Polish

Swahili: New Testament

Acts

17

1A przeszedłszy Amfipolim i Apoloniję przyszli do Tesaloniki, gdzie była bóżnica żydowska.
1Kwa kupitia Amfipoli na Apolonia, walisafiri mpaka Thesalonika ambako kulikuwa na sunagogi la Wayahudi.
2Tedy Paweł według zwyczaju swego wszedł do nich, a przez trzy sabaty kazał im z Pisma.
2Paulo alijiunga nao kama ilivyokuwa desturi yake akajadiliana nao Sabato tatu mfululizo, akatumia Maandiko Matakatifu.
3Wywodząc i pokazując to, że Chrystus miał cierpieć i powstać od umarłych, a iż ten Jezus jest Chrystusem, którego ja wam opowiadam.
3Aliyaeleza na kuonyesha kwamba ilimbidi Kristo kuteswa na kufufuka kutoka wafu. Akawaambia, "Yesu ambaye mimi namhubiri kwenu ndiye Kristo."
4I uwierzyli niektórzy z nich, a przyłączyli się do Pawła i do Syli, i wielkie mnóstwo nabożnych Greków, i niewiast przedniejszych niemało.
4Baadhi yao walikubali wakajiunga na Paulo na Sila. Kadhalika, idadi kubwa ya Wagiriki waliomcha Mungu pamoja na wanawake wengi wa tabaka la juu, walijiunga nao.
5Ale Żydowie, którzy nie uwierzyli, zdjęci zazdrością, przywziąwszy do siebie niektórych lekkomyślnych i złych mężów, a zebrawszy kupę uczynili rozruch w mieście, a naszedłszy na dom Jazona, szukali ich, aby ich wywiedli przed lud.
5Lakini Wayahudi wakaona wivu; wakawakodi wafidhuli sokoni, wakafanya kikundi na kuzusha fujo mjini kote. Wakaivamia nyumba ya Yasoni wakitumaini kuwapata humo Paulo na Sila ili wawalete hadharani.
6A nie znalazłszy ich, ciągnęli Jazona i niektórych braci do przełożonych miasta, wołając: Oto ci, którzy wszystek świat wzruszyli i tu też przyszli;
6Lakini hawakuwapata na hivyo walimburuta Yasoni pamoja na ndugu wengine mpaka kwa wakuu wa mji, wakapiga kelele: "Watu hawa wamekuwa wakivuruga dunia yote na sasa wako hapa mjini.
7Które przyjął Jazon; a ci wszyscy czynią przeciwko dekretom cesarskim, powiadając, iż jest inszy król, Jezus.
7Yasoni amewakaribisha nyumbani kwake. Wote wanafanya kinyume cha amri ya Kaisari wakisema eti Kuna mfalme mwingine aitwaye Yesu."
8A tak wzburzyli pospólstwo i przełożonych miasta, którzy to słyszeli.
8Kwa maneno hayo waliwatia wasiwasi wakuu wa mji na kundi la watu.
9Ale oni wziąwszy słuszną sprawę od Jazona i od innych, puścili je.
9Wakawafanya Yasoni na wenzake watoe dhamana, kisha wakawaacha waende zao.
10A bracia wnet w nocy wysłali i Pawła, i Sylę do Berei; którzy tam przyszedłszy weszli do bóżnicy żydowskiej.
10Usiku, wale ndugu waliwahimiza Paulo na Sila waende Berea. Mara tu walipofika huko, walikwenda katika sunagogi la Wayahudi.
11A cić byli zacniejsi nad one, co byli w Tesalonice, którzy przyjęli słowo Boże ze wszystką ochotą, na każdy dzieó rozsądzając Pisma, jeźliby się tak miało.
11Watu wa huko walikuwa wasikivu zaidi kuliko wale wa Thesalonika. Waliupokea ule ujumbe kwa hamu kubwa, wakawa wanayachunguza Maandiko Matakatifu kila siku, ili kuona kama yale waliyosema Paulo na Sila yalikuwa kweli.
12Przetoż wiele ich z nich uwierzyło, i Greckich niewiast uczciwych, i mężów niemało.
