1Huan, Jesun sawm leh nihte a sam khawma, dawi tengteng tunga thilhihtheihna leh thuneihna leh natnate hihdam theihna a pia a.
1Yesu aliwaita wale kumi na wawili, akawapa uwezo juu ya pepo wote, na uwezo wa kuponya wagonjwa.
2Huchiin, Pathian gam thugen ding leh dam loute hihdam dingin a sawlkhetaa.
2Halafu akawatuma waende kuhubiri Ufalme wa Mungu na kuponya wagonjwa.
3Huan, a kiang uah, Zinna adingin chiang khun hiam, kawljal hiam, tanghou hiam, dangka hiam, bangmah keng kei un; puannak nih leng neikei un.
3Akawaambia, "Mnaposafiri msichukue chochote: msichukue fimbo, wala mkoba, wala chakula, wala fedha, wala hata koti la ziada.
4Huan, na tunna in peuh uah tung kinken jel un, huai in akipanin paikhia un.
4Nyumba yoyote mtakayoingia na kukaribishwa, kaeni humo mpaka mtakapoondoka katika kijiji hicho.
5Huan, a honkipahpih lou peuhmah tuh huai khua akipan na paikhiak chiang un amau mohpaihna dingin na khepek ua leivui tatkhia unla, a chi a.
5Watu wakikataa kuwakaribisha, tokeni katika mji huo, nanyi mnapotoka kung'uteni mavumbi miguuni mwenu kama onyo kwao."
6Huchiin, a kuanta ua, khua a tawn vialvial ua. Gam chihah Tanchiin Hoih a hilh ua, mi a hihdam jel uh.
6Basi, wakaanza safari, wakapitia vijijini wakihubiri Habari Njema na kuponya wagonjwa kila mahali.
7Huan, kumpipa Herodin a thilhih tengteng uh a nazataa; khenkhatin Johan hing nawnta ei ve a chi ua, khenkhatin,
7Sasa, mtawala Herode, alipata habari za mambo yote yaliyokuwa yanatendeka, akawa na wasiwasi kwa vile walikuwa wakisema: "Yohane amefufuka kutoka wafu!"
8Elija hongkilakta ei ve a chi ua, khenkhatin, Nidang laia jawlnei kuahiam thou nawnta ei ve, a chih jiak un, a lungjingtaa.
8Wengine walisema kwamba Eliya ametokea, na wengine walisema kwamba mmojawapo wa manabii wa kale amerudi duniani.
9Huan, Herodin, Johan a lu ka tanta a; himahleh hichi lawmlawma a thu ka jakjak kua ahia? a chi a. Huan, amah tuh muh a tumta hi.
9Lakini Herode akasema, "Huyo Yohane nilimkata kichwa; sasa ni nani huyu ninayesikia habari zake?" Akawa na hamu ya kumwona.
10Huan, sawltakte a hongkik nawn un, a kiangah a thilhihte uh a hilh ua. Huan, aman amau piin khopi Bethsaida kichi ah a pai tuamta a.
10Wale mitume waliporudi, walimweleza yote waliyoyafanya. Yesu akawachukua, wakaenda peke yao mjini Bethsaida.
11Himahleh mipin a thei ua, a jui jel uh; huan, aman amau a nakipahpiha, Pathian gam thu a hilha, hihdam kiphamoh peuhmah a hihdama.
11Lakini wale watu walipojua alikokwenda, walimfuata. Yesu akawakaribisha akawazungumzia juu ya Ufalme wa Mungu, akawaponya wale waliohitaji kuponywa.
12Huan, nitaklam a honghi dektaa; huan, sawm leh nihte a hongpai ua, a kiangah, khuate leh a kim gam khawnga giahna leh annektuidawn zong dingin mipite paisak tanla; tua, gamkeu muna om hi ngal hang a, a chi ua.
12Jua lilipokuwa linaanza kutua, wale kumi na wawili walimwendea wakamwambia, "Waage watu waende kwenye vijiji na mashamba ya karibu, wakajipatie chakula na mahali pa kulala, kwa maana hapa tulipo ni nyikani."
