Paite

Swahili: New Testament

Luke

1

1Huai thilte i lak ua takpetpeta gina om, mi tampiin a thu gelh ana tup uh,
1Mheshimiwa Theofilo: Watu wengi wamejitahidi kuandika juu ya mambo yale yaliyotendeka kati yetu.
2A tunga pata a mute leh thu nasemten honhilh bang un,
2Waliandika kama tulivyoelezwa na wale walioyaona kwa macho yao tangu mwanzo, na waliotangaza ujumbe huo.
3Theophil aw, a bul apat bangkim chiantakin ka suia, kizom jelin nanga dingin kigelh leh a hoih ding, ka chi ahi;
3Inafaa nami pia, Mheshimiwa, baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote tangu mwanzo, nikuandikie kwa mpango,
4tumaa thu nang honhilh uh a dik ngelngel hi chih na theihna dingin.
4ili nawe uweze kujionea mwenyewe ukweli wa mambo yale uliyofundishwa.
5Judia gam kumpipa Herod a dam laiin, Abija pawla mi a min Zakaria khat a om a; huaiin Aron tanute laka khat jiin a neia, a min tuh Elizabet ahi.
5Wakati Herode alipokuwa mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani mmoja jina lake Zakaria, wa kikundi cha Abia. Mke wake alikuwa anaitwa Elisabeti, naye alikuwa wa ukoo wa kuhani Aroni.
6A nih un Pathian mitmuhin diktatin a om ua, gensiat beiin Toupa thupiak leh a dan tengteng juiin a omjel ua.
6Wote wawili walikuwa wanyofu mbele ya Mungu, wakiishi kwa kufuata amri na maagizo yote ya Bwana bila lawama.
7Himahleh Elizabet a chin jiakin ta a neikei ua, a nih un upa pitak ahi tuak ngal ua.
7Lakini hawakuwa wamejaliwa watoto kwa vile Elisabeti alikuwa tasa, nao wote wawili walikuwa wazee sana.
8Huan, hichibang ahi a, a pawlte hihdan bang jela Pathian maa siampua a gamtat laiin,
8Siku moja, ilipokuwa zamu yake ya kutoa huduma ya ukuhani mbele ya Mungu,
9siampu dan bangin Toupa biakina lut leh gimlim hal tuh a tan ahi a.
9Zakariya alichaguliwa kwa kura, kama ilivyokuwa desturi, kuingia hekaluni ili afukize ubani.
10Huan, gimlim hal hun laiin mipite a vek un inpua ah a na thum ua.
10Watu, umati mkubwa, walikuwa wamekusanyika nje wanasali wakati huo wa kufukiza ubani.
11Huan, Toupa angel khat gimlim halna maitam taklama dingin a kiangah a kilak a.
11Malaika wa Bwana akamtokea humo ndani, akasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia ubani.
12Huan, Zakariain a muh takin a lungjinga, lau leng a lau a.
12Zakariya alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.
13Himahleh angelin a kiangah, Zakaria, lau ken, na nget jaka a om jiakin, na ji Elizabet in tapa a honneihsak dia, a min Johan na sak ding ahi.
13Lakini malaika akamwambia, "Zakariya, usiogope, kwa maana sala yako imesikilizwa, na Elisabeti mkeo atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohane.
14Huan, nang na nuamin na kipak dinga; amah a suahin mi tampi a kipak ding uh.
14Utakuwa na furaha kubwa na watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
15Toupa ngaihin mi lian ahi dia, uain leh ju himhim a dawn kei ding; a nu sung apat himin Kha Siangthouin a hongdim ding.
15Atakuwa mkuu mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kileo, atajazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
16Israel suante tampi Toupa a Pathian lam uh a ngasak nawn ding a.
16Atawaelekeza wengi wa watu wa Israeli kwa Bwana Mungu wao.