12Wengi wao waliamini na pia wanawake wa Kigiriki wa tabaka la juu na wanaume pia.
13A gdy się dowiedzieli oni, co byli z Tesaloniki Żydowie, że i w Berei opowiadane było słowo Boże od Pawła, przyszli i tam, podburzając pospólstwo.
13Lakini, Wayahudi wa Thesalonika walipogundua kwamba Paulo alikuwa anahubiri neno la Mungu huko Berea, walikwenda huko, wakaanza kufanya fujo na kuchochea makundi ya watu.
14Ale bracia wnet wysłali Pawła, aby szedł jakoby do morza; a Sylas i Tymoteusz tam zostali.
14Wale ndugu wakamsindikiza haraka aende pwani lakini Sila na Timotheo walibaki Berea.
15A ci, którzy prowadzili Pawła, doprowadzili go aż do Aten, a wziąwszy rozkazanie do Syli i do Tymoteusza, żeby co najrychlej przyszli do niego, odeszli.
15Wale ndugu waliomsindikiza Paulo walikwenda pamoja naye mpaka Athene. Kisha, wakarudi pamoja na maagizo kutoka kwa Paulo kwamba Sila na Timotheo wamfuate upesi iwezekanavyo.
16A gdy ich Paweł w Atenach czekał, poruszał się w nim duch jego, widząc ono miasto poddane bałwochwalstwu.
16Paulo alipokuwa anawasubiri Sila na Timotheo huko Athene, moyo wake ulighadhibika sana alipoona jinsi mji huo ulivyokuwa umejaa sanamu za miungu.
17A przetoż miewał rozmowę z Żydami i z ludźmi nabożnymi, w bóżnicy i na rynku na każdy dzieó, z kim się mu trafiło.
17Alijadiliana na Wayahudi na watu wengine waliomcha Mungu katika sunagogi; na kila siku alikuwa na majadiliano sokoni pamoja na wowote wale waliojitokeza.
18Tedy niektórzy z Epikurejczyków i Stoików filozofowie spierali się z nim, a niektórzy mówili: Cóż wżdy ten plotkarz mówić chce? A drudzy: Zdaje się być opowiadaczem obcych bogów; bo im Jezusa i zmartwychwstanie opowiadał.
18Wengine waliofuata falsafa ya Epikuro na Stoiki walibishana naye. Wengine walisema, "Anataka kusema nini huyu bwanamaneno?" Kwa kuwa Paulo alikuwa anahubiri juu ya Yesu na juu ya ufufuo, wengine walisema, "Inaonekana kama anahubiri juu ya miungu ya kigeni."
19A porwawszy go, wiedli do Areopagu, mówiąc: Możemyli wiedzieć, co to jest za nowa nauka, którą ty opowiadasz?
19Hivyo walimchukua Paulo, wakampeleka Areopago, wakasema, "Tunataka kujua jambo hili jipya ulilokuwa unazungumzia.
20Bo jakieś obce rzeczy przynosisz do uszów naszych; chcemy tedy wiedzieć, co wżdy z tego ma być?
20Vitu vingine tulivyosikia kwa masikio yetu vinaonekana kuwa viroja kwetu. Tungependa kujua mambo haya yana maana gani."
21(A wszyscy Ateóczycy i cudzoziemscy goście niczem inszem się nie bawili, tylko powiadaniem albo słuchaniem nowin.)
21Wananchi wa Athene na wakazi wengine wa huko walikuwa wanatumia wakati wao wote kuhadithiana na kusikiliza habari mpyampya.
22Tedy Paweł stanąwszy w pośrodku Areopagu, rzekł: Mężowie Ateóscy! z każdej miary was widzę nader nabożnych.
22Basi, Paulo alisimama mbele ya baraza la Areopago, akasema, "Wananchi wa Athene! Ninaona kwamba ninyi, kwa vyovyote, ni watu wa dini sana.
23Albowiem przechadzając się i przypatrując waszym nabożeóstwom, znalazłem też ołtarz, na którym napisano: Nieznajomemu Bogu. Którego tedy nie znając chwalicie, tego ja wam opowiadam.