13Aman bel a kiang uah, Nou nek ding pia un, a chi a. Huan, amau, Mi hiai zahzah adia nek ding I valei sak keileh, tanghou phel nga leh nga nih kia loungal bangmah I neikei uh, a chi ua.
13Lakini Yesu akawaambia, "Wapeni ninyi chakula." Wakamjibu, "Hatuna chochote ila mikate mitano na samaki wawili. Labda twende wenyewe tukawanunulie chakula watu wote hawa!"
14Piching ngen leng sang nga hiam phial ahi ngal ua. Huan, a nungjuite kiangah, A pawlpawlin tu sak un, sawm nga khawng jelin, a chi a.
14(Walikuwepo pale wanaume wapatao elfu tano.) Basi, Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Waambieni watu waketi katika makundi ya watu hamsinihamsini."
15Huchiin a hih ua, a tu sak vekta ua.
15Wanafunzi wakafanya walivyoambiwa, wakawaketisha wote.
16Huan, tanghou phel nga leh ngasa nih tuh a laa, van lam enin vual a jawla a balkhama, mipi maa lui dingin a nungjuite kiang ah a piaa.
16Kisha Yesu akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akamshukuru Mungu, akavimega, akawapa wanafunzi wake wawagawie watu.
17Huan, a ne ua, a vah vekta ua, huan, a khamval nengte uh bawm sawm leh nih a luak dim uh.
17Wakala wote, wakashiba; wakakusanya makombo ya chakula, wakajaza vikapu kumi na viwili.
18Huan, hi chi ahi a, Jesu amah kiaa a thum lain a nungjuite a kiangah a om ua; a kiang uah, Mipiten kua ka hi a honchi ua? chiin a donga.
18Siku moja, Yesu alikuwa anasali peke yake, na wanafunzi wake walikuwa karibu. Basi, akawauliza, "Eti watu wanasema mimi ni nani?"
19Huan, amau, Baptispa Johan ahi, honchi uh; himahleh khenkhatin, Nidang laia jawlnei kuahiam a thou nawnta ahi, a honchi uh, chiin, a dawng ua.
19Nao wakamjibu, "Wengine wanasema kuwa wewe ni Yohane mbatizaji, wengine wanasema wewe ni Eliya, hali wengine wanasema kuwa wewe ni mmoja wa manabii wa kale ambaye amefufuka."
20Huan, aman a kiang uah, Ahihleh, nou kua ka hi non chi ua? a chi a. Peterin, Pathian kris mah, chiin, a dawnga.
20Hapo akawauliza, "Na ninyi je, mwasema mimi ni nani?" Petro akajibu, "Wewe ndiwe Kristo wa Mungu."
21Huan, huai thu kuamah hilh louh ding chi bikbekin, thu a piaa:
21Halafu Yesu akawaamuru wasimwambie mtu yeyote habari hiyo.
22Mihing Tapain thil tampi a thuak dia, upate, siampu liante, laigelhmite deih louhin a om dia, thahin a om dia, ni thum niin kaihthohin a om ding ahi, a chi a.
22Akaendelea kusema: "Ni lazima Mwana wa Mtu apate mateso mengi na kukataliwa na wazee na makuhani wakuu na walimu wa Sheria; atauawa, lakini siku ya tatu atafufuliwa."
23Huan, amahmahin, mi tengteng kiangah, kuapeuhin honzuih a ut leh, amah kingaihsak louin, niteng a kros puin honjui hen.
23Kisha akawaambia watu wote, "Mtu yeyote akitaka kuwa mfuasi wangu, ni lazima ajikane nafsi yake, auchukue msalaba wake kila siku, anifuate.
24Kuapeuh a hin humbit utin a tan ding; kuapeuh keimah jiaka a hin tanin, huai mi mahin a humbit ding.
24Maana, mtu anayetaka kuyaokoa maisha yake mwenyewe, atayapoteza; lakini atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu, atayaokoa.
25Min khovel a pumin nei henla, amah kimangsak hiam, ahihkeileh kimanloh leh, amah adingin bang a phatuam dia?
