin tajaddit-is, ur neẓri melmi i glul neɣ melmi i gemmut. Yella d lemtel n Mmi-s n Ṛebbi, yeqqim d lmuqeddem i dayem.
3Baba yake na mama yake hawatajwi, wala ukoo wake hautajwi; haisemwi alizaliwa lini au alikufa lini. Anafanana na Mwana wa Mungu, na anaendelea kuwa kuhani daima.
4Walit acḥal meqqeṛ ccan n win iwumi yefka Sidna Ibṛahim leɛcuṛ seg wayen i d-yerbeḥ deg umenɣi.
4Basi, mwaona jinsi mtu huyu alivyokuwa maarufu. Baba Abrahamu alimpa sehemu moja ya kumi ya vitu vyote alivyoteka vitani.
5At Lewwi yellan d lmuqedmin, țțawin leɛcuṛ ɣef wat Isṛail yellan d atmaten-nsen akken i d-tenna ccariɛa, ɣas akken ula d nutni ț-țarwa n Sidna Ibṛahim.
5Tunajua vilevile kwamba kufuatana na Sheria, wana wa Lawi ambao ni makuhani, wanayo haki ya kuchukua sehemu ya kumi kutoka kwa watu, yaani ndugu zao, ingawaje nao ni watoto wa Abrahamu.
6Ma d Malxisadeq ur nelli ara n at Lewwi, yewwi leɛcuṛ s ɣuṛ Sidna Ibṛahim yerna iburek-it.
6Lakini huyo Melkisedeki hakuwa wa ukoo wa Lawi, hata hivyo alipokea sehemu ya kumi kutoka kwa Abrahamu; tena akambariki yeye ambaye alikuwa amepewa ahadi ya Mungu.
7Mbla ccekk win yețbaraken yugar win yețțubarken.
7Hakuna mashaka hata kidogo kwamba anayebariki ni mkuu zaidi kuliko yule anayebarikiwa.
8At Lewwi-agi yețțawin leɛcuṛ, d imdanen yețmețțaten, ma d Malxisadeq d win i ɣef d-nnant tira iqedsen : Mazal idder.
8Tena, hao makuhani wanaopokea sehemu ya kumi, ni watu ambao hufa; lakini hapa anayepokea sehemu ya kumi, yaani Melkisedeki, anasemekana kwamba hafi.
9Nezmer ihi a d-nini belli Lewwi yețțawin leɛcuṛ ɣef wat Isṛail, yefka leɛcuṛ i Malxisadeq uqbel a d-ilal s ufus n Sidna Ibṛahim yellan si lejdud-is ;
9Twaweza, basi, kusema kwamba Abrahamu alipotoa sehemu moja ya kumi, Lawi (ambaye watoto wake hupokea sehemu moja ya kumi) alitoa sehemu moja ya kumi pia.
10axaṭer asmi yemmuger Malxisadeq Sidna Ibṛahim, Lewwi urɛad d-ilul.
10Maana Lawi hakuwa amezaliwa bado, bali ni kama alikuwa katika mwili wa baba yake, Abrahamu, wakati Melkisedeki alipokutana naye.
11Ccɣel i xeddmen lmuqedmin n at Lewwi, d lsas n ccariɛa yețțunefken i wegdud n wat Isṛail ; meɛna lemmer yennekmal ccɣel-agi, acuɣeṛ ihi ara d-yili lmuqeddem nniḍen am Malxisadeq mačči am Haṛun n at Lewwi ?
11Kutokana na ukuhani wa Walawi, watu wa Israeli walipewa Sheria. Sasa, kama huduma ya Walawi ingalikuwa kamilifu hapangekuwa tena na haja ya kutokea ukuhani mwingine tofauti, ukuhani ambao umefuata utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki, na si ule wa Aroni.
12Ma yella ccɣel i xeddmen lmuqeddmin n at Lewwi yuɣal di rrif, ihi ula d ccariɛa aț-țuɣal di rrif.
12Maana ukuhani ukibadilika ni lazima Sheria nayo ibadilike.
13Axaṭer Ssid-nneɣ, ur d-yekki ara seg wedrum n at Lewwi, meɛna yekka-d seg wedrum nniḍen. Adrum-nni ulac deg-s ula d yiwen n lmuqeddem i gqedcen deg wudekkan n iseflawen.
13Naye Bwana wetu ambaye mambo hayo yote yanasemwa juu yake, alikuwa wa kabila lingine, na wala hakuna hata mmoja wa kabila lake aliyepata kutumikia madhabahuni akiwa kuhani.
14Ihi neẓra belli Ssid-nneɣ yeffeɣ ed seg wedrum n Yahuda, yerna Sidna Musa ur d-yenni ara a d-yeffeɣ lmuqeddem seg wedrum agi.
14Inafahamika wazi kwamba yeye alizaliwa katika kabila la Yuda ambalo Mose hakulitaja alipokuwa anasema juu ya makuhani.
15Yella wayen i d-ibeggnen annect agi, axaṭer yeffeɣ-ed lmuqeddem nniḍen yecban Malxisadeq.
