Polish

Swahili: New Testament

Acts

12

1A pod onże czas, udał się na to Herod król, aby trapił niektóre ze zboru.
1Karibu wakati huohuo, mfalme Herode alianza kuwatesa baadhi ya Wakristo.
2I zabił Jakóba, brata Janowego, mieczem.
2Alimwua kwa upanga Yakobo ndugu yake Yohane.
3A widząc, że się to podobało Żydom, umyślił pojmać i Piotra: (a były dni przaśników).
3Alipoona kuwa kitendo hiki kiliwapendeza Wayahudi, aliendelea, akamkamata Petro. (Hiyo ilifanyika wakati wa sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu.)
4Którego pojmawszy, podał do więzienia, poruczywszy go szesnastu żołnierzom, aby go strzegli, chcąc go po wielkanocy wywieść ludowi.
4Baada ya kutiwa nguvuni, Petro alifungwa gerezani, akawekwa chini ya ulinzi wa vikundi vinne vya askari wannewanne. Herode alikusudia kumtoa hadharani baada ya sikukuu ya Pasaka.
5Tedy strzeżono Piotra w więzieniu, a modlitwa ustawiczna działa się od zboru do Boga za nim.
5Basi, Petro alipokuwa gerezani, kanisa lilikuwa linamwombea kwa Mungu kwa moyo.
6A gdy go już miał wywieść Herod, onejże nocy spał Piotr między dwoma żołnierzami, związany dwoma łaócuchami, a stróże przed drzwiami strzegli więzienia.
6Usiku, kabla ya siku ile ambayo Herode angemtoa Petro hadharani, Petro alikuwa amelala kati ya askari wawili. Alikuwa amefungwa minyororo miwili, na walinzi walikuwa wanalinda lango la gereza.
7A oto Anioł Paóski przystąpił, a światłość się rozświeciła w gmachu; a trąciwszy w bok Piotra, obudził go, mówiąc: Wstaó rychło! I opadły łaócuchy z rąk jego.
7Ghafla, malaika wa Bwana akasimama karibu naye na mwanga ukaangaza kile chumba cha gereza. Malaika akamgusa akisema, "Amka upesi!" Mara ile minyororo ikaanguka kutoka katika mikono yake.
8I rzekł Anioł do niego: Opasz się, a powiąż obuwie twoje. I uczynił tak. I rzekł mu: Odziej się w płaszcz twój, a pójdź za mną.
8Malaika akamwambia, "Jifunge mshipi wako, vaa viatu vyako." Akafanya hivyo. Kisha huyo malaika akamwambia, "Vaa koti lako, unifuate."
9Tedy wyszedłszy Piotr, szedł za nim, a nie wiedział, że się to działo po prawdzie, co się działo przez Anioła; lecz mniemał, że widzenie widział.
9Petro akamfuata nje lakini hakujua kama hayo yaliyofanywa na huyo malaika yalikuwa ya kweli; alidhani alikuwa anaota ndoto.
10A gdy minęli pierwszą i wtórą straż, przyszli do bramy żelaznej, która wiedzie do miasta; a ta się im sama przez się otworzyła. A wyszedłszy, przeszli jednę ulicę, a zarazem odstąpił Anioł od niego.
10Walipita kituo cha kwanza cha ulinzi na cha pili, halafu wakafika kwenye mlango wa chuma wa kuingilia mjini. Huo mlango ukawafungukia wenyewe, nao wakatoka nje. Wakawa wanatembea katika barabara moja na mara yule malaika akamwacha Petro peke yake.
11Tedy Piotr przyszedłszy do siebie rzekł: Teraz znam prawdziwie, iż posłał Pan Anioła swego i wyrwał mię z ręki Herodowej i ze wszystkiego oczekiwania ludu żydowskiego.
11Hapo ndipo Petro alipotambua yaliyotukia, akasema, "Sasa najua kwa hakika kwamba Bwana amemtuma malaika wake akaniokoa kutoka katika mkono wa Herode na kutoka katika mambo yale yote watu wa Israeli waliyotazamia."
12A obaczywszy się, przyszedł do domu Maryi, matki Janowej, którego nazywano Markiem, gdzie się ich było wiele zgromadziło i modlili się.
12Alipotambua hivyo alikwenda moja kwa moja mpaka nyumbani kwa Maria mama yake Yohane aitwaye Marko. Humo watu wengi walikuwa wamekusanyika wakisali.
13A gdy Piotr kołatał we drzwi u przysionka, wyszła dzieweczka, imieniem Rode, aby posłuchała:
13Petro alibisha mlango wa nje na mtumishi mmoja msichana aitwaye Roda, akaenda mlangoni kuitikia.
14A poznawszy głos Piotrowy, od radości nie otworzyła drzwi, ale wbieżawszy oznajmiła, iż Piotr stoi u drzwi.
14Huyo msichana aliitambua sauti ya Petro akafurahi mno, hata badala ya kuufungua ule mlango, akakimbilia ndani na kuwaambia kwamba Petro alikuwa amesimama nje mlangoni.
15A oni rzekli do niej: Szalejesz! Wszakże ona twierdziła, iż się tak rzecz ma. A oni rzekli: Anioł jego jest.
15Wakamwambia yule msichana, "Una wazimu!" Lakini yeye akasisitiza kwamba ilikuwa kweli. Nao wakamwambia, "Huyo ni malaika wake."
16Ale Piotr nie przestał kołatać; a gdy otworzyli, ujrzeli go i zdumieli się.
16Wakati huo Petro alikuwa anaendelea kupiga hodi. Mwishowe walifungua mlango, wakamwona, wakashangaa.
17A skinąwszy na nie ręką, aby umilknęli, rozpowiedział im, jako go Pan wywiódł z więzienia i rzekł: Oznajmijcie to Jakóbowi i braciom. A wyszedłszy, szedł na inne miejsce.
17Petro aliwaashiria kwa mkono wakae kimya, akawaeleza jinsi Bwana alivyomtoa gerezani. Kisha akawaambia watoe taarifa ya jambo hilo kwa Yakobo na wale ndugu wengine, halafu akatoka akaenda mahali pengine.
18A gdy był dzieó, stał się rozruch niemały między żołnierzami o to, co by się z Piotrem stało.
18Kulipokucha, ulitokea wasiwasi mkubwa kati ya wale askari kuhusu yaliyokuwa yamempata Petro.
19Lecz Herod, gdy się o nim wywiadywał, a nie znalazł go, uczyniwszy sąd o stróżach, kazał je na stracenie wywieść; a wyjechawszy z Judzkiej ziemi do Cezaryi, mieszkał tam.
19Herode aliamuru ufanywe msako lakini hawakuweza kumpata. Hivyo aliamuru wale askari wahojiwe, akatoa amri wauawe. Halafu akatoka huko Yudea akaenda Kaisarea ambako alikaa.
20A natenczas Herod myślił o wojnie przeciwko Tyryjczykom i Sydoóczykom; ale oni jednomyślnie przyszli do niego, a namówiwszy Blasta, podkomorzego królewskiego, prosili o pokój, dlatego iż kraina ich miała żywność z dzierżawy królewskiej.
20Herode alikasirishwa sana na watu wa Tiro na Sidoni. Lakini wao walimpelekea wajumbe. Nao wakafaulu kwanza kumpata Blasto awe upande wao. Blasto alikuwa msimamizi mkuu wa ikulu ya mfalme. Kisha, wakamwendea Herode wakamwomba kuwe na amani, kwa maana nchi yao ilitegemea nchi ya mfalme kwa chakula.
21A dnia pewnego Herod oblekłszy się w szatę królewską i siadłszy na stolicy, uczynił rzecz do nich.
21Siku moja iliyochaguliwa, Herode akiwa amevaa mavazi rasmi na kuketi katika kiti cha kifalme aliwahutubia watu.
22A lud wołał: Głos Boży a nie człowieczy.
22Wale watu walimpigia kelele za shangwe wakisema, "Hii ni sauti ya mungu, si ya mtu."
23A zarazem uderzył go Anioł Paóski, przeto, że nie dał chwały Bogu, a będąc roztoczony od robactwa, zdechł.
23Papo hapo malaika wa Bwana akamwangusha Herode chini kwa sababu hakumpa Mungu hizo sifa. Akaliwa na wadudu, akafa.
24A słowo Paóskie rozrastało się i rozmnażało.
24Neno la Mungu likazidi kuenea na kukua.
25A Barnabasz i Saul wrócili się z Jeruzalemu, wykonawszy posługę, wziąwszy z sobą Jana, którego nazywano Markiem.
25Baada ya Barnaba na Saulo kutekeleza shughuli zao, walitoka tena Yerusalemu wakamchukua Yohane aitwaye pia Marko.