23Sababu yenyewe ni kwamba katika pitapita yangu niliangalia sanamu zenu za ibada nikakuta madhabahu moja ambayo imeandikwa: Kwa ajili ya Mungu yule Asiyejulikana. Basi, huyo mnayemwabudu bila kujua, ndiye ninayemhubiri kwenu.
24Bo Bóg, który uczynił świat i wszystko, co na nim, ten będąc Panem nieba i ziemi, nie mieszka w kościołach ręką uczynionych.
24Mungu, aliyeumba ulimwengu na vyote vilivyomo, ni Bwana wa mbingu na nchi; yeye hakai katika hekalu zilizojengwa na watu.
25Ani rękoma ludzkiemi chwalony bywa, jakoby czego potrzebował, ponieważ on daje wszystkim żywot i oddech, i wszystko.
25Wala hatumikiwi kwa mikono ya watu kana kwamba anahitaji chochote kile, kwa maana yeye mwenyewe ndiye anayewapa watu uhai, anawawezesha kupumua na anawapa kila kitu.
26I uczynił z jednej krwi wszystek naród ludzki, aby mieszkał po wszystkiem obliczu ziemi, zamierzywszy przedtem rozrządzone czasy i zamierzone granice mieszkania ich;
26Kutokana na mtu mmoja aliumba mataifa yote na kuyawezesha kuishi duniani kote. Aliamua na kupanga kabla kabisa lini na wapi mataifa hayo yangeishi.
27Aby szukali Pana, owaby go snać namacali i znaleźli, aczkolwiek od każdego z nas nie jest daleko.
27Alifanya hivyo, ili mataifa hayo yapate kumfuata, na kama vile kwa kupapasapapasa, yapate kumfikia. Hata hivyo lakini, Mungu hayuko mbali na kila mmoja wetu.
28Albowiem w nim żyjemy i ruszamy się, i jesteśmy, jako i niektórzy z waszych poetów powiedzieli: Żeśmy i my rodziną jego.
28Kama alivyosema mtu mmoja: Ndani yake yeye sisi tunaishi, tunajimudu, na tuko! Ni kama washairi wenu wengine walivyosema: Sisi ni watoto wake.
29Będąc tedy rodziną Bożą, nie mamy rozumieć, żeby złotu albo srebru, albo kamieniowi misternie rytemu, albo wymysłowi człowieczemu, Bóg miał być podobny.
29Ikiwa basi, sisi ni watoto wa Mungu, haifai kumfikiria Mungu kuwa kama dhahabu, fedha au hata jiwe lililochongwa na kutiwa nakshi na binadamu.
30Aczkolwiek tedy przeglądał Bóg czasom tej niewiadomości, ale teraz oznajmuje ludziom wszystkim wszędy, aby pokutowali;
30Mungu alifanya kama kwamba haoni nyakati zile watu walipokuwa wajinga. Lakini sasa, anaamuru watu wote kila mahali watubu.
31Przeto iż postanowił dzieó, w który będzie sądził wszystek świat w sprawiedliwości przez męża, którego na to naznaczył, upewniając o tem wszystkich, wzbudziwszy go od umarłych.
31Kwa maana amekwisha weka siku ambayo atauhukumu ulimwengu kwa haki kwa njia ya mtu mmoja aliyemteua. Mungu amewathibitishia wote jambo hili kwa kumfufua mtu huyo kutoka wafu!"
32A usłyszawszy o zmartwychwstaniu jedni się naśmiewali, a drudzy mówili: Będziemy cię znowu o tem słuchać.
32Walipomsikia Paulo anasema juu ya jambo la kufufuka kwa wafu, wengine wao waliangua kicheko; lakini wengine walisema, "Tunataka kukusikia tena juu ya jambo hili!"
33I tak Paweł wyszedł z pośrodku ich.
33Hivyo, Paulo aliwaacha, akatoka barazani.
34A mężowie niektórzy przyłączywszy się do niego, uwierzyli, między którymi też był Dyjonizyjusz Areopagitczyk i niewiasta imieniem Damarys, i inni z nimi.
34Lakini watu kadhaa waliandamana naye, wakawa waumini. Miongoni mwao walikuwa Dionisio wa Areopago, mwanamke mmoja aitwaye Damari na wengineo.