1형제들아 때와 시기에 관하여는 너희에게 쓸 것이 없음은
1Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.
2주의 날이 밤에 도적같이 이를 줄을 너희 자신이 자세히 앎이라
2Maana ninyi wenyewe mwajua kwamba Siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajavyo usiku.
3저희가 평안하다, 안전하다 할 그 때에 잉태된 여자에게 해산 고통이 이름과 같이 멸망이 홀연히 저희에게 이르리니 결단코 피하지 못하리라
3Watu watakapokuwa wanasema: "Kila kitu ni shwari na salama" ndipo uharibifu utakapowaangukia ghafla! Mambo hayo yatatukia ghafla kama uchungu wa uzazi unavyomjia mama anayejifungua, wala watu hawataweza kuepukana nayo.
4형제들아 너희는 어두움에 있지 아니하매 그 날이 도적같이 너희에게 임하지 못하리니
4Lakini ninyi ndugu, hamko gizani, na siku hiyo haipaswi kuwajieni ghafla kama vile mwizi.
5너희는 다 빛의 아들이요 낮의 아들이라 우리가 밤이나 어두움에 속하지 아니하나니
5Ninyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.
6그러므로 우리는 다른 이들과 같이 자지 말고 오직 깨어 근신할지라
6Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.
7자는 자들은 밤에 자고 취하는 자들은 밤에 취하되
7Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.
8우리는 낮에 속하였으니 근신하여 믿음과 사랑의 흉배를 붙이고 구원의 소망의 투구를 쓰자
8Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.
9하나님이 우리를 세우심은 노하심에 이르게 하심이 아니요 오직 우리 주 예수 그리스도로 말미암아 구원을 얻게 하신 것이라
9Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
10예수께서 우리를 위하여 죽으사 우리로 하여금 깨든지 자든지 자기와 함께 살게 하려 하셨느니라
10ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.
11그러므로 피차 권면하고 피차 덕을 세우기를 너희가 하는 것같이 하라
11Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana ninyi kwa ninyi kama mnavyofanya sasa.
12형제들아 우리가 너희에게 구하노니 너희 가운데서 수고하고 주 안에서 너희를 다스리며 권하는 자들을 너희가 알고
12Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.
13저의 역사로 말미암아 사랑 안에서 가장 귀히 여기며 너희끼리 화목하라
13Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa sababu ya kazi wanayofanya. Muwe na amani kati yenu.
14또 형제들아 너희를 권면하노니 규모없는 자들을 권계하며 마음이 약한 자들을 안위하고 힘이 없는 자들을 붙들어 주며 모든 사람을 대하여 오래 참으라
14Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.
15삼가 누가 누구에게든지 악으로 악을 갚지 말게 하고 오직 피차 대하든지 모든 사람을 대하든지 항상 선을 좇으라
15Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.
16항상 기뻐하라 !
16Furahini daima,
17쉬지 말고 기도하라 !
17salini kila wakati
18범사에 감사하라 ! 이는 그리스도 예수 안에서 너희를 향하신 하나님의 뜻이니라
18na muwe na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.
19성령을 소멸치 말며
19Msimpinge Roho Mtakatifu;
20예언을 멸시치 말고
20msidharau unabii.
21범사에 헤아려 좋은 것을 취하고
21Pimeni kila kitu: zingatieni kilicho chema,
22악은 모든 모양이라도 버리라 !
22na epukeni kila aina ya uovu.
23평강의 하나님이 친히 너희로 온전히 거룩하게 하시고 또 너희 온 영과 혼과 몸이 우리 주 예수 그리스도 강림하실 때에 흠 없게 보전되기를 원하노라
23Mungu anayetupatia amani awafanye ninyi watakatifu kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu--roho, mioyo na miili yenu--mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
24너희를 부르시는 이는 미쁘시니 그가 또한 이루시리라
24Yeye anayewaita ninyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.
25형제들아 우리를 위하여 기도하라
25Ndugu, tuombeeni na sisi pia.
26거룩하게 입맞춤으로 모든 형제에게 문안하라
26Wasalimuni ndugu wote kwa ishara ya upendo.
27내가 주를 힘입어 너희를 명하노니 모든 형제에게 이 편지를 읽어 들리라
27Nawahimizeni kwa jina la Bwana muwasomee ndugu zetu wote barua hii.
28우리 주 예수 그리스도의 은혜가 너희에게 있을지어다 !
28Tunawatakieni neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.