25Je, kuna faida gani mtu kuupata utajiri wote wa dunia kwa kujipoteza au kujiangamiza yeye mwenyewe?
26Kuapeuh keimah leh ka thu zahpih mi jaw Mihing Tapain, amah thupina toh, a Pa thupina toh, a angel siangthoute thupina toh a hongpai chiangin a honzahpih ding.
26Mtu akinionea aibu mimi na mafundisho yangu, Mwana wa Mtu atamwonea aibu mtu huyo wakati atakapokuja katika utukufu wake na wa Baba na wa malaika watakatifu.
27Diktakin ka honhilh ahi, Hiaia dingte akhen, Pathian gam a muh masiah uh sihna chiam lou hial ding a om uh, a chi a.
27Nawaambieni kweli, kuna wengine papa hapa ambao hawatakufa kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu."
28Huan, hichi ahi a, huai thugen nung ni giat hiam khawngin, Jesun Peter, Johan leh Jakob a pi a, thum dingin tangah a hohtou a.
28Yapata siku nane baada ya kusema hayo, Yesu aliwachukua Petro, Yohane na Yakobo, akaenda nao mlimani kusali.
29Huan, a thum laiin a mel omdan a honglamdanga, a puansilhte mi leng theiin a hongngoutaa.
29Alipokuwa akisali, sura yake ilibadilika, mavazi yake yakawa meupe na kung'aa sana.
30Huan, ngai in, mi nih amah toh a kihou ua, huai mite tuh Mosi leh Elija ahi uh.
30Na watu wawili wakaonekana wakizungumza naye, nao ni Mose na Eliya,
31Thupinaa kithuamin a kilak ua, Jerusalem khuaa sihna a hihkim ding thu a gen uh.
31ambao walitokea wakiwa wenye utukufu, wakazungumza naye juu ya kifo chake ambacho angekikamilisha huko Yerusalemu.
32Peter leh a lawmte bel a ihmut uh a suaka, himahleh a hak teitei ua a thupina leh a kianga mi nih ding a mu uh.
32Petro na wenzake walikuwa wamelemewa na usingizi mzito, hata hivyo waliamka, wakauona utukufu wake, wakawaona na wale watu wawili waliokuwa wamesimama pamoja naye.
33Huan, huai miten Jesu a paisan dek lai un, Peterin, Jesu kiangah, Heutupa, ei din hiaia om hoih veh, aidakbuk thum i khoh dia, nang din khat, Mosi din khat, Elija din khat, a chi a-a thugen lengthei louin.
33Basi, watu hao wawili walipokuwa wakiondoka, Petro alimwambia Yesu, "Bwana, ni vizuri kwamba tupo hapa: basi, tujenge vibanda vitatu: kimoja chako, kimoja cha Mose na kimoja cha Eliya." --Kwa kweli hakujua anasema nini.
34Huan huai thute a gen laiin mei a hongkaia, amau tuh a liahta; mei laka a lut laiun a lau ua.
34Petro alipokuwa akisema hayo, mara wingu likatokea na kuwafunika; na wingu hilo lilipowajia, wale wanafunzi waliogopa sana.
35Huan mei akipan aw a hongsuaka, Hiai ka Tapa, ka tel ahi, amah thu ngai un, a chi a.
35Sauti ikasikika kutoka katika hilo wingu: "Huyu ndiye Mwanangu niliyemchagua, msikilizeni."
36Huan aw a daih takin Jesu amah kiain a muta uh. Huan, a dai dide ua, huailai khawngin a thil muh uh kuamah bangmah a hilh kei uh.
36Baada ya hiyo sauti kusikika, Yesu alionekana akiwa peke yake. Wanafunzi walikaa kimya juu ya tukio hilo, na wakati ule hawakumwambia mtu yeyote mambo hayo waliyoyaona.
37Huan, hichi ahi a, a jingin tang akipana a paisuk nung un, mipi thupi takin amah a nadawn ua.
