Polish

Swahili: New Testament

Acts

1

1Pierwsze wprawdzie księgi napisałem, o Teofilu! o wszystkiem, co począł Jezus i czynić, i uczyć.
1Ndugu Theofilo, Katika kitabu cha kwanza niliandika juu ya mambo yote Yesu aliyotenda na kufundisha tangu mwanzo wa kazi yake
2Aż do dnia onego, którego dawszy rozkazanie Apostołom, które był przez Ducha Świętego obrał, wzięty jest w górę.
2mpaka siku ile alipochukuliwa mbinguni. Kabla ya kuchukuliwa mbinguni aliwapa maagizo kwa njia ya Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua.
3Którym też samego siebie po męce swojej żywym stawił w wielu niewątpliwych dowodach, przez czterdzieści dni ukazując się im i mówiąc o królestwie Bożem.
3Kwa muda wa siku arobaini baada ya kifo chake aliwatokea mara nyingi kwa namna ambazo zilithibitisha kabisa kwamba alikuwa hai. Walimwona, naye aliongea nao juu ya ufalme wa Mungu.
4A zgromadziwszy je przykazał im, aby nie odchodzili z Jeruzalemu, ale iżby czekali obietnicy ojcowskiej, o którejście mówić słyszeli ode mnie.
4Wakati walipokutana pamoja aliwaamuru hivi: "Msiondoke Yerusalemu, bali ngojeeni ile zawadi aliyoahidi Baba, zawadi ambayo mlikwisha nisikia nikiongea juu yake.
5Albowiemci Jan chrzcił wodą; ale wy będziecie ochrzczeni Duchem Świętym po niewielu tych dniach.
5Kwani Yohane alibatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache, ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu."
6A tak oni zszedłszy się, pytali go, mówiąc: Panie! izali w tym czasie naprawisz królestwo Izraelskie?
6Basi, mitume walipokutana pamoja na Yesu, walimwuliza, "Je Bwana, wakati huu ndipo utakaporudisha ule ufalme kwa Israeli?"
7Lecz on rzekł do nich: Nie wasza rzecz jest, znać czasy i chwile, które Ojciec w swojej mocy położył.
7Lakini Yesu akawaambia, "Nyakati na majira ya mambo hayo viko chini ya mamlaka ya Baba yangu, wala si shauri lenu kujua yatakuwa lini.
8Ale przyjmiecie moc Ducha Świętego, który przyjdzie na was; i będziecie mi świadkami i w Jeruzalemie, i we wszystkiej Judzkiej ziemi, i w Samaryi, aż do ostatniego kraju ziemi.
8Lakini wakati Roho Mtakatifu atakapowashukieni ninyi, mtajazwa nguvu na mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika nchi yote ya Yudea na Samaria, na hata miisho ya dunia."
9A to rzekłszy, gdy oni patrzali, w górę podniesiony jest, a obłok wziął go od oczów ich.
9Baada ya kusema hayo, wote wakiwa wanamtazama, alichukuliwa mbinguni; wingu likamficha wasimwone tena.
10A gdy za nim do nieba idącym pilnie patrzali, oto dwaj mężowie stanęli przy nich w białem odzieniu,
10Walipokuwa bado wanatazama juu angani, akiwa anakwenda zake, mara watu wawili waliokuwa wamevaa nguo nyeupe walisimama karibu nao,
11I rzekli: Mężowie Galilejscy! przecz stoicie, patrząc w niebo? Ten Jezus, który w górę wzięty jest od was do nieba, tak przyjdzie, jakoście go widzieli idącego do nieba.
11wakasema, "Enyi wananchi wa Galilaya! Mbona mnasimama mkitazama angani? Yesu huyu ambaye amechukuliwa kutoka kwenu kwenda mbinguni atakuja tena namna hiyohiyo mliivyomwona akienda mbinguni."
12Tedy się wrócili do Jeruzalemu od góry, którą zowią oliwną, która jest blisko Jeruzalemu, mając drogi przez jeden sabat.
12Kisha mitume wakarudi Yerusalemu kutoka mlima wa Mizeituni ulioko karibu kilomita moja kutoka mjini.
13A gdy weszli, wstąpili na salę, gdzie mieszkali Piotr, i Jakób, i Jan, i Andrzej, i Filip, i Tomasz, Bartłomiej, i Mateusz, Jakób Alfeuszowy, i Szymon Zelotes, i Judas Jakóbowy.
