1A to wiedz, iż w ostateczne dni nastaną czasy trudne.
1Kumbuka kwamba, katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za taabu.
2Albowiem będą ludzie sami siebie miłujący, łakomi, chlubni, pyszni, bluźniercy, rodzicom nieposłuszni, niewdzięczni, niepobożni,
2watu watakuwa na ubinafsi, wenye tamaa ya fedha, wenye majivuno, wenye kujiona, wenye kumtukana Mungu, wasiowatii wazazi wao, wasio na shukrani na waovu;
3Bez przyrodzonej miłości, przymierza nie trzymający, potwarcy, niepowściągliwi, nieskromni, dobrych nie miłujący,
3watatokea watu wasio na upendo moyoni, wasio na huruma, wachongezi, walafi na wakali; watachukia chochote kilicho chema;
4Zdrajcy, skwapliwi, nadęci, rozkoszy raczej miłujący niż miłujący Boga;
4watakuwa wahaini, wakaidi na waliojaa kiburi; watapenda anasa kuliko kumpenda Mungu.
5Którzy mają kształt pobożności, ale się skutku jej zaparli; i tych się chroó.
5Kwa nje wataonekana kama watu wenye kumcha Mungu, lakini wataikana nguvu yake. Jiepushe kabisa na watu wa namna hiyo.
6Albowiem z tych są ci, którzy się wrywają w domy i pojmane wiodą niewiastki grzechami obciążone, które uwodzą rozmaite pożądliwości;
6Baadhi yao huenda katika nyumba za watu na huwateka wanawake dhaifu waliolemewa mizigo ya dhambi na ambao wanaongozwa na tamaa za kila aina;
7Które się zawsze uczą, a nigdy do znajomości prawdy przyjść nie mogą.
7wanawake ambao wanajaribu daima kujifunza lakini hawawezi kuufikia ujuzi wa huo ukweli.
8A jako Jannes i Jambres sprzeciwiali się Mojżeszowi, tak i ci sprzeciwiają się prawdzie, ludzie rozumu skażonego, odrzuceni z strony wiary.
8Watu hao huupinga ukweli kama vile Yane na Yambre walivyompinga Mose.
9Ale nie postąpią dalej; albowiem głupstwo ich jawne będzie wszystkim, jako i onych było.
9Lakini hawataweza kuendelea zaidi kwa maana upumbavu wao utaonekana wazi kwa wote. Ndivyo ilivyokuwa kwa akina Yane na Yambre.
10Aleś ty doszedł nauki mojej, sposobu żywota mego, przedsięwzięcia wiary, nieskwapliwości, miłości i cierpliwości,
10Wewe lakini, umeyafuata mafundisho yangu, mwenendo wangu, makusudi yangu katika maisha, imani yangu, uvumilivu wangu, upendo wangu, subira yangu,
11Prześladowania, ucierpienia, które mię spotkały w Antyjochii, w Ikonii i w Listrze, jakiem prześladowania podejmował; a ze wszystkich wyrwał mię Pan.
11udhalimu na mateso yangu. Unayajua mambo yaliyonipata huko Antiokia, Ikonio na Lustra. Nilivumilia udhalimu mkubwa mno! Lakini Bwana aliniokoa katika mambo hayo yote.
12Aleć i wszyscy, którzy chcą pobożnie żyć w Chrystusie Jezusie, prześladowani będą.
12Kila mtu anayetaka kuishi maisha ya kumcha Mungu katika kuungana na Kristo Yesu lazima adhulumiwe.
13Lecz źli ludzie i zwodziciele postąpią w gorsze, jako zwodzący tak i zwiedzeni.
13Watu waovu na wadanyanyifu watazidi kuwa waovu zaidi na zaidi kwa kuwadanganya wengine na kudanganyika wao wenyewe.
14Ale ty trwaj w tem, czegoś się nauczył i czegoć powierzono, wiedząc, od kogoś się tego nauczył.
14Lakini wewe dumu katika ukweli ule uliofundishwa, ukaukubali kabisa. Unawajua wale waliokuwa walimu wako.
15A iż z dziecióstwa umiesz Pisma święte, które cię mogą uczynić mądrym ku zbawieniu przez wiarę, która jest w Chrystusie Jezusie.
15Unakumbuka kwamba tangu utoto wako umeyajua Maandiko Matakatifu ambayo yaweza kukupatia hekima iletayo wokovu kwa njia ya imani kwa Kristo Yesu.
16Wszystko Pismo od Boga jest natchnione i pożyteczne ku nauce, ku strofowaniu, ku naprawie, ku ćwiczeniu, które jest w sprawiedliwości;
16Maandiko yote Matakatifu yameandikwa kwa uongozi wa Mungu, na yanafaa katika kufundishia ukweli, kuonya, kusahihisha makosa, na kuwaongoza watu waishi maisha adili,
17Aby człowiek Boży był doskonały, ku wszelkiej sprawie dobrej dostatecznie wyćwiczony.
17ili mtu anayemtumikia Mungu awe mkamilifu, na tayari kabisa kufanya kila tendo jema.