Norwegian

Swahili: New Testament

Jude

1

1Judas, Jesu Kristi tjener og Jakobs bror - til de kalte, som er elsket i Gud Fader og bevart for Jesus Kristus:
1Mimi Yuda, mtumishi wa Yesu Kristo, ndugu yake Yakobo, nawaandikia ninyi mlioitwa na Mungu na ambao mnaishi katika upendo wa Mungu Baba, na katika ulinzi wa Yesu Kristo.
2Miskunn og fred og kjærlighet bli eder mangfoldig til del!
2Nawatakieni huruma, amani na upendo kwa wingi.
3I elskede! mens jeg gjorde mig all flid for å skrive til eder om vår felles frelse, så jeg mig nødt til å skrive til eder med formaning om å stride for den tro som én gang er overgitt til de hellige.
3Ndugu wapenzi, wakati nimo katika jitihada ya kuwaandikieni juu ya ule wokovu tunaoshiriki sote, nimeona lazima ya kuwaandikieni na kuwahimizeni mwendelee kupigana kwa ajili ya imani ambayo Mungu amewajalia watu wake mara moja tu kwa wakati wote.
4For nogen mennesker har sneket sig inn, som denne dom allerede for lenge siden er opskrevet for: ugudelige, som forvender vår Guds nåde til skamløshet og nekter vår eneste hersker og herre, Jesus Kristus.
4Maana watu wasiomcha Mungu wamepata kujiingiza kwa siri miongoni mwetu, watu ambao, kwa faida ya maisha yao mabaya, wanaupotosha ujumbe wa neema ya Mungu wetu na kumkana Yesu Kristo aliye peke yake kiongozi na Bwana wetu. Maandiko Matakatifu yalikwisha bashiri tangu awali hukumu inayowangojea watu hao.
5Men da I nu engang vet alt, vil jeg minne eder om at Herren, efterat han hadde frelst folket ut av Egyptens land, siden ødela dem som ikke trodde,
5Nataka kuwakumbusheni mambo fulani ambayo mmekwisha yajua: kumbukeni jinsi Bwana alivyowaokoa watu wa Israeli na kuwatoa katika nchi ya Misri, lakini baadaye aliwaangamiza wale ambao hawakuamini.
6og om at de engler som ikke tok vare på sin høie stand, men forlot sin egen bolig, dem holder han i varetekt i evige lenker under mørket til dommen på den store dag;
6Na, malaika ambao hawakuridhika na cheo chao, wakayaacha makao yao ya asili, Mungu amewafunga gizani kwa minyororo ya milele wahukumiwe Siku ile kuu.
7likesom Sodoma og Gomorra og byene deromkring, som på samme måte som disse drev hor og gikk efter fremmed kjød, ligger for våre øine som et eksempel, idet de lider en evig ilds straff.
7Kumbukeni pia Sodoma na Gomora, na miji ya kandokando yake; wenyeji wake walifanya kama wale malaika; walifanya uzinzi na mambo yaliyo kinyume cha maumbile, wakapewa hukumu ya moto wa milele, iwe onyo kwa watu wote.
8Og dog gjør også disse like ens: idet de går i drømme, gjør de kjødet urent, ringeakter herredømme, spotter høie makter.
8Hivyo ndivyo pia walivyo watu hawa. ndoto zao huwaongoza katika kuichafua miili yao wenyewe, kuyadharau mamlaka ya Mungu na kuvitukana viumbe vitukufu vya huko juu.
9Overengelen Mikael vågde dog ikke å uttale en spottende dom dengang han trettet med djevelen om Mose legeme, men sa: Herren refse dig!
9Hata Mikaeli, malaika mkuu, hakufanya hivyo. Katika ule ubishi kati yake na Ibilisi waliobishana juu ya mwili wa Mose, Mikaeli hakuthubutu kumhukumu Ibilisi kwa matusi; ila alisema: "Bwana mwenyewe na akukaripie."
10Disse derimot spotter det de ikke kjenner; men det de av naturen skjønner, likesom de ufornuftige dyr, med det ødelegger de sig.
10Lakini watu hawa hutukana chochote wasichokielewa; mambo yaleyale wanayoyajua kwa silika kama vile wanyama wanayoyajua ndiyo yanayowaangamiza.
11Ve dem! for de har gått Kains vei og for vinnings skyld kastet sig inn i Bileams forvillelse og er gått under ved Korahs gjenstridighet.
11Ole wao! Watu hao wamefuata mwenendo uleule wa Kaini. Kwa ajili ya fedha, wamejiingiza katika mkosi uleule wa Baalamu. Wameasi kama Kora alivyoasi na wameangamizwa kama yeye alivyoangamizwa.
12Disse er skamflekkene ved eders kjærlighets-måltider, uten blygsel holder de gilde med eder og forer sig selv; vannløse skyer som drives avsted av vinden; trær, nakne som om høsten, ufruktbare, to ganger død, oprykket med rot;
12Kwa makelele yao yasiyo na adabu, watu hao ni kama madoa machafu katika mikutano yenu ya karamu ya Bwana. Hujipendelea wao wenyewe tu, na wako kama mawingu yanayopeperushwa huko na huko na upepo bila ya kuleta mvua. Wao ni kama miti isiyozaa matunda hata wakati wa majira yake, wamekufa kabisa.
13ville havsbårer som utskummer sin egen skam; villfarende stjerner, for hvem mørkets natt er rede til evig tid.
13Watu hao ni kama mawimbi makali ya bahari, na matendo yao ya aibu yanaonekana dhahiri kama vile mapovu ya mawimbi. Wao ni kama nyota zinazotangatanga, ambao Mungu amewawekea mahali pao milele katika giza kuu.
14Disse var det også Enok, den syvende fra Adam, spådde om da han sa: Se, Herren kommer med sine mange tusen hellige
14Henoki, ambaye ni babu wa saba tangu Adamu, alibashiri hivi juu ya watu hawa: "Sikilizeni! Bwana atakuja pamoja na maelfu ya malaika wake watakatifu
15for å holde dom over alle og refse alle de ugudelige for alle de ugudelige gjerninger som de gjorde, og for alle de hårde ord som de talte mot ham, de ugudelige syndere.
15kutoa hukumu juu ya binadamu wote, kuwahukumu wote kwa ajili ya matendo yao yote maovu waliyotenda na kwa ajili ya maneno yote mabaya ambayo watu waovu walimkashifu nayo."
16Disse er folk som knurrer og klager over sin skjebne, enda de farer frem efter sine lyster, og deres munn taler skrytende ord, enda de smigrer for folk for vinnings skyld.
16Watu hawa wananung'unika daima na kuwalaumu watu wengine. Hufuata tamaa zao mbaya, hujigamba na kuwasifu watu wengine mno kusudi wafaulu katika mipango yao.
17Men I, elskede, kom i hu de ord som forut er talt av vår Herre Jesu Kristi apostler,
17Lakini ninyi wapenzi wangu, kumbukeni yale mliyoambiwa hapo awali ni mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo.
18hvorledes de sa til eder at det i den siste tid skal komme spottere som farer frem efter sine ugudelige lyster!
18Waliwaambieni: "Siku za mwisho zitakapofika, watatokea watu watakaowadhihaki ninyi, watu wafuatao tamaa zao mbaya."
19Disse er de som skiller sig ut, naturlige mennesker, som ikke har ånd.
19Hao ndio watu wanaosababisha mafarakano, watu wanaotawaliwa na tamaa zao za kidunia, watu wasio na Roho wa Mungu.
20Men I, elskede, opbygg eder på eders høihellige tro, bed i den Hellige Ånd,
20Lakini ninyi, wapenzi wangu, endeleeni kujijenga kikamilifu katika imani yenu takatifu. Salini kwa nguvu ya Roho Mtakatifu,
21og hold eder således i Guds kjærlighet, mens I venter på vår Herre Jesu Kristi miskunn til evig liv!
21na kubaki katika upendo wa Mungu, mkiwa mnamngojea Bwana wetu Yesu Kristo awapeni uzima wa milele kwa huruma yake.
22Og nogen skal I tale til rette fordi de tviler,
22Muwe na huruma kwa watu walio na mashaka;
23andre skal I frelse ved å rive dem ut av ilden, andre igjen skal I miskunne eder over med frykt, idet I hater endog den av kjødet smittede kjortel.
23waokoeni kwa kuwanyakua kutoka motoni; na kwa wengine muwe na huruma pamoja na hofu, lakini chukieni hata mavazi yao ambayo yamechafuliwa na tamaa zao mbaya.
24Men ham som er mektig til å verne om eder, så I ikke snubler, og å stille eder lyteløse frem for sin herlighet i fryd,
24Kwake yeye awezaye kuwalinda msije mkaanguka, na kuwaleta ninyi bila hatia mpaka mbele ya utukufu wake,
25den eneste Gud, vår frelser ved Jesus Kristus, vår Herre, ham tilhører herlighet, storhet, styrke og makt før all tid og nu og i all evighet. Amen.
25kwake yeye aliye peke yake Mungu, Mkombozi wetu, uwe utukufu, ukuu, nguvu na mamlaka kwa njia ya Kristo Bwana wetu, tangu zama zote, sasa na hata milele! Amina.