1 Walaɣ igenni d lqaɛa ijdiden, igenni aqdim d lqaɛa taqdimt xfan, lebḥur ur d-qqimen ara.
1Kisha nikaona mbingu mpya na dunia mpya. Mbingu ile ya kwanza na dunia ile ya kwanza vilikuwa vimetoweka, nayo bahari pia haikuweko tena.
2Walaɣ tamdint iqedsen tṣubb-ed seg igenni tekka-d s ɣuṛ Sidi Ṛebbi, ț-țagi i ț-țamdint n Lquds tajdiṭ, thegga am teslit icebbḥen iman-is i yesli.
2Nikaona mji mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka kwa Mungu mbinguni. Ulikuwa umetayarishwa vizuri kama bibi arusi aliyepambwa tayari kukutana na mumewe.
3Sliɣ i yiwet taɣect tenṭeq-ed s ṣṣut eɛlayen seg ukersi-nni n lḥekma tenna-d : Tura Sidi Ṛebbi yezdeɣ ger yemdanen, nutni ad ilin d agdud-is nețța s yiman-is ad yili yid-sen.
3Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka katika kiti cha enzi ikisema, "Tazama! Mungu amefanya makao yake kati ya watu. Atakaa kati yao, nao watakuwa watu wake, naye atakuwa Mungu wao.
4 A sen-yesfeḍ imeṭṭawen, ur tețțili lmut, ur yețțili leḥzen, ur yețțili umeǧǧed ur yețțili lqeṛḥ axaṭer leḥwayeǧ timezwura ɛeddant ur țɛawadent ara a d-țuɣalent.
4Yeye atayafuta machozi yao yote; maana hakutakuwako tena na kifo, wala uchungu, wala kilio, wala maumivu; maana ile hali ya kale imepita!"
5Win akken yeqqimen ɣef wukersi n lḥekma yenna : Tura rriɣ-ed kullec d ajdid. Yenna daɣen : Aru imeslayen-agi, axaṭer imeslayen-iw ṣeḥḥan yerna deg-sen lețkal.
5Kisha yule aliyeketi juu ya kiti cha enzi akasema, "Tazama, nafanya yote mapya." Tena akaniambia, "Andika hili, maana maneno haya ni ya kuaminika na ya kweli!"
6Yerna yenna-yi-d : Dayen ! Kullec yețwakemmel ! D nekk i d alfa d nekk i d umiga yeɛni d nekk i d lḥeṛf amezwaru, d nekk i d lḥeṛf aneggaru. Lliɣ si tazwara alamma ț-țaggara. Win iffuden, a s-d-fkeɣ aman si lɛinseṛ n tudert yerna baṭel.
6Kisha akaniambia, "Yametimia! Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Aliye na kiu nitampa kinywaji cha bure kutoka katika chemchemi ya maji ya uzima.
7Win yeṭṭfen deg-i ur yeɣli ara a t-kafiɣ s wayen yuklal ; nekk ad iliɣ d Illu-ines, nețța ad yili d mmi ;
7Yeyote atakayeshinda atapokea hiki, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.
8ma d ixeddaɛen, wid ur nețțamen ara, imejhal akk-d wid ineqqen timegṛaḍ, wid ixeddmen ticmatin akk d iseḥḥaren, wid iɛebden lmeṣnuɛat d ssadaț, imeskaddaben, wigi meṛṛa ad yili umur-nsen di temda n tmes ireqqen d ukebri. ?-țagi i d lmut tis snat.
8Lakini watu waoga, wasioamini, wapotovu, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, na waongo wote, mahali pao patakuwa ndani ya lile ziwa linalowaka moto na kiberiti; hicho ndicho kifo cha pili."
9Yiwen si sebɛa lmalayekkat-nni yeṭṭfen sebɛa teqbucin yeččuṛen d sebɛa lmuṣibat tineggura yusa-d yenna-yi-d : Eyya-d a k-d-sekneɣ tislit, tameṭṭut n Izimer.
9Kisha mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na yale mabakuli saba yaliyokuwa yamejaa mabaa saba ya mwisho, akaja na kuniambia, "Njoo! Mimi nitakuonyesha bibi arusi, mkewe Mwanakondoo!"
10Imiren irfed-iyi Ṛṛuḥ n Sidi Ṛebbi, ufiɣ-ed iman-iw ɣef yiwen wedrar ɛlayen. Isken-iyi-d tamdint n Lquds tețṣubbu-d seg igenni s ɣuṛ Sidi Ṛebbi.
10Basi, Roho akanikumba, naye malaika akanipeleka juu ya mlima mrefu sana. Akanionyesha mji mtakatifu, ukishuka kutoka kwa Mungu mbinguni,
11Tecceɛceɛ am lyaman yeṣfan yețṛeqṛiqen am djaj, ț-țamanegt n Sidi Ṛebbi i gersen fell-as.
11uking'aa kwa utukufu wa Mungu. Mwangaza wake ulikuwa kama wa jiwe la thamani kubwa kama yaspi, angavu kama kioo.
12Zzin-as-d leswaṛ ɛlayen yesɛan tnac tewwura, mkul yiwet ibedd zdat-es yiwen lmelk, uran ɣef tewwura-agi yismawen n tnac leɛṛac n wat Isṛail.
12Ulikuwa na ukuta mrefu na mkubwa, wenye milango kumi na miwili, na malaika wanangojea kumi na wawili. Majina ya wangoja milango kumi na mawili ya Israeli yalikuwa yameandikwa juu ya milango hiyo.
13Tlata tewwura wehhant ɣer cceṛq, tlata ɣer lɣeṛb, tlata ɣer usammer, tlata nniḍen ɣer umalu.