17Huan, pate lungtang tate lam ngasak ding, mi chihmohte mi diktat pilna lam ngasak ding, Toupa dinga mi pite mansaa om sak dinga na bawl khol dingin Elija lungsim leh thilhihtheihna puin Toupa ma ah a pai ding. a chi hi.
17Atamtangulia Bwana akiongozwa na nguvu na roho kama Eliya. Atawapatanisha kina baba na watoto wao; atawafanya wasiotii wawe na fikira za uadilifu, na hivyo amtayarishie Bwana watu wake."
18Huan, Zakariain angel kiangah, Huai bangchin ka thei dia? kei putek hi inga, ka ji leng pitek ahi ngala, a chi a.
18Zakariya akamwambia huyo malaika, "Ni kitu gani kitakachonihakikishia jambo hilo? Mimi ni mzee, hali kadhalika na mke wangu."
19Huan, angelin a dawnga, a kiangah, Gabriel, Pathian maa ding jel ka hia; nang houpih ding leh, huai thu hoih honhilh dinga sawl ka hi.
19Malaika akamjibu, "Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele ya Mungu, na nimetumwa niseme nawe, nikuletee hii habari njema.
20Ngaiin, ka thugente a huntaka hongtung ding, na gintak louh jiakin huai thilte a hongtun masiah na dai dide dia, pau leng na pau theikei ding, a chi a.
20Sikiliza, utakuwa bubu kwa sababu huyasadiki haya maneno yatakayotimia kwa wakati wake. Hutaweza kusema mpaka hayo niliyokuambia yatakapotimia."
21Huan, vantang in Zakaria a nangak ua, Pathian biakin sunga a om sawt jiakin lamdang a sa mahmah ua.
21Wakati huo, wale watu walikuwa wanamngoja Zakariya huku wakishangaa juu ya kukawia kwake Hekaluni.
22Huan, a hongpawtin a kiang uah thu a gen theita kei a; huchiin, biakin ah kha kilak a mu ahi chih a theita ua; huan, a kiang uah chiamtehna te a bawl a, pau theilouin a om lailai hi.
22Alipotoka nje, hakuweza kusema nao. Ikawa dhahiri kwao kwamba alikuwa ameona maono Hekaluni. Lakini akawa anawapa ishara kwa mikono, akabaki bubu.
23Huan, hichi ahi a, a nasepna ni a kim takin a in ah a paita a.
23Zamu yake ya kuhudumu ilipokwisha, alirudi nyumbani.
24Huan, tua nite nungin, a ji Elizabet tuh a honggaita a, kha nga a buta a,
24Baadaye Elisabeti mkewe akapata mimba. Akajificha nyumbani kwa muda wa miezi mitano, akisema:
25Mi laka ka min se khuhna dingin, Toupan a honmuhin, hichibangin ka tungah a hihta, chiin.
25"Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana; ameniangalia na kuniondolea aibu niliyokuwa nayo mbele ya watu."
26Huan, a kha gukna ah Pathianin angel Gabriel, Galili gama khua khat Nazaret a chih uah,
26Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya,
27nungak siangthou khat kiangah a sawla, huai nungak tuh David suan mikhat a min Joseph toh ki kham ahi ua; nungak min tuh Mari ahi.
27kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi.
28Huan, angel tuh a kiangah a luta, Chibai, nang nakpitaka deihtuam: Toupa na kiangah a om, a chi a.
28Malaika akamwendea, akamwambia, "Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe."
29Huan, huai thu jiakin a lunghimoh mahmaha, Bangchidana chibai honbuk a diam aw? chiin, a kingaihtuaha.
29Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini?
30Huan, angelin a kiangah, Mari, lau ken; Pathian lakah deihsakna na tang hi.
30Malaika akamwambia, "Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.
31Ngai in, na gai dia, tapa na nei dia, a min din Jesu na sa ding ahi.
31Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu.
32Amah mi lian a honghi dinga, Tungnungpen Tapa a chi ding uh; Toupa Pathianin a kiangah a pu David tutphah a pe dia.
32Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake.