37Kesho yake walipokuwa wakishuka kutoka kule mlimani, kundi kubwa la watu lilikutana na Yesu.
38Huan, ngaiin, mipi lakah mi khat a kikoua, Sinsakpa, ka tapa en dingin ka honngen ahi, ka tapa neihsun ahi ngala.
38Hapo, mtu mmoja katika lile kundi akapaaza sauti, akasema, "Mwalimu! Ninakusihi umwangalie mwanangu--mwanangu wa pekee!
39Ngai in, dawiin a mana, a kikou khe guih jela; huchiin, a chilphuan bang ke hialin a gimbawla, nakpitaka hihsidupin a pai san phet jela.
39Pepo huwa anamshambulia, na mara humfanya apige kelele; humtia kifafa, na povu likamtoka kinywani. Huendelea kumtesa sana, asimwache upesi.
40Huan na nungjuite kiangah delhkhe dingin ka ngena, a hih theikei uh, a chi a.
40Niliwaomba wanafunzi wako wamfukuze, lakini hawakuweza."
41Huan, Jesun, Khangthak ginna neilou leh lampialte aw, bangtan ahia ka honthuak theih ding? Na tapa tuh hiaiah honpi in, a chi a, a dawng a.
41Yesu akasema, "Enyi kizazi kisicho na imani, kilichopotoka! Nitakaa nanyi na kuwavumilia mpaka lini?" Kisha akamwambia huyo mtu, "Mlete mtoto wako hapa."
42Huan, a honglaiin dawiin a hihpuk eka, nakpitakin a gimbawltaa, himahleh, Jesun dawi nin tuh a taia, naupang tuh a hihdama, a pa kiangah a paisak nawnta.
42Wakati mtoto huyo alipokuwa anamjia Yesu, yule pepo alimwangusha chini na kumtia kifafa. Lakini Yesu akamkemea yule pepo mchafu akamponya mtoto na kumkabidhi kwa baba yake.
43Huan, mi tengtengin Pathian thupidan lamdang a sa mahmah uh. Huchiin mi tengtengin a thilhih tengteng lamdang a sak lai un, Jesun a nungjuite kiangah,
43Watu wote wakashangazwa na uwezo mkuu wa Mungu. Wale watu walipokuwa bado wanashangaa juu ya mambo yote aliyofanya, Yesu aliwaambia wanafunzi wake,
44Hiai thute na bil uah lut heh. Mihing Tapa mihingte khuta mat saka om ding ahi ngala, a chi a
44"Tegeni masikio, myasikie mambo haya: Mwana wa Mtu anakwenda kutiwa mikononi mwa watu."
45Himahleh, a thugen tuh a theisiam kei uh, a theihtheih louhna ding un a kisel ahi, huai thugen tanchin tuh amah a dong ngam ngal kei ua.
45Lakini wao hawakuelewa maana ya usemi huo. Jambo hilo lilikuwa limefichwa kwao ili wasitambue; nao wakaogopa kumwuliza juu ya msemo huo.
46Huan, a lak uah kua a thupipen dia? Chih thuin a nakisel ua.
46Kukatokea majadiliano kati ya wale wanafunzi kuhusu nani kati yao aliyekuwa mkuu zaidi.
47Huchiin, Jesun a lungtang ua a ngaihtuah uh a theia, naupang neu khat a kaia, a sik ah a omsaka, a kiang uah,
47Yesu aliyajua mawazo yaliyokuwa mioyoni mwao; basi akamchukua mtoto mdogo akamweka karibu naye,
48Kuapeuh ka min jiaka hiai naupang neu kipahpih tuh keimah honkipahpih ahi ding uh; na vek ua laka neupen ahi, a thupipen, a chi a.
48akawaambia, "Mtu yeyote anayempokea mtoto huyu mdogo kwa jina langu, ananipokea mimi; na yeyote anayenipokea mimi, anampokea yule aliyenituma. Maana yule aliye mdogo kuliko wote kati yenu ndiye aliye mkubwa kuliko wote."
49Huan, Johanin, Heutupa, kuahiam na mina dawite delkhia ka mu ua, kon zuihna ua a pan sam louh jiakin ka khamta ve ua, a chi a, dawnga.
49Yohane alidakia na kusema, "Bwana, tumemwona mtu mmoja akitoa pepo kwa kulitumia jina lako nasi tukajaribu kumkataza kwa kuwa yeye si mmoja wetu."
50Jesun bel a kiang ah, Kham nawn kei un, kuapeuh nou hondal loutuh nou lama pang ahi uh, a chi a.
50Lakini Yesu akamwambia, "Msimkataze; kwani asiyepingana nanyi yuko upande wenu."
51Huan, hichi ahi a, amah pi touh a hun dingin, Jerusalem khuaa hoh a tum chiltela, a maah mi a matai saka;
51Wakati ulipokaribia ambapo Yesu angechukuliwa juu mbinguni, yeye alikata shauri kwenda Yerusalemu.
52Huan, a pai ua, amah adia nakimansak dingin Samari mite kho khatah a lut ua.
52Basi, akawatuma wajumbe wamtangulie, nao wakaenda wakaingia kijiji kimoja cha Wasamaria ili wamtayarishie mahali.
53Huan, a mai tuh Jerusalem kho lam naiha a lat jiakin amah a nakipahpih kei uh.
53Lakini wenyeji wa hapo hawakutaka kumpokea kwa sababu alikuwa anaelekea Yerusalemu.
54Huchiin a nungjui Jakob leh Johanin huai a theih takun, Toupa, amaute kangmang dingin van akipan mei sam khe leng hoih na sa hia? a chi ua.
54Basi, wanafunzi wake, kina Yohane na Yakobo, walipoona hayo, wakasema, "Bwana, wataka tuamuru moto ushuke kutoka mbinguni uwateketeze?"
55Amah tuh a kiheia, amau a taitaa.
55Lakini yeye akawageukia, akawakemea akasema, "Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo;
56Huan, kho dangah a paita uh.
56kwa maana Mwana wa Mtu hakuja kuyaangamiza maisha ya watu, bali kuyaokoa." Wakatoka, wakaenda kijiji kingine.
57Huan, lampia a pai lai un, kuahiamin a kiangah, Na paina peuhah kon jui ding, a chi a.
57Walipokuwa wakisafiri njiani, mtu mmoja akamwambia Yesu, "Nitakufuata kokote utakakokwenda."
58Huan, Jesun a kiangah, Sehalten kua a nei ua, tungleng vasaten leng bu a nei uh, ahihhangin Mihing Tapain jaw a lu ngakna ding mun a neikei, a chi a.
58Yesu akasema, "Mbweha wana mapango, na ndege wana viota; lakini Mwana wa Mtu hana mahali pa kupumzikia."
59Huan, Jesun mi dang kiangah, Honjui in, a chi a. Himahleh aman, Toupa, ka pa honvui sak phot in, a chi a.
59Kisha akamwambia mtu mwingine, "Nifuate." Lakini huyo akasema, "Bwana, niruhusu kwanza niende kumzika baba yangu."
60Jesun tuh a kiangah, Misiin a misi uh vui uheh; nang Pathian gam thu vahilh jak jaw in, a chi a.
60Yesu akamwambia, "Waache wafu wazike wafu wao; bali wewe nenda ukatangaze Ufalme wa Mungu."
61Huan, mi dangin leng, Toupa, kon jui ding, a hihhangin ka ina mite kamphain honkha sak photin, a chi a.Huan, Jesun a kiangah, Kuapeuh leilehna lena, nunglam nga tuh, Pathian gam mi hitak ahi kei, a chi.
61Na mtu mwingine akamwambia, "Nitakufuata, lakini niruhusu kwanza nikawaage wale walio nyumbani kwangu."
62Huan, Jesun a kiangah, Kuapeuh leilehna lena, nunglam nga tuh, Pathian gam mi hitak ahi kei, a chi.
62Yesu akamwambia, "Yeyote anayeshika jembe tayari kulima na huku anaangalia nyuma, hafai kwa Ufalme wa Mungu."