13Kila upande ulikuwa na milango mitatu: upande wa mashariki, milango mitatu, kaskazini milango mitatu, kusini milango mitatu na magharibi milango mitatu.
14Leswaṛ-nni ersen ɣef tnac lsisan i ɣef uran tnac yismawen n ṛṛusul n Izimer n Ṛebbi.
14Kuta za mji huo zilikuwa zimejengwa juu ya mawe ya msingi kumi na mawili, na juu ya mawe hayo yalikuwa yameandikwa majina na mitume kumi na wawili wa Mwanakondoo.
15Win akken i yi-d-ițmeslayen yeṭṭef aɣanim n ddheb iwakken ad yektil tamdint, tiwwura-ines d leswaṛ-is.
15Basi, yule malaika aliyekuwa anasema nami alikuwa na kijiti cha dhahabu cha kupimia, kwa ajili ya kuupima huo mji, milango yake na kuta zake.
16Tuɣzi ț-țehri n leḥyuḍ n temdint-nni ɛedlen. Yektal tamdint-nni, yufa lqis n tnac alef n wannaren ama di tuɣzi-ines, ama di tehri-ines, ama di leɛli-ines.
16Mji wenyewe ulikuwa wa mraba, upana na urefu wake sawa. Basi, malaika akaupima mji huo kwa kijiti chake: ulikuwa na urefu, upana na urefu wa kwenda juu, kama kilomita elfu mbili na mia nne.
17Lmelk yektal daɣen leɛli n leswaṛ n temdint s uɣanim-nni, yufa meyya uṛebɛa uṛebɛin alef n iɣallen.
17Kisha akaupima ukuta wake pia; nao ulikuwa mita sitini kwa kipimo cha macho cha kibinadamu ambacho malaika alitumia.
18Leswaṛ-is bnan s lyaman, ma ț-țamdint tebna s ddheb iṣfan yecban djaj yețṛeqṛiqen.
18Ukuta huo ulikuwa umejengwa kwa mawe mekundu ya thamani, na mji wenyewe ulikuwa umejengwa kwa dhahabu safi, angavu kama kioo.
19Lsisan n leswaṛ-is ṛeqqmen s yezṛa ɣlayen n mkul ṣṣenf. Amezwaru s Lyaman n Jasb, wis sin n Safir, wis tlata s lyaman n Agat, wis ṛebɛa n ?umṛud,
19Mawe ya msingi wa ukuta huo yalikuwa yamepambwa kwa kila aina ya mawe ya thamani. Jiwe la kwanza la msingi lilikuwa jiwe la thamani jekundu, la pili yakuti samawati, la tatu kalkedoni, la nne zamaradi,
20wis xemsa n Sardwan, wis sețța n Kurnalin, wis sebɛa n Krizulit, wis tmanya n Biril, wis tesɛa n Tubaz, wis ɛecṛa n Krisubraz, wis ḥdac n Turkwaz, wis tnac n Amitist.
20la tano sardoniki, la sita akiki, la saba krisolito, la nane zabarijadi, la tisa topazi, la kumi krisopraso, la kumi na moja yasinto, na la kumi na mbili amethisto.
21Tnac n tewwura-nni țwaxedment s tɛeqcin, mkul tawwurt ț-țaɛeqquct tameqqrant. Abṛaḥ n temdint-nni yessa s ddheb yeṣfan am djaj yețṛeqṛiqen.
21Na ile milango kumi na miwili ilikuwa lulu kumi na mbili; kila mlango ulikuwa umetengenezwa kwa lulu moja. Barabara kuu ya mji ilikuwa imetengenezwa kwa dhahabu safi, angavu kama kioo.
22Ur walaɣ ara lǧameɛ di temdint-nni axaṭer d Sidi Ṛebbi Bab n tezmert s yiman-is akk-d Izimer i d lǧameɛ-ines.
22Sikuona hekalu katika mji huo, maana Bwana Mungu Mwenye Uwezo na yule Mwanakondoo ndio Hekalu lake.
23Tamdint-agi ur teḥwaǧ iṭij, ur teḥwaǧ agur iwakken a s-d-fken tafat axaṭer ț-țamanegt n Sidi Ṛebbi i ț-ițnewwiṛen, yerna d Izimer i d lmeṣbeḥ-ines.
23Mji huo hauhitaji jua wala mwezi kuangazia, maana utukufu wa Mungu huuangazia, na taa yake ni yule Mwanakondoo.
24Leǧnas meṛṛa ad lḥun di tafat-is, igelliden n ddunit a d-asen ad seǧǧden, ad anzen zdat-es.
24Watu wa mataifa watatembea katika mwanga wake, na wafalme wa dunia watauletea utajiri wao.
25Tiwwura-ines ur ɣelqent ara maḍi axaṭer dinna ur d-yețțili ara yiḍ.
25Milango ya mji huo itakuwa wazi mchana wote; maana hakutakuwa na usiku humo.
26Leǧnas meṛṛa yesɛan ccan a d-asen ad seǧǧden zdat-es.
26Fahari na utajiri wa watu wa mataifa utaletwa humo ndani.
27Ur ikeččem ɣuṛ-es wayen ineǧsen, ur ikeččem ɣuṛ-es win ixeddmen cceṛ neɣ win yeskiddiben ; anagar wid yețțujerden di tektabt n tudert n Izimer ara ikecmen ɣer dinna.
27Lakini hakuna chochote kilicho najisi kitakachoingia humo; wala mtu yeyote atendaye mambo ya kuchukiza au ya uongo hataingia humo. Ni wale tu walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwanakondoo ndio watakaoingia ndani.