33Jakob suante tungah khantawnin a lal dia, a gam in bei ni a neikei ding hi, a chi a.
33Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho."
34Huan, Mariin angel kiangah, Hiai bangchin ahi dia? pasal lah neilou inga, a chi a.
34Maria akamjibu, "Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?"
35Huan, angelin a dawnga, a kiang ah, Kha Siangthou na tungah a hongtung dinga, Tungnungpen thilhihtheihnain a honliah khum ding, huai jiakin misiangthou hongpiang ding leng, siangthou Pathian Tapa, chihin a om ding, a chi a.
35Malaika akamjibu, "Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu.
36Huan, ngaiin, na sanggamnu Elizabetin leng a tek nungin tapa a paita; a ching a chihchih uh, tu kha a kha gukna a hita.
36Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa.
37Pathian thu pawt himhim thil hih theilouin a om kei ding, a chi a.
37Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu."
38Huan, Mariin, Ngai in, Toupa sikhanu ka hi, na thu bang jelin ka tungah tung hen, a chi a. Huan, angelin a paisanta.
38Maria akasema, "Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema." Kisha yule malaika akaenda zake.
39Huai laiin Mari a thou a, singtangah, Judia gama khua khat ah a hoh paha;
39Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yuda.
40Huan, Zakaria in ah a luta, Elizabet chibai a buk a.
40Huko, aliingia katika nyumba ya Zakariya, akamsalimu Elisabeti.
41Huan, hichi ahia, Elizabetin Mari chibai buk a jak takin, a sung a naungek a tanga; huan, Elizabet tuh Kha Siangthouin a hongdimta; huan, aw ngaihtakin a kikou a,
41Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifiu,
42Nang numei sapsap din na hampha hi, na gil gah leng a hampha hi.
42akasema kwa sauti kubwa, "Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa.
43Ka Toupa nu ka kianga na hong bangchidan ahia oi?
43Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
44Ngai in, non chibai buk husa ka bila a lut takin, a kipah jiakin naungek ka sungah a tang ahi.
44Nakwambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
45A gingnu a hampha hi, a kianga Toupan thu a gen tuh tung ding a hih jiakin, a chi a.
45Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokwambia."
46Huan, Mariin, Ka nuntaknain Toupa a pahtawi e,
46Naye Maria akasema,
47Ka kha leng ka Hondampa Pathian tungah a kipak mahmaha.
47"Moyo wangu wamtukuza Bwana, roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.
48A sikhanu nam tom dan a mu a, a hehpiha; ngai in, tu nung siah khangthak tengtengin hampha honchi ding uh.
48Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu. Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.
49Amah Mi hatin ka tungah thil thupi tak honhih saka, a min leng a siangthou hi.
49Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu, jina lake ni takatifu.
50A laudansiamte tuh khangthak tanin a hehpih jeljel.
50Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi.
51A banin a tha hatdan a ensaka, mi kisatheite tuh a lungtang gelna a hihdalhta.
51Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
52A laltutphah ua lal tute a kai khia a, nam tomte tuh a pahtawita a.
52amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.
53Gilkial te thil hoihin a hihvah a, mihaute khut vuakin a pai mang sakta hi.
53Wenye njaa amewashibisha mema, matajiri amewaacha waende mikono mitupu.
54A sikha Israel taksap awng tuh a huta, a zahngaihna theihgigena dingin.
54Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.
55I pipute kianga a gen bangin khantawin Abraham leh a suante lamah.
55Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele."
56Huan, Mari kha thum khawng a kiang ah a oma, huan, a in lamah a pai nawnta.
56Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.
57Huan, Elizabet nau suah a honghunta a; huchiin tapa a honneita a.
57Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.
58Huan, a vengte leh a sanggamten Toupan a hehpih mahmah chih a na ja ua, a kipahpih uh.
58Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.
59Huan, hichi ahia, a ni giat nin naungek zeksum dingin a hong ua; a min din a pa min mah Zakaria sak a tum ua.
59Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakariya.
