1Jėzus kalbėjo ir savo mokiniams: “Buvo vienas turtingas žmogus ir turėjo ūkvedį. Tas buvo jam apskųstas, esą eikvojąs jo turtą.
1Yesu aliwaambia wanafunzi wake: "Tajiri mmoja alikuwa na karani wake. Huyu karani alichongewa kwamba alitumia ovyo mali ya tajiri wake.
2Tuomet, pasišaukęs jį, šeimininkas pasakė: ‘Ką aš girdžiu apie tave šnekant? Duok savo ūkvedžiavimo apyskaitą, nes daugiau nebegalėsi būti ūkvedžiu’.
2Yule tajiri akamwita akamwambia: Ni mambo gani haya ninayosikia juu yako? Toa hesabu ya mapato na matumizi ya mali yangu, kwa maana huwezi kuwa karani tena.
3O ūkvedys tarė sau: ‘Ką veiksiu, kad šeimininkas atima iš manęs ūkvedžiavimą? Kasti neįstengiu, o elgetautigėda.
3Yule karani akafikiri: Bwana wangu amenifukuza kazi ya ukarani; nitafanya nini? Kwenda kulima siwezi; kwenda kuombaomba kama maskini ni aibu.
4Žinau, ką daryti, kad žmonės mane priimtų į savo namus, kai būsiu atleistas iš tarnybos’.
4Naam, najua la kufanya, ili nitakapofukuzwa kazi, watu waweze kunikaribisha nyumbani kwao.
5Jis pasikvietė po vieną savo šeimininko skolininkus ir klausė pirmąjį: ‘Kiek esi skolingas mano šeimininkui?’
5Basi, akawaita wadeni wa bwana wake, mmoja mmoja, akamwambia yule wa kwanza: Unadaiwa kiasi gani na bwana wangu?
6Šis atsakė: ‘Šimtą statinių aliejaus’. Tada jis tarė: ‘Imk savo skolos raštą, sėsk ir tuoj pat rašyk: penkiasdešimt’.
6Yeye akamjibu: Mapipa mia ya mafuta ya zeituni. Yule karani akamwambia: Chukua hati yako ya deni, keti haraka, andika hamsini.
7Paskui klausė kitą: ‘O kiek tu skolingas?’ Anas atsakė: ‘Šimtą saikų kviečių’. Jis tarė: ‘Imk skolos raštą ir rašyk: aštuoniasdešimt’.
7Kisha akamwuliza mdeni mwingine: Wewe unadaiwa kiasi gani? Yeye akamjibu: Magunia mia ya ngano. Yule karani akamwambia: Chukua hati yako ya deni, andika themanini.
8Šeimininkas pagyrė neteisųjį ūkvedį, kad jis gudriai pasielgė. Šio pasaulio vaikai sumanesni tarp savųjų negu šviesos vaikai”.
8"Basi, yule bwana akamsifu huyo karani asiye mwaminifu, kwa kuwa alitumia busara. Kwa maana watu wa dunia hii wana busara zaidi na mambo yao kuliko watu wa mwanga."
9“Ir Aš jums sakau: darykitės bičiulių neteisiosios Mamonos dėka, kad, jūsų galui atėjus, jie priimtų jus į amžinuosius namus.
9Naye Yesu akaendelea kusema, "Nami nawaambieni, jifanyieni marafiki kutokana na mali ya dunia, ili zitakapowaishieni, mweze kupokewa nao katika makao ya milele.
10Kas ištikimas mažame dalyke, tas ištikimas ir dideliame, o kas neteisingas mažame, tas neteisingas ir dideliame.
10Yeyote aliye mwaminifu katika mambo madogo, atakuwa mwaminifu katika mambo makubwa; na yeyote asiye mwaminifu katika mambo madogo, hatakuwa mwaminifu katika mambo makubwa.
11Jei nebuvote ištikimi, tvarkydami neteisiąją Mamoną, tai kas jums patikės tikruosius turtus?
11Kama basi, ninyi si hamjawa waaminifu mali mbaya za dunia, ni nani atakayewakabidhi zile mali za kweli?
12Ir jeigu nebuvote ištikimi su svetimu daiktu, tai kas jums duos tai, kas jūsų?
12Na kama hamjakuwa waaminifu katika mali ya mtu mwingine, ni nani atakayewakabidhi mali yenu wenyewe?
13Joks tarnas negali tarnauti dviem šeimininkams, nes jis arba vieno nekęs, o kitą mylės, arba prie vieno prisiriš, o kitą nieku vers. Negalite tarnauti Dievui ir Mamonai”.
13"Hakuna mtumishi awezaye kuwatumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia mmoja na kumpenda mwingine, au ataambatana na mmoja na kumdharau mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali."
14Visa tai girdėjo mėgstantys pinigus fariziejai ir šaipėsi iš Jėzaus.
14Lakini Mafarisayo waliposikia hayo, kwa vile wao walikuwa wanapenda sana fedha, wakamdharau Yesu.
15O Jis jiems pasakė: “Jūs žmonių akyse dedatės teisūs, bet Dievas mato jūsų širdis. Nes tai, kas žmonėse aukštinama, Dievo akyse bjauru”.
15Hapo akawaambia, "Ninyi mnajifanya wema mbele ya watu, lakini Mungu anaijua mioyo yenu. Kwa maana kile kinachoonekana kuwa kitukufu mbele ya watu, Mungu anakiona kuwa takataka.
16“Įstatymas ir pranašaiiki Jono; nuo tada skelbiama Dievo karalystė, ir kiekvienas į ją veržiasi.
16"Sheria na maandishi ya manabii vilikuweko mpaka wakati wa Yohane mbatizaji. Tangu hapo, Ufalme wa Mungu unahubiriwa, na kila mmoja anauingia kwa nguvu.
17Greičiau dangus ir žemė praeis, negu iš Įstatymo iškris bent vienas brūkšnelis.
17Lakini ni rahisi zaidi mbingu na dunia kupita, kuliko hata herufi moja ya Sheria kufutwa.
18Kiekvienas, kuris atleidžia žmoną ir veda kitąsvetimauja. Ir kas veda vyro atleistąją, taip pat svetimauja”.
18"Yeyote anayemwacha mke wake na kuoa mwingine, anazini; na yeyote anayemwoa mwanamke aliyepewa talaka, anazini.
19“Gyveno vienas turtuolis. Jis vilkėjo purpuru bei ploniausia drobe ir kasdien ištaigingai linksminosi.
19"Palikuwa na mtu mmoja tajiri, ambaye alikuwa anavaa mavazi ya bei kubwa sana ya rangi ya zambarau, na ya kitani safi, na kufanya sherehe kila siku.
20O prie jo vartų gulėjo votimis aptekęs elgeta, vardu Lozorius.
20Kulikuwa pia na maskini mmoja jina lake Lazaro, aliyekuwa amejaa vidonda na alikuwa analazwa mlangoni pa nyumba ya huyo tajiri.
21Jis troško numarinti alkį bent trupiniais nuo turtuolio stalo, bet tik šunys atbėgę laižydavo jo votis.
21Lazaro alitamani kula makombo yaliyoanguka kutoka meza ya tajiri; na zaidi ya hayo, mbwa walikuwa wanakuja na kulamba vidonda vyake!
22Ir štai elgeta mirė ir buvo angelų nuneštas į Abraomo prieglobstį. Mirė ir turtuolis ir buvo palaidotas.
22"Ikatokea kwamba huyo maskini akafa, malaika wakamchukua, wakamweka karibu na Abrahamu. Na yule tajiri pia akafa, akazikwa.
23Kentėdamas pragare, jis pakėlė akis ir iš tolo pamatė Abraomą ir jo prieglobstyje Lozorių.
23Huyo tajiri, alikuwa na mateso makali huko kuzimu, akainua macho yake, akamwona Abrahamu kwa mbali na Lazaro karibu naye.
24Jis ėmė šaukti: ‘Tėve Abraomai, pasigailėk manęs! Atsiųsk Lozorių, kad, suvilgęs vandenyje piršto galą, atvėsintų man liežuvį, nes baisiai kenčiu šioje liepsnoje’.
24Basi, akaita kwa sauti: Baba Abrahamu, nionee huruma; umtume Lazaro angalau achovye ncha ya kidole chake katika maji, auburudishe ulimi wangu, maana ninateseka mno katika moto huu.
25Bet Abraomas atsakė: ‘Atsimink, sūnau, kad tu gyvendamas atsiėmei savo gėrybes, o Lozoriustik nelaimes. Todėl jis susilaukė paguodos, o tu kenti.
25Lakini Abrahamu akamjibu: Kumbuka mwanangu, kwamba ulipokea mema yako katika maisha, naye Lazaro akapokea mabaya. Sasa lakini, yeye anatulizwa, nawe unateswa.
26Be to, mus nuo jūsų skiria milžiniška praraja, ir niekas iš čia panorėjęs negali nueiti pas jus, nei iš ten persikelti pas mus’.
26Licha ya hayo, kati yetu na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wanaotaka kuja kwenu kutoka huku wasiweze, wala wanaotaka kutoka kwenu kuja kwetu wasiweze.
27Tas vėl tarė: ‘Tai meldžiu tave, tėve, nusiųsk jį bent į mano tėvo namus,
27Huyo aliyekuwa tajiri akasema: Basi baba, nakuomba umtume aende nyumbani kwa baba yangu,
28nes aš turiu penkis brolius. Teįspėja juos, kad ir jie nepatektų į šią kančių vietą’.
28maana ninao ndugu watano, ili awaonye wasije wakaja huku kwenye mateso.
29Abraomas atsiliepė: ‘Jie turi Mozę bei pranašus, tegul jų klauso!’
29Lakini Abrahamu akamwambia: Ndugu zako wanao Mose na manabii; waache wawasikilize hao.
30O anas atsakė: ‘Ne, tėve Abraomai! Bet jei kas iš mirusiųjų nueitų pas juos, jie atgailautų!’
30Lakini yeye akasema: Sivyo baba Abrahamu, ila kama mtu atafufuka kutoka wafu na kuwaendea, watatubu.
31Tačiau Abraomas tarė: ‘Jeigu jie neklauso Mozės ir pranašų, tai nepatikės, jei kas ir iš numirusių prisikeltų’ ”.
31Naye Abrahamu akasema: Kama hawawasikilizi Mose na manabii, hawatajali hata kama mtu angefufuka kutoka wafu."