15Tena jambo hili ni dhahiri zaidi: kuhani mwingine anayefanana na Melkisedeki amekwisha tokea.
16Mačči d ccariɛa i t-yerran d lmuqeddem meɛna yuɣal d lmuqeddem s tezmert n tudert ur nețfaka ;
16Yeye hakufanywa kuwa kuhani kwa sheria na maagizo ya kibinadamu, bali kwa nguvu ya uhai ambao hauna mwisho.
17imi yura fell-as : Kečč d lmuqeddem i dayem am Malxisadeq.
17Maana Maandiko yasema: "Wewe ni kuhani milele, kufuatana na utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki."
18Lameṛ aqdim yeɛnan lmuqedmin yețwabeddel, axaṭer ixuṣṣ yerna ur yenfiɛ ara.
18Basi, ile amri ya zamani ilifutwa kwa sababu ilikuwa hafifu na isiyofaa kitu.
19Ccariɛa n Musa ur tezmir ara a ɣ-terr d iḥeqqiyen zdat Sidi Ṛebbi, meɛna yella yiwen usirem s wayes ara nqeṛṛeb ɣuṛ-es ;
19Maana Sheria ya Mose haikuweza kukamilisha jambo lolote. Lakini sasa, mahali pake pamewekwa tumaini lililo bora zaidi ambalo kwalo tunaweza kumkaribia Mungu.
20yerna ayagi yedṛa-d s limin n Sidi Ṛebbi, mačči am at Lewwi yuɣalen d lmuqedmin mbla limin ;
20Zaidi ya hayo hapa pana kiapo cha Mungu. Wakati wale wengine walipofanywa makuhani hapakuwako kiapo.
21ma d Sidna Ɛisa yesbedd-it Sidi Ṛebbi s limin mi s-yenna : Sidi Ṛebbi yeggul ur yeḥnit aț-țiliḍ d lmuqeddem i dayem .
21Lakini Yesu alifanywa kuhani kwa kiapo wakati Mungu alipomwambia: "Bwana ameapa, wala hataigeuza nia yake: Wewe ni kuhani milele."
22Ɛisa, d nețța i ɣ-iḍemnen lɛahed yifen amezwaru.
22Basi, kutokana na tofauti hii, Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.
23Aṭas seg wat Lewwi i gellan d lmuqedmin axaṭer lmut ur ten-tețțaǧa ara ad dumen di ccɣel-nsen ;
23Kuna tofauti nyingine pia: hao makuhani wengine walikuwa wengi kwa sababu walikufa na hawakuweza kuendelea na kazi yao.
24ma d Sidna Ɛisa, d win yețdumun, ur yuḥwaǧ ara a d-yeǧǧ lxedma-s n lmuqeddem i wayeḍ.
24Lakini Yesu si kama wao, yeye anaishi milele; ukuhani wake hauondoki kwake.
25Daymi i gezmer ad isellek di mkul lweqt wid akk yețqeṛṛiben ɣer Ṛebbi s yisem-is, imi nețța yedder i dayem, ideɛɛu fell-asen ɣer Sidi Ṛebbi.
25Hivyo, yeye anaweza daima kuwaokoa kabisa wote wanaomwendea Mungu kwa njia yake, maana yeye anaishi milele kuwaombea kwa Mungu.
26D wagi i d lmuqeddem ameqqran i ɣ-ilaqen, d imqeddes, d azedgan, ur yesɛi ara lɛib, yemxalaf d imdanen idenben yerna ițwarfed sennig igenwan.
26Basi, Yesu ndiye Kuhani Mkuu ambaye anatufaa sana katika mahitaji yetu. Yeye ni mtakatifu, hana hatia wala dhambi ndani yake; hayumo katika kundi la wenye dhambi na ameinuliwa mpaka juu mbinguni.
27Ur yeḥwaǧ ara ad yefk iseflawen am lmuqedmin nniḍen ɣef ddnubat-is neɣ ɣef wid n wegdud, lameɛna yefka iman-is d asfel yiwet n tikkelt kan ɣef ddemma n ddnubatnneɣ.
27Yeye si kama wale makuhani wakuu wengine; hana haja ya kutoa dhabihu kila siku, kwanza kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe, kisha kwa ajili ya dhambi za watu. Yeye alifanya hivyo mara moja tu wakati alipojitoa yeye mwenyewe, na hiyo yatosha kwa nyakati zote.
28Lmuqedmin imeqqranen i d tesbeddad ccariɛa, d irgazen ixuṣṣen di lǧehd, ma d win i gesbedd Sidi Ṛebbi s limin deffir ccariɛa, d Mmi-s i gessaweḍ ɣer tezmert tameqqrant i dayem.
28Sheria ya Mose huwateua watu waliokuwa dhaifu kuwa makuhani wakuu; lakini ahadi ya Mungu aliyoifanya kwa kiapo na ambayo imefika baada ya sheria imemteua Mwana ambaye amefanywa mkamilifu milele.