1Pirmąją savaitės dieną, vos brėkštant, jos atėjo prie kapo, nešdamos paruoštus tepalus.
1Jumapili, alfajiri na mapema, wale wanawake walikwenda kaburini wakichukua yale manukato waliyotayarisha.
2Jos rado akmenį nuritintą nuo kapo,
2Walikuta lile jiwe limeviringishwa mbali na kaburi.
3o įėjusios vidun, neberado Viešpaties Jėzaus kūno.
3Walipoingia ndani, hawakuona mwili wa Bwana Yesu.
4Moterys apstulbo ir nežinojo, ką daryti. Ir štai prie jų atsirado du vyrai spindinčiais drabužiais.
4Walipokuwa bado wanashangaa juu ya jambo hilo, mara watu wawili waliovaa mavazi yenye kung'aa sana, wakasimama karibu nao.
5Jos išsigando ir nuleido akis, o tie vyrai tarė: “Kam ieškote gyvojo tarp mirusiųjų?
5Hao wanawake wakaingiwa na hofu, wakainama chini. Ndipo wale watu wakawaambia, "Kwa nini mnamtafuta aliye hai kati ya wafu?
6Nėra Jo čia, Jis prisikėlė! Atsiminkite, ką Jis jums sakė, būdamas dar Galilėjoje:
6Hayuko hapa; amefufuka. Kumbukeni aliyowaambieni alipokuwa kule Galilaya:
7‘Žmogaus Sūnus turi būti atiduotas į nusidėjėlių rankas ir nukryžiuotas, o trečią dieną prisikelti!’ ”
7Ni lazima Mwana wa Mtu atolewe kwa watu waovu, nao watamsulubisha, na siku ya tatu atafufuka."
8Tuomet jos prisiminė Jėzaus žodžius
8Hapo wanawake wakayakumbuka maneno yake,
9ir, sugrįžusios nuo kapo, viską pranešė vienuolikai ir visiems kitiems.
9wakarudi kutoka kaburini, wakawapa mitume wale kumi na mmoja na wengine habari za mambo hayo yote.
10Tai buvo Marija Magdalietė, Joana, Jokūbo motina Marija ir kitos su jomis, kurios papasakojo tai apaštalams.
10Hao waliotoa habari hizo kwa mitume ni: Maria Magdalene, Yoana na Maria mama wa Yakobo, pamoja na wanawake wengine walioandamana nao.
11Jų žodžiai jiems pasirodė esą tuščios šnekos, ir jie moterimis nepatikėjo.
11Mitume waliyachukua maneno hayo kama yasiyo na msingi, hivyo hawakuamini.
12Vis dėlto Petras pakilęs nubėgo prie kapo ir pasilenkęs pamatė tiktai drobules. Jis grįžo atgal, labai stebėdamasis tuo, kas atsitiko.
12Lakini Petro alitoka, akaenda mbio hadi kaburini. Alipoinama kuchungulia ndani, akaiona tu ile sanda. Akarudi nyumbani huku akiwa anashangaa juu ya hayo yaliyotokea.
13Ir štai du iš jų tą pačią dieną keliavo į kaimą už šešiasdešimties stadijų nuo Jeruzalės, vadinamą Emausu.
13Siku hiyohiyo, wawili kati ya wafuasi wake Yesu wakawa wanakwenda katika kijiji kimoja kiitwacho Emau, umbali wa kilomita kumi na moja kutoka Yerusalemu.
14Jie kalbėjosi apie visus tuos įvykius.
14Wakawa wanazungumza juu ya hayo yote yaliyotukia.
15Jiems taip besikalbant ir besvarstant, prisiartino pats Jėzus ir ėjo kartu.
15Walipokuwa wakizungumza na kujadiliana, Yesu mwenyewe akatokea, akatembea pamoja nao.
16Jų akys buvo uždengtos, ir jie Jo neatpažino.
16Walimwona kwa macho, lakini hawakumtambua.
17O Jis paklausė jų: “Apie ką kalbatės, eidami nuliūdę?”
17Akawauliza, "Mnazungumza nini huku mnatembea?" Nao wakasimama kimya, nyuso zao wamezikunja kwa huzuni.
18Vienas iš jų, vardu Kleopas, atsakė Jam: “Nejaugi Tu esi vienintelis ateivis Jeruzalėje ir nežinai, kas joje šiomis dienomis atsitiko?”
18Mmoja, aitwaye Kleopa, akamjibu, "Je, wewe ni mgeni peke yako Yerusalemu ambaye hujui yaliyotukia huko siku hizi?"
19Jėzus paklausė: “O kas gi?” Jie tarė Jam: “Su Jėzumi iš Nazareto, kuris buvo pranašas, galingas darbais ir žodžiais Dievo ir visos tautos akyse.
19Naye akawajibu, "Mambo gani?" Wao wakamjibu, "Mambo yaliyompata Yesu wa Nazareti. Yeye alikuwa nabii mwenye uwezo wa kutenda na kufundisha mbele ya Mungu na mbele ya watu wote.
20Aukštieji kunigai ir mūsų vadovai Jį pasmerkė mirti ir nukryžiavo.
20Makuhani na watawala wetu walimtoa ahukumiwe kufa, wakamsulubisha.
21O mes vylėmės, kad Jis yra Tas, kuris atpirks Izraelį. Dabar po viso to jau trečia diena, kaip tai atsitiko.
21Lakini sisi tulitumaini kwamba yeye ndiye angeikomboa Israeli. Zaidi ya hayo yote, leo ni siku ya tatu tangu mambo hayo yalipotendeka.
22Be to, kai kurios mūsiškės moterys mus labai nustebino. Anksti rytą jos buvo nuėjusios pažiūrėti kapo
22Tena, wanawake wengine wa kwetu wametushtua. Walikwenda kaburini mapema asubuhi,
23ir nerado Jo kūno. Jos sugrįžo ir papasakojo regėjusios angelus, kurie sakę Jį esant gyvą.
23wasiukute mwili wake. Wakarudi wakasema kwamba walitokewa na malaika waliowaambia kwamba alikuwa hai.
24Kai kurie iš mūsiškių buvo nuėję prie kapo ir rado viską, kaip moterys sakė, bet Jo paties nematė”.
24Wengine wetu walikwenda kaburini wakashuhudia yale waliyosema hao wanawake; ila yeye hawakumwona."
25Tada Jis jiems tarė: “O jūs, neišmanėliai! Kokios nerangios jūsų širdys tikėti tuo, ką yra skelbę pranašai!
25Kisha Yesu akawaambia, "Mbona mu wapumbavu kiasi hicho na mioyo yenu ni mizito hivyo kusadiki yote yaliyonenwa na manabii?
26Argi ne taip turėjo Kristus kentėti ir įeiti į savo šlovę?”
26Je, haikumpasa Kristo kuteswa, na hivyo aingie katika utukufu wake?"
27Ir, pradėjęs nuo Mozės, primindamas visus pranašus, Jis aiškino jiems, kas visuose Raštuose apie Jį pasakyta.
27Akawafafanulia mambo yote yaliyomhusu yeye katika Maandiko Matakatifu kuanzia Mose hadi manabii wote.
28Jie prisiartino prie kaimo, į kurį keliavo, ir Jis dėjosi einąs toliau.
28Walipokikaribia kile kijiji walikokuwa wanakwenda, Yesu akafanya kana kwamba anaendelea na safari;
29Bet jie sulaikė Jį, sakydami: “Pasilik su mumis! Vakaras arti, diena jau baigiasi”. Jis užsuko ir pasiliko su jais.
29lakini wao wakamsihi wakisema, "Kaa pamoja nasi, maana kunakuchwa, na usiku unakaribia." Basi, akaingia kijijini, akakaa pamoja nao.
30Atsisėdęs su jais prie stalo, paėmė duoną, laimino, laužė ir davė jiems.
30Alipoketi kula chakula pamoja nao, akachukua mkate, akaubariki, akaumega, akawapa.
31Tada jų akys atsivėrė, ir jie pažino Jėzų, bet Jis pranyko jiems iš akių.
31Mara macho yao yakafumbuliwa, wakamtambua; lakini yeye akatoweka kati yao.
32O jie kalbėjo: “Argi mūsų širdys nedegė, kai Jis kelyje mums kalbėjo ir atvėrė Raštų prasmę?”
32Basi, wakaambiana, "Je, mioyo yetu haikuwa inawaka ndani yetu wakati alipokuwa anatufafanulia Maandiko Matakatifu kule njiani?"
33Jie tuoj pat pakilo ir sugrįžo į Jeruzalę. Ten jie rado susirinkusius vienuolika ir kitus su jais,
33Wakaondoka saa ileile, wakarudi Yerusalemu: wakawakuta wale mitume kumi na mmoja na wale wengine waliokuwa pamoja nao, wamekusanyika
34kurie tvirtino: “Viešpats tikrai prisikėlė ir pasirodė Simonui!”
34wakisema, "Hakika Bwana amefufuka, amemtokea Simoni."
35O jie papasakojo, kas jiems atsitiko kelyje ir kaip jie pažino Jėzų, kai Jis laužė duoną.
35Basi, hao wafuasi wawili wakawajulisha yale yaliyowapata njiani, na jinsi walivyomtambua katika kumega mkate.
36Jiems apie tai bekalbant, Jis pats atsirado tarp jų ir tarė: “Ramybė jums!”
36Wanafunzi wote wawili walipokuwa wakiwaambia hayo, Yesu mwenyewe akasimama kati yao, akawaambia "Amani kwenu."
37Sutrikę ir išsigandę, jie tarėsi matą dvasią.
37Wakashtuka na kushikwa na hofu wakidhani wameona mzimu.
38O Jis paklausė: “Ko taip sutrikote? Kodėl jūsų širdyse kyla abejonės?
38Lakini yeye akawaambia, "Kwa nini mnafadhaika? Mbona mnakuwa na mashaka mioyoni mwenu?
39Pasižiūrėkite į mano rankas ir kojas. Juk tai Aš pats! Palieskite mane ir įsitikinsite: dvasia juk neturi kūno nei kaulų, kaip matote mane turint”.
39Angalieni mikono na miguu yangu, ya kwamba ni mimi mwenyewe. Nipapaseni mkanione, maana mzimu hauna mwili na mifupa kama mnionavyo."
40Tai taręs, Jis parodė jiems rankas ir kojas.
40Baada ya kusema hayo, akawaonyesha mikono na miguu.
41Jiems iš džiaugsmo vis dar netikint ir stebintis, Jėzus paklausė: “Ar turite čia ko nors valgyti?”
41Wakiwa bado katika hali ya kutosadiki kwa sababu ya furaha yao, na wakiwa wanastaajabu, akawauliza, "Mnacho chakula chochote hapa?"
42Jie padavė Jam gabalą keptos žuvies ir korį medaus.
42Wakampa kipande cha samaki wa kuokwa.
43Jis paėmė ir valgė jų akyse.
43Akakichukua, akala, wote wakimwona.
44Paskui Jėzus jiems tarė: “Ar ne tokie buvo mano žodžiai, kuriuos jums kalbėjau dar būdamas su jumis: turi išsipildyti visa, kas parašyta apie mane Mozės Įstatyme, Pranašuose ir Psalmėse”.
44Halafu akawaambia, "Hii ndiyo maana ya maneno niliyowaambia nilipokuwa pamoja nanyi: kwamba ilikuwa lazima kukamilisha yote yaliyoandikwa juu yangu katika Sheria ya Mose na katika vitabu vya manabii na katika kitabu cha Zaburi."
45Tada Jis atvėrė jiems protą, kad jie suprastų Raštus,
45Kisha, akaziangazia akili zao ili wapate kuelewa Maandiko Matakatifu.
46ir pasakė: “Parašyta, kad Kristus kentės ir trečią dieną prisikels iš numirusių
46Akawaambia, "Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na siku ya tatu atafufuka kutoka wafu,
47ir, pradedant nuo Jeruzalės, Jo vardu visoms tautoms bus skelbiama atgaila ir nuodėmių atleidimas.
47na kwamba ni lazima, kwa jina lake, mataifa yote kuanzia na Yerusalemu yahubiriwe juu ya kutubu na kusamehewa dhambi.
48Jūs esate šių dalykų liudytojai.
48Ninyi ni mashahidi wa mambo hayo.
49Ir štai Aš atsiųsiu jums savo Tėvo pažadą. Jūs pasilikite Jeruzalės mieste, kol būsite apgaubti jėga iš aukštybių”.
49Nami mwenyewe nitawapelekeeni yule ambaye Baba aliahidi kumtuma, lakini ngojeni huku mjini mpaka mtakapopewa ile nguvu itokayo juu."
50Jėzus nusivedė juos iki Betanijos ir, iškėlęs rankas, palaimino juos.
50Kisha akawaongoza nje ya mji hadi Bethania, akainua mikono yake juu, akawabariki.
51Laimindamas Jis atsiskyrė nuo jų ir buvo paimtas į dangų.
51Alipokuwa anawabariki, akawaacha; akachukuliwa mbinguni.
52Jie pagarbino Jį ir, didelio džiaugsmo kupini, sugrįžo į Jeruzalę.
52Wao wakamwabudu, wakarudi Yerusalemu wakiwa na furaha kubwa:
53Jie nuolat buvo šventykloje ir šlovino bei laimino Dievą. Amen.
53wakakaa muda wote Hekaluni wakimsifu Mungu.