60Huan, a nun, Hi lou e, amah jaw Johan sak jawk ding ahi, a chi a, a dawng a.
60Lakini mama yake akasema, "La, sivyo, bali ataitwa Yohane."
61Huan, a nu kiangah, Na sanggamte lakah hiai min pu kuamah a om sam ua, a chi ua.
61Wakamwambia, "Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?"
62Huan, a pa kiangah chiamtehnate bawlin, A min din bang sa lehang na deih a? a chi ua.
62Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.
63Huan, lai gelhnapek a ngena, A min Johan ahi, chiin a gelh a.
63Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: "Yohane ndilo jina lake." Wote wakastaajabu.
64Huan, a vek un lamdang a sa mahmah uh. Huan, thakhatin a kam hongkihongin a lei a hongkiphel a, Pathian phatin a hongpau kheta a.
64Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
65Huan, a kim ua omte tengtengin a lau ta ua; Huchiin, huai thute tuh Judia gam singtang tengtengah a thang ta a.
65Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.
66Huan, a za peuhmahin, a lungtang un a vei chiat ua, Huai naungek bangchi phet a honghi de aw? chiin. Huan, Toupa khutin amah a panpih ngala.
66Wote waliosikia mambo hayo waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: "Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?" Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.
67Huan, a pa Zakaria tuh, Kha Siangthouin a hongdima, a genkhol a,
67Zakariya, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka ujumbe wa Mungu:
68Toupa, Israel Pathian, phatin om hen, a mite a honveha, tatna a siamsak a.
68"Asifiwe Bwana Mungu wa Israeli, kwani amekuja kuwasaidia na kuwakomboa watu wake.
69A sikha David inkuanpihte lakah hotdamna ki a honbawlsaktak jiakin;
69Ametupatia Mwokozi shujaa, mzawa wa Daudi mtumishi wake.
70Tang laia kipan a jawlnei siangthoute kama, a gen bangin.
70Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu,
71I doute lakah leh honhote tengteng laka hotdam-a i om ding thu,
71kwamba atatuokoa mikononi mwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72I pipute kianga achiam zahngaihna tangtungsak dingin leh a thukhun siangthou theigige dingin.
72Alisema atawahurumia wazee wetu, na kukumbuka agano lake takatifu.
73I pu Abraham kianga a kichiam a.
73Kiapo alichomwapia Abrahamu baba yetu, ni kwamba atatujalia sisi
74I doute laka a honbit saka, lau loua a na i sepna ding.
74tukombolewe kutoka adui zetu, tupate kumtumikia bila hofu,
75I dam sung teng a mit muha siangthou leh diktat taka omna dingin.
75kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu.
76A hi, Bawi, nang jaw Tungnungpen jawlnei a honchi ding ua; a lampi khawng bawl dingin Toupa maah na pai ding ahi ngala.
76Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu, utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;
77A khelhnate uh ngaihdamna dia a mite kianga hotdamna theihna pe ding in.
77kuwatangazia watu kwamba wataokolewa kwa kuondolewa dhambi zao.
78I Pathian lungtanga hehpihna jiakin, huchia tunglam akipan i tunga ni a tan chianga.
78Mungu wetu ni mpole na mwenye huruma. Atasababisha pambazuko angavu la ukombozi litujie kutoka juu,
79Mial laka leh sihna lima tute tanvak ding leh khamuanna lampia i khete kalsuan sak dingin, a chi a.Huan, naungek tuh a hongkhang lian deuhdeuha, a kha lam a honghat hiaihiai a, Israelte kianga a hongkilak masiah gamdai ah a om gige.
79na kuwaangazia wote wanaokaa katika giza kuu la kifo, aongoze hatua zetu katika njia ya amani."
80Huan, naungek tuh a hongkhang lian deuhdeuha, a kha lam a honghat hiaihiai a, Israelte kianga a hongkilak masiah gamdai ah a om gige.
80Mtoto akakua, akapata nguvu rohoni. Alikaa jangwani mpaka alipojionyesha rasmi kwa watu wa Israeli.