1A w oneż dni, gdy się przymnażało uczniów, wszczęło się szemranie Greków przeciwko Żydom, iż były zaniedbywane w posługiwaniu powszedniem wdowy ich.
1Baadaye, idadi ya wanafunzi ilipokuwa inazidi kuongezeka, kulitokea manung'uniko kati ya wanafunzi waliosema Kigiriki na wale waliosema Kiebrania. Wale waliosema Kigiriki walinung'unika kwamba wajane wao walikuwa wanasahauliwa katika ugawaji wa mahitaji ya kila siku.
2A tak oni dwunastu zwoławszy mnóstwo uczniów, rzekli: Nie jest słuszna, żebyśmy my opuściwszy słowo Boże, służyli stołom.
2Kwa hiyo, mitume kumi na wawili waliita jumuiya yote ya wanafunzi, wakasema, "Si vizuri sisi tuache kulihubiri neno la Mungu ili tushughulikie ugawaji wa mahitaji.
3Upatrzcież tedy, bracia! między sobą siedm mężów, dobre świadectwo mających, pełnych Ducha Świętego i mądrości, których byśmy postanowili nad tą sprawą.
3Hivyo, ndugu zetu, chagueni miongoni mwenu watu saba wenye sifa njema, waliojawa na Roho na wenye hekima; nasi tutawakabidhi jukumu hilo.
4A my modlitwy i usługi słowa pilnować będziemy.
4Sisi, lakini, tutashughulika na sala na kazi ya kuhubiri neno la Mungu."
5I podobała się ta rzecz onemu wszystkiemu mnóstwu. I obrali Szczepana, męża pełnego wiary i Ducha Świętego, i Filipa, i Prochora, i Nikanora, i Tymona, i Parmena, i Mikołaja, nowonawróconego Antyjocheóczyka.
5Jambo hilo likaipendeza jumuiya yote ya waumini. Wakawachagua Stefano, mtu mwenye imani kubwa na mwenye kujawa na Roho Mtakatifu, Filipo, Prokoro, Nikanora, Timona, Parmena na Nikolao wa Antiokia ambaye hapo awali alikuwa ameongokea dini ya Kiyahudi.
6Tych stawili przed Apostołów, którzy pomodliwszy się, kładli na nich ręce.
6Wakawaweka mbele ya mitume, nao wakawaombea na kuwawekea mikono.
7I rosło słowo Boże, i pomnażał się bardzo poczet uczniów w Jeruzalemie: wielkie też mnóstwo kapłanów było posłuszne wierze.
7Neno la Mungu likazidi kuenea na idadi ya waumini huko Yerusalemu ikaongezeka zaidi, na kundi kubwa la makuhani wakaipokea imani.
8A Szczepan będąc pełen wiary i mocy, czynił cuda i znamiona wielkie między ludem.
8Mungu alimjalia Stefano neema tele, akampa nguvu nyingi hata akawa anatenda miujiza na maajabu kati ya watu.
9I powstali niektórzy z tych, którzy byli z bóżnicy, którą zowią Libertynów i Cyrenejczyków, i Aleksandryjanów, i tych, którzy byli z Cylicyi i z Azyi, gadając z Szczepanem.
9Lakini watu fulani wakatokea ili wabishane na Stefano. Baadhi ya watu hao walikuwa wa sunagogi moja lililoitwa "Sunagogi la Watu Huru", nao walitoka Kurene na Aleksandria; wengine walitoka Kilikia na Asia.
10Lecz nie mogli odporu dać mądrości i duchowi, który mówił.
10Lakini hawakuweza kumshinda kwa sababu ya hekima yake na kwa sababu ya yule Roho aliyeongoza maneno yake.
11Tedy naprawili mężów, którzy powiedzieli: Myśmy go słyszeli mówiącego słowa bluźniercze przeciwko Mojżeszowi i przeciwko Bogu.
11Kwa hiyo waliwahonga watu kadhaa waseme: "Tumemsikia Stefano akisema maneno ya kumkashifu Mose na kumkashifu Mungu."
12A tak wzruszyli lud i starszych, i nauczonych w Piśmie; a powstawszy, porwali