Norwegian

Swahili: New Testament

Revelation

15

1Og jeg så et annet tegn i himmelen, stort og underfullt: syv engler som hadde de syv siste plager; for med dem er Guds vrede fullendt.
1Kisha nikaona ishara nyingine mbinguni, kubwa na ya kushangaza. Palikuwa hapo malaika saba wenye mabaa makubwa saba ya mwisho. Kwa mabaa hayo makubwa saba, ghadhabu ya Mungu imekamilishwa.
2Og jeg så likesom et glasshav blandet med ild; og dem som hadde seiret over dyret og dets billede og dets navns tall, så jeg stå ved glasshavet med Guds harper i hånd;
2Kisha nikaona kitu kama bahari ya kioo, imechanganywa na moto. Nikawaona pia wale watu waliomshinda yule mnyama na sanamu yake na ambaye jina lake lilitajwa kwa ile tarakimu. Watu hao walikuwa wamesimama kando ya hiyo bahari ya kioo, wakiwa na vinubi walivyopewa na Mungu.
3og de sang Moses', Guds tjeners sang og Lammets sang og sa: Store og underfulle er dine gjerninger, Herre Gud, du allmektige! rettferdige og sanne er dine veier, du folkenes konge!
3Walikuwa wakiimba wimbo wa Mose, mtumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwanakondoo: "Bwana Mungu Mwenye Uwezo, matendo yako ni makuu mno! Ewe Mfalme wa mataifa, njia zako ni za haki na za kweli!
4Hvem skulde ikke frykte, Herre, og ære ditt navn? Du alene er hellig, og alle folkene skal komme og tilbede for ditt åsyn, fordi dine rettferdige dommer er blitt åpenbaret.
4Bwana, ni nani asiyekucha wewe? Nani asiyelitukuza jina lako? Wewe peke yako ni Mtakatifu. Mataifa yote yatakujia na kukuabudu maana matendo yako ya haki yameonekana na wote."
5Og derefter så jeg, og templet med vidnesbyrdets telt i himmelen blev åpnet,
5Baada ya hayo nikaona Hekalu limefunguliwa mbinguni, na ndani yake hema ionyeshayo kuwapo kwa Mungu.
6og de syv engler som hadde de syv plager, kom ut av templet, klædd i rent og skinnende lin og ombundet om brystet med gullbelter.
6Basi, wale malaika saba wenye mabaa saba wakatoka humo Hekaluni, wakiwa wamevaa nguo za kitani safi zenye kung'aa, na kanda za dhahabu vifuani mwao.
7Og et av de fire livsvesener gav de syv engler syv gullskåler fylt med Guds vrede, hans som lever i all evighet.
7Kisha, mmojawapo wa vile viumbe vinne akawapa hao malaika saba mabakuli ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu, aishiye milele na milele.
8Og templet blev fylt med røk av Guds herlighet og av hans makt; og ingen kunde gå inn i templet før de syv englers syv plager var fullendt.
8Hekalu likajaa moshi uliosababishwa na utukufu na nguvu ya Mungu, na hakuna mtu aliyeweza kuingia Hekaluni mpaka mwisho wa mabaa makubwa saba ya wale malaika saba.