13Walipofika mjini waliingia katika chumba ghorofani ambamo walikuwa wanakaa; nao walikuwa Petro, Yohane, Yakobo, Andrea, Filipo na Thoma, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda mwana wa Yakobo.
14Ci wszyscy trwali jednomyślnie na modlitwie i prośbach, z żonami i z Maryją, matką Jezusową, i z braćmi jego.
14Hawa wote walikusanyika pamoja kusali, pamoja na wanawake kadha wa kadha, na Maria mama yake Yesu, na ndugu zake.
15A w oneż dni, powstawszy Piotr w pośrodku uczniów, rzekł: (A był poczet osób wespół zgromadzonych około sta i dwudziestu):
15Siku chache baadaye, kulikuwa na mkutano wa waumini, karibu watu mia moja na ishirini. Petro alisimama mbele yao,
16Mężowie bracia! musiało się wypełnić ono pismo, które opowiedział Duch Święty przez usta Dawidowe o Judaszu, który był wodzem tych, co pojmali Jezusa;
16akasema, "Ndugu zangu, ilikuwa lazima ile sehemu ya Maandiko Matakatifu itimie, sehemu ambayo Roho Mtakatifu, kwa maneno ya Daudi, alibashiri habari za Yuda ambaye aliwaongoza wale waliomtia Yesu nguvuni.
17Bo był policzony z nami i dostał był cząstki tego usługiwania.
17Yuda alikuwa mmoja wa kikundi chetu maana alichaguliwa ashiriki huduma yetu.
18Tenci wprawdzie otrzymał rolę z zapłaty niesprawiedliwości, a powiesiwszy się, rozpukł się na poły i wypłynęły wszystkie wnętrzności jego.
18("Mnajua kwamba yeye alinunua shamba kwa zile fedha alizopata kutokana na kitendo chake kiovu. Akaanguka chini, akapasuka na matumbo yake yakamwagika nje.
19I było to jawne wszystkim mieszkającym w Jeruzalemie, tak iż nazwano onę rolę własnym ich językiem Akieldama, to jest rola krwi.
19Kila mtu katika Yerusalemu alisikia habari za tukio hilo na hivyo, kwa lugha yao, wakaliita lile shamba Hekeli Dama, maana yake, Shamba la Damu.)
20Albowiem napisano w księgach Psalmów: Niechaj będzie mieszkanie jego puste, a niech nie będzie, kto by w niem mieszkał, a biskupstwo jego niech weźmie inny.
20Basi, imeandikwa katika kitabu cha Zaburi: Nyumba yake ibaki mahame; mtu yeyote asiishi ndani yake. Tena imeandikwa: Mtu mwingine achukue nafasi yake katika huduma hiyo.
21Potrzeba tedy, aby jeden z tych mężów, którzy z nami bywali po wszystek czas, który Pan Jezus przebywał między nami,
21Kwa hiyo, ni lazima mtu mwingine ajiunge nasi kama shahidi wa ufufuo wake Bwana Yesu.
22Począwszy od chrztu Janowego, aż do tego dnia, którego jest wzięty w górę od nas, był z nami świadkiem zmartwychwstania jego.
22Anapaswa kuwa mmoja wa wale waliokuwa katika kundi letu wakati wote Bwana alipokuwa anasafiri pamoja nasi, tangu wakati Yohane alipokuwa anabatiza mpaka siku ile Yesu alipochukuliwa kutoka kwetu kwenda mbinguni."
23I postawili dwóch: Józefa, którego zwano Barsabaszem, którego też nazywano Justem, i Macieja.
23Basi, wakataja majina ya watu wawili; wa kwanza Yosefu aliyeitwa Barsaba (au pia Yusto), na wa pili Mathia.
24A modląc się mówili: Ty Panie! który znasz serca wszystkich, okaż z tych dwóch jednego, któregoś obrał;
24Kisha wakasali: "Bwana, wewe unajua mioyo ya watu wote. Hivyo, utuonyeshe ni yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua
25Aby przyjął cząstkę usługiwania tego i apostolstwa, z którego wypadł Judasz, aby odszedł na miejsce swoje.
25ili achukue nafasi hii ya huduma ya kitume aliyoacha Yuda akaenda mahali pake mwenyewe."
26I rzucili losy ich. I padł los na Macieja; a przyłączony jest spólnem zdaniem do jedenastu Apostołów.
26Hapo, wakapiga kura; kura ikampata Mathia, naye akaongezwa katika idadi ya wale mitume wengine kumi na mmoja.