Polish

Swahili: New Testament

Acts

14

1I stało się w Ikonii, że także weszli do bóżnicy żydowskiej, a tak mówili, że uwierzyło i Żydów, i Greków wielkie mnóstwo.
1Kule Ikonio, mambo yalikuwa kama yalivyokuwa kule Antiokia; Paulo na Barnaba walikwenda katika sunagogi la Wayahudi wakaongea kwa uhodari hata Wayahudi wengi na Wagiriki wakawa waumini.
2Lecz Żydowie, którzy nie uwierzyli, podburzyli i zajątrzyli serca pogan przeciwko braciom.
2Lakini Wayahudi wengine waliokataa kuwa waumini walichochea na kutia chuki katika mioyo ya watu wa mataifa mengine ili wawapinge hao ndugu.
3I byli tam przez długi czas, bezpiecznie mówiąc w Panu, który dawał świadectwo słowu łaski swojej i czynił to, że się działy znamiona i cuda przez ręce ich.
3Paulo na Barnaba waliendelea kukaa huko kwa muda mrefu. Waliongea kwa uhodari juu ya Bwana, naye Bwana akathibitisha ukweli wa ujumbe walioutoa juu ya neema yake, kwa kuwawezesha kutenda miujiza na maajabu.
4I rozerwało się mnóstwo miejskie, a byli jedni z Żydami a drudzy z Apostołami.
4Watu wa mji huo waligawanyika: wengine waliwaunga mkono Wayahudi, na wengine walikuwa upande wa mitume.
5A gdy się wzburzyli i poganie, i Żydzi z książęty swoimi, aby je zelżyli i ukamionowali:
5Mwishowe, baadhi ya watu wa mataifa mengine na Wayahudi, wakishirikiana na wakuu wao, waliazimu kuwatendea vibaya hao mitume na kuwapiga mawe.
6Zrozumiawszy to, uciekli do miast Likaoóskich, do Listry i do Derby, i do okolicznej krainy,
6Mitume walipogundua jambo hilo, walikimbilia Lustra na Derbe, miji ya Lukaonia, na katika sehemu za jirani,
7A tam kazali Ewangieliję.
7wakawa wanahubiri Habari Njema huko.
8A mąż niektóry w Listrze chory na nogi siedział, będąc chromy z żywota matki swojej, który nigdy nie chodził.
8Kulikuwa na mtu mmoja huko Lustra ambaye alikuwa amelemaa miguu tangu kuzaliwa, na alikuwa hajapata kutembea kamwe.
9Ten słuchał Pawła mówiącego; który naó pilnie patrząc i widząc, iż miał wiarę, żeby mógł być uzdrowiony,
9Mtu huyo alikuwa anamsikiliza Paulo alipokuwa anahubiri. Paulo alimtazama kwa makini, na alipoona kuwa alikuwa na imani ya kuweza kuponywa,
10Rzekł wielkim głosem: Staó prosto na nogi twoje; i wyskoczył i chodził.
10akasema kwa sauti kubwa, "Simama wima kwa miguu yako!" Huyo mtu aliyelemaa akainuka ghafla, akaanza kutembea.
11A lud widząc, co Paweł uczynił, podnieśli głos swój, mówiąc po likaoósku: Bogowie stawszy się podobni ludziom, zstąpili do nas.
11Umati wa watu walipoona alichofanya Paulo, ulianza kupiga kelele kwa lugha ya Kilukaonia: "Miungu imetujia katika sura za binadamu!"
12I nazwali Barnabasza Jowiszem, a Pawła Merkuryjuszem, ponieważ on prowadził rzecz.
12Barnaba akaitwa Zeu, na Paulo, kwa vile yeye ndiye aliyekuwa anaongea, akaitwa Herme.
13Tedy kapłan Jowisza, który był przed miastem ich, woły z wieócami do wrót przywiódłszy, chciał ofiary z ludem sprawować.
13Naye kuhani wa hekalu la Zeu lililokuwa nje ya mji akaleta fahali na shada za maua mbele ya mlango mkuu wa mji, na pamoja na ule umati wa watu akataka kuwatambikia mitume.
14Co gdy usłyszeli Apostołowie Barnabasz i Paweł, rozdarłszy szaty swoje, wpadli między lud, wołając,
14Barnaba na Paulo walipopata habari hiyo waliyararua mavazi yao na kukimbilia katika lile kundi la watu wakisema kwa sauti kubwa:
15I mówiąc: Mężowie! cóż to czynicie? I myśmyć ludzie, tymże biedom jako i wy poddani, którzy wam opowiadamy, abyście się od tych marności nawrócili do Boga żywego, który uczynił niebo i ziemię i morze, i wszystko co w nich jest.
15"Ndugu, kwa nini mnafanya mambo hayo? Sisi pia ni binadamu kama ninyi. Na, tuko hapa kuwahubirieni Habari Njema, mpate kuziacha hizi sanamu tupu, mkamgeukie Mungu aliye hai, Mungu aliyeumba mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo.
16Który za przeszłych wieków dopuszczał wszystkim poganom, aby chodzili za drogami swemi.
16Zamani Mungu aliruhusu kila taifa lifanye lilivyopenda.
17Aczkolwiek nie zaniechał samego siebie prócz świadectwa, czyniąc dobrze, dawając nam z nieba dżdże i czasy urodzajne, napełniając pokarmem i weselem serca nasze.
17Hata hivyo, Mungu hakuacha kujidhihirisha kwa mambo mema anayowatendea: huwanyeshea mvua toka angani, huwapa mavuno kwa wakati wake, huwapa chakula na kuijaza mioyo yenu furaha."
18A to mówiąc, zaledwie uspokoili lud, że im nie ofiarował.
18Ingawa walisema hivyo haikuwa rahisi kuwazuia wale watu wasiwatambikie.
19A nadeszli z Antyjochyi i z Ikonii Żydowie, którzy namówiwszy lud i ukamionowawszy Pawła, wywlekli za miasto, mniemając żeby umarł.
19Lakini Wayahudi kadhaa walikuja kutoka Antiokia na Ikonio, wakawafanya watu wajiunge nao, wakampiga mawe Paulo na kumburuta hadi nje ya mji wakidhani amekwisha kufa.
20Lecz gdy go uczniowie obstąpili, wstawszy wszedł do miasta, a nazajutrz odszedł z Barnabaszem do Derby.
20Lakini waumini walipokusanyika na kumzunguka, aliamka akarudi mjini. Kesho yake, yeye pamoja na Barnaba walikwenda Derbe.
21A opowiedziawszy Ewangieliję onemu miastu i wiele uczniów pozyskawszy, wrócili się do Listry, do Ikonii, i do Antyjochyi;
21Baada ya Paulo na Barnabas kuhubiri Habari Njema huko Derbe na kupata wafuasi wengi, walifunga safari kwenda Antiokia kwa kupitia Lustra na Ikonio.
22Utwierdzając dusze uczniów i napominając, aby trwali w wierze, i mówiąc: Że przez wiele ucisków musimy wnijść do królestwa Bożego.
22Waliwaimarisha waumini wa miji hiyo na kuwatia moyo wabaki imara katika imani. Wakawaambia, "Ni lazima sisi sote tupitie katika taabu nyingi ili tuingie katika ufalme wa Mungu."
23A gdy im przez głosy postanowili starsze w każdym zborze i modlili się z postami, poruczyli je Panu, w którego uwierzyli.
23Waliteua wazee katika kila kanisa kwa ajili ya waumini, na baada ya kusali na kufunga, wakawaweka chini ya ulinzi wa Bwana ambaye walikuwa wanamwamini.
24A przeszedłszy Pisydyję, przyszli do Pamfilii.
24Baada ya kupitia katika nchi ya Pisidia, walifika Pamfulia.
25I opowiedziawszy słowo Boże w Pergi, poszli do Atalii.
25Baada ya kuhubiri ule ujumbe huko Perga, walikwenda Atalia.
26A stamtąd płynęli do Antyjochyi, skąd byli oddani łasce Bożej ku tej sprawie, którą wykonali.
26Kutoka huko walisafiri kwa meli wakarudi Antiokia ambako hapo awali walikuwa wamewekwa chini ya ulinzi wa neema ya Mungu kwa ajili ya kazi ambayo sasa walikuwa wameitimiza.
27A gdy tam przyszli i zgromadzili zbór, oznajmili, co Bóg przez nie uczynił, a iż poganom drzwi wiary otworzył.
27Walipofika huko Antiokia walifanya mkutano wa kanisa la mahali hapo, wakawapa taarifa juu ya mambo Mungu aliyofanya pamoja nao, na jinsi alivyowafungulia mlango watu wa mataifa mengine mlango wa kuingia katika imani.
28I mieszkali tam czas niemały z uczniami.
28Wakakaa pamoja na wale waumini kwa muda mrefu.