1Jėzus nuėjo į Alyvų kalną.
1lakini Yesu akaenda kwenye mlima wa Mizeituni.
2Anksti rytą Jis vėl atėjo į šventyklą. Visi žmonės rinkosi prie Jo, ir Jis atsisėdęs juos mokė.
2Kesho yake asubuhi na mapema alikwenda tena Hekaluni. Watu wote wakamwendea, naye akaketi akawa anawafundisha.
3Rašto žinovai ir fariziejai atvedė pas Jį moterį, sugautą svetimaujant. Pastatė ją viduryje
3Basi, walimu wa Sheria na Mafarisayo wakamletea mwanamke mmoja aliyefumaniwa katika uzinzi. Wakamsimamisha katikati yao.
4ir kreipėsi į Jį: “Mokytojau, ši moteris buvo pagauta svetimaujant.
4Kisha wakamwuliza Yesu, "Mwalimu! Mwanamke huyu alifumaniwa katika uzinzi.
5Mozė Įstatyme mums įsakė tokias užmėtyti akmenimis. O ką Tu pasakysi?”
5Katika Sheria yetu Mose alituamuru mwanamke kama huyu apigwe mawe. Basi, wewe wasemaje?"
6Jie tai sakė, mėgindami Jį, kad turėtų kuo apkaltinti. Bet Jėzus, jų nepaisydamas, pasilenkęs rašė pirštu ant žemės.
6Walisema hivyo kumjaribu, wapate kisa cha kumshtaki. Lakini Yesu akainama chini, akaandika ardhini kwa kidole.
7Jiems nesiliaujant klausinėti, Jis atsitiesė ir tarė: “Kas iš jūsų be nuodėmės, tegul pirmas sviedžia į ją akmenį”.
7Walipozidi kumwuliza, Yesu akainuka, akawaambia, "Mtu asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza kumpiga jiwe."
8Ir vėl pasilenkęs rašė ant žemės.
8Kisha akainama tena, akawa anaandika ardhini.
9Tai išgirdę, sąžinės apkaltinti jie vienas po kito ėmė trauktis šalin, pradedant nuo vyresniųjų iki paskutiniojo.
9Waliposikia hivyo, wakaanza kutoweka mmojammoja, wakitanguliwa na wazee. Yesu akabaki peke yake, na yule mwanamke amesimama palepale.
10Atsitiesęs ir nebematydamas nė vieno, tik moterį, Jėzus paklausė: “Moterie, kur tie tavo kaltintojai? Niekas tavęs nepasmerkė?”
10Yesu alipoinuka akamwuliza huyo mwanamke, "Wako wapi wale watu? Je, hakuna hata mmoja aliyekuhukumu?"
11Ji atsiliepė: “Niekas, Viešpatie”. Jėzus jai tarė: “Nė Aš tavęs nesmerkiu. Eik ir daugiau nebenusidėk”.
11Huyo mwanamke akamjibu, "Mheshimiwa, hakuna hata mmoja!" Naye Yesu akamwambia, "Wala mimi sikuhukumu. Nenda zako; na tangu sasa usitende dhambi tena."
12Jėzus vėl prabilo: “Ašpasaulio šviesa. Kas seka manimi, nebevaikščios tamsoje, bet turės gyvenimo šviesą”.
12Yesu alipozungumza nao tena, aliwaambia, "Mimi ndimi mwanga wa ulimwengu. Anayenifuata mimi hatembei kamwe gizani, bali atakuwa na mwanga wa uzima."
13Tada fariziejai Jam pasakė: “Tu pats apie save liudiji,tavo liudijimas netikras”.
13Basi, Mafarisayo wakamwambia, "Wewe unajishuhudia mwenyewe; kwa hiyo ushahidi wako si halali."
14Jėzus jiems atsakė: “Nors Aš ir liudiju pats apie save, mano liudijimas yra tikras, nes Aš žinau, iš kur atėjau ir kur einu. O jūs nežinote, nei iš kur Aš atėjau, nei kur einu.
14Yesu akawajibu, "Hata kama ninajishuhudia mwenyewe, ushahidi wangu ni wa kweli kwa sababu mimi najua nilikotoka na ninakokwenda. Lakini ninyi hamjui nilikotoka wala ninakokwenda.
15Jūs teisiate pagal kūną, Aš neteisiu nė vieno.
15Ninyi mnahukumu kwa fikira za kibinadamu, lakini mimi simhukumu mtu.
16O jeigu Aš ir teisiumano teismas teisingas, nes Aš ne vienas, bet esu Aš ir mane siuntęs Tėvas.
16Hata nikihukumu, hukumu yangu ni ya haki kwa sababu mimi siko peke yangu; Baba aliyenituma yuko pamoja nami.
17Ir jūsų Įstatyme parašyta, kad dviejų asmenų liudijimas tikras.
17Imeandikwa katika Sheria yenu ya kwamba ushahidi wa watu wawili ni halali.
18Aš liudiju pats apie save, ir apie mane liudija mane siuntęs Tėvas”.
18Mimi najishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenituma, ananishuhudia pia."
19Jie paklausė: “Kur yra Tavo Tėvas?” Jėzus atsakė: “Jūs nepažįstate nei manęs, nei mano Tėvo. Jei pažintumėte mane, pažintumėte ir mano Tėvą”.
19Hapo wakamwuliza, "Baba yako yuko wapi?" Yesu akawajibu "Ninyi hamnijui mimi wala hamumjui Baba. Kama mngenijua mimi, mngemjua na Baba yangu pia."
20Šiuos žodžius Jėzus pasakė, mokydamas šventyklos iždinėje. Ir niekas Jo nesuėmė, nes dar nebuvo atėjusi Jo valanda.
20Yesu alisema maneno hayo kwenye chumba cha hazina alipokuwa anafundisha Hekaluni. Wala hakuna mtu aliyemtia nguvuni, kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
21Jėzus vėl jiems kalbėjo: “Aš išeinu, ir jūs ieškosite manęs ir mirsite savo nuodėmėse. Kur Aš einu, jūs negalite nueiti”.
21Yesu akawaambia tena, "Naenda zangu nanyi mtanitafuta, lakini mtakufa katika dhambi zenu. Niendako mimi, ninyi hamwezi kufika."
22Tada žydai ėmė kalbėti: “Nejaugi Jis nusižudys, kad sako: ‘Kur Aš einu, jūs negalite nueiti’?”
22Basi, viongozi wa Wayahudi wakasema, "Je, atajiua? Mbona anasema: Niendako ninyi hamwezi kufika?"
23Jis atsakė: “Jūs esate iš pažemių, o Aš esu iš aukštybės. Jūsiš šio pasaulio, o Ašne iš šio pasaulio.
23Yesu akawaambia, "Ninyi mmetoka papa hapa chini, mimi nimetoka juu; ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.
24Dėl to Aš jums sakiau, kad mirsite savo nuodėmėse. Jeigu netikėsite, kad Aš Esu,mirsite savo nuodėmėse”.
24Ndiyo maana niliwaambieni mtakufa katika dhambi zenu. Kama msipoamini kwamba Mimi ndimi, mtakufa katika dhambi zenu."
25Tada jie klausė: “Kas Tu esi?” Jėzus atsakė: “Tas, ką nuo pradžios jums sakiau.
25Nao wakamwuliza, "Wewe ni nani?" Yesu akawajibu, "Nimewaambieni tangu mwanzo!
26Daug turiu ką apie jus kalbėti ir teisti, bet teisingas yra mano Siuntėjas, ir Aš skelbiu pasauliui, ką iš Jo girdėjau”.
26Ninayo mengi ya kusema na kuhukumu juu yenu. Lakini yule aliyenituma ni kweli; nami nauambia ulimwengu mambo yale tu niliyoyasikia kutoka kwake."
27Jie nesuprato, kad Jis kalbėjo jiems apie Tėvą.
27Hawakuelewa kwamba Yesu alikuwa akisema nao juu ya Baba.
28O Jėzus tęsė: “Kai Žmogaus Sūnų būsite aukštyn iškėlę, tuomet suprasite, kad Aš Esu ir kad nieko nedarau iš savęs, bet skelbiu tai, ko mane Tėvas išmokė.
28Basi, Yesu akawaambia, "Mtakapokwisha mwinua Mwana wa Mtu hapo ndipo mtakapojua kwamba Mimi ndimi, na kwamba sifanyi chochote mimi mwenyewe, ila nasema tu yale Baba aliyonifundisha.
29Mano Siuntėjas yra su manimi; Tėvas nepaliko manęs vieno, nes visuomet darau, kas Jam patinka”.
29Yule aliyenituma yuko pamoja nami; yeye hakuniacha peke yangu kwani nafanya daima yale yanayompendeza."
30Jam tai kalbant, daugelis įtikėjo Jį.
30Baada ya kusema hayo watu wengi walimwamini.
31Jėzus kalbėjo įtikėjusiems Jį žydams: “Jei jūs pasiliekate mano žodyje, iš tiesų esate mano mokiniai;
31Basi, Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, "Kama mkiyazingatia mafundisho yangu mtakuwa kweli wanafunzi wangu.
32ir jūs pažinsite tiesą, ir tiesa padarys jus laisvus”.
32Mtaujua ukweli, nao ukweli utawapeni uhuru."
33Jie Jam atsakė: “Mes esame Abraomo palikuonys ir niekada niekam nevergavome. Kaipgi Tu sakai: ‘Tapsite laisvi’?”
33Nao wakamjibu, "Sisi ni wazawa wa Abrahamu, na hatujapata kamwe kuwa watumwa wa mtu yeyote yule. Una maana gani unaposema: mtakuwa huru?"
34Jėzus jiems tarė: “Iš tiesų, iš tiesų sakau jums: kiekvienas, kas daro nuodėmę, yra nuodėmės vergas.
34Yesu akawajibu, "Kweli nawaambieni, kila mtu anayetenda dhambi ni mtumwa wa dhambi.
35Bet vergas nepasilieka namuose amžinai, o Sūnus pasilieka amžinai.
35Mtumwa hana makao ya kudumu nyumbani, lakini mwana anayo makao ya kudumu.
36Jei tad Sūnus jus išlaisvins, iš tiesų būsite laisvi.
36Kama mwana akiwapeni uhuru mtakuwa huru kweli.
37Aš žinau, kad jūs Abraomo palikuonys. Bet jūs norite mane nužudyti, nes mano žodžiui nėra jumyse vietos.
37Najua kwamba ninyi ni wazawa wa Abrahamu. Hata hivyo, mnataka kuniua kwa sababu hamuyakubali mafundisho yangu.
38Aš kalbu, ką esu matęs pas savo Tėvą. O jūs darote, ką matėte pas savo tėvą”.
38Mimi nasema yale aliyonionyesha Baba, lakini ninyi mwafanya yale aliyowaambieni baba yenu."
39Jie atsiliepė: “Mūsų tėvas Abraomas!” Jėzus jiems tarė: “Jei jūs būtumėte Abraomo vaikai, darytumėte Abraomo darbus.
39Wao wakamjibu, "Baba yetu ni Abrahamu!" Yesu akawaambia, "Kama ninyi mngekuwa watoto wa Abrahamu, mngefanya kama alivyofanya Abrahamu,
40Bet dabar jūs norite nužudyti manežmogų, kuris kalbėjo jums tiesą, girdėtą iš Dievo. Šitaip Abraomas nedarė!
40Mimi nimewaambieni ukweli niliousikia kwa Mungu; hata hivyo, ninyi mwataka kuniua. Abrahamu hakufanya hivyo!
41Jūs darote savo tėvo darbus”. Jie atsakė: “Mes nesame pavainikiai ir turime vieną TėvąDievą”.
41Ninyi mnafanya mambo yaleyale aliyofanya babu yenu." Wao wakamwambia, "Sisi si watoto haramu! Tunaye baba mmoja tu, yaani Mungu."
42Jėzus kalbėjo jiems toliau: “Jei Dievas būtų jūsų Tėvas, jūs mylėtumėte mane, nes Aš iš Dievo išėjau ir čia atėjau. Aš ne pats nuo savęs atėjau, bet Jis mane siuntė.
42Yesu akawaambia, "Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda mimi, maana mimi nilitoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe, ila yeye alinituma.
43Kodėl gi nesuprantate, ką jums sakau? Todėl, kad negalite mano žodžių klausyti.
43Kwa nini hamwelewi hayo ninayosema? Ni kwa kuwa hamwezi kuusikiliza ujumbe wangu.
44Jūsų tėvasvelnias, ir jūs norite vykdyti savo tėvo troškimus. Jis nuo pat pradžios buvo žmogžudys ir nesilaikė tiesos, nes jame nėra tiesos. Kalbėdamas melą, jis kalba, kas jam sava, nes jis melagis ir melo tėvas.
44Ninyi ni watoto wa baba yenu Ibilisi na mnataka tu kutekeleza tamaa za baba yenu. Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo; hana msimamo katika ukweli, kwani ukweli haumo ndani yake. Kila asemapo uongo, husema kutokana na hali yake ya maumbile, maana yeye ni mwongo na baba wa uongo.
45O kadangi Aš kalbu tiesą, jūs netikite manimi.
45Mimi nasema ukweli, na ndiyo maana ninyi hamniamini.
46Kas iš jūsų apkaltins mane nuodėme? Jeigu tad tiesą sakau, kodėl netikite manimi?
46Nani kati yenu awezaye kuthibitisha kuwa mimi nina dhambi? Ikiwa basi nasema ukweli, kwa nini hamniamini?
47Kas iš Dievo yra, tas Dievo žodžių klauso. Jūs neklausote todėl, kad nesate iš Dievo”.
47Aliye wa Mungu husikiliza maneno ya Mungu. Lakini ninyi hamsikilizi kwa sababu ninyi si (watu wa) Mungu."
48Tuomet žydai atsiliepė: “Argi mes ne teisingai sakome, kad Tu samarietis ir Tavyje demonas?”
48Wayahudi wakamwambia, "Je, hatukusema kweli kwamba wewe ni Msamaria, na tena una pepo?"
49Jėzus jiems atsakė: “Nėra manyje demono. Aš gerbiu savo Tėvą, o jūs negerbiate manęs.
49Yesu akajibu, "Mimi sina pepo; mimi namheshimu Baba yangu, lakini ninyi hamniheshimu.
50Aš neieškau sau šlovės: yra, kas ieško ir teisia.
50Mimi sijitafutii utukufu wangu mwenyewe; yuko mmoja mwenye kuutafuta utukufu huo, naye ni hakimu.
51Iš tiesų, iš tiesų sakau jums: kas laikysis mano žodžio, nematys mirties per amžius”.
51Kweli nawaambieni, anayeuzingatia ujumbe wangu hatakufa milele."
52Žydai Jam pasakė: “Dabar mes žinome, kad Tu demono apsėstas! Juk mirė Abraomas ir pranašai, o Tu sakai: ‘Kas laikysis mano žodžio, tas neragaus mirties per amžius’.
52Basi, Wayahudi wakasema, "Sasa tunajua kweli kwamba wewe ni mwendawazimu! Abrahamu alikufa, na manabii pia walikufa, nawe wasema ati, Anayeuzingatia ujumbe wangu hatakufa milele!
53Argi Tu didesnis už mūsų tėvą Abraomą, kuris mirė? Pranašai irgi mirė. Kuo Tu dediesi?”
53Je, unajifanya mkuu zaidi kuliko baba yetu Abrahamu ambaye alikufa? Hata na manabii walikufa. Wewe unajifanya kuwa nani?"
54Jėzus atsakė: “Jei Aš save šlovinčiau, mano šlovė būtų niekai. Mane šlovina mano Tėvas, apie kurį jūs sakote: ‘Jis yra mūsų Dievas’.
54Yesu akawajibu, "Nikijitukuza mwenyewe, utukufu wangu si kitu. Baba yangu ambaye ninyi mwasema ni Baba yenu, ndiye anayenitukuza.
55Ir jūs Jo nepažįstate, o Aš Jį pažįstu. Jei sakyčiau, kad Jo nepažįstu, būčiau toks kaip jūsmelagis. Bet Aš Jį pažįstu ir laikausi Jo žodžio.
55Ninyi hamjapata kumjua, lakini mimi namjua. Na, nikisema simjui, nitakuwa mwongo kama ninyi. Mimi namjua na ninashika neno lake.
56Jūsų tėvas Abraomas džiūgavo, kad matysiąs manąją dieną; jis ją išvydo ir džiaugėsi”.
56Abrahamu, baba yenu, alishangilia aione siku yangu; naye aliiona, akafurahi."
57Tada žydai Jam sakė: “Dar neturi nė penkiasdešimt metų ir esi matęs Abraomą?!”
57Basi, Wayahudi wakamwambia, "Wewe hujatimiza miaka hamsini bado, nawe umemwona Abrahamu?"
58Jėzus jiems tarė: “Iš tiesų, iš tiesų sakau jums: pirmiau, negu buvo Abraomas, Aš Esu!”
58Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, kabla Abrahamu hajazaliwa, mimi niko."
59Tada jie griebėsi akmenų, norėdami mesti į Jį, bet Jėzus pasislėpė ir, praeidamas pro juos, išėjo iš šventyklos ir nuėjo tolyn.
59Hapo wakaokota mawe ili wamtupie, lakini Yesu akajificha, akatoka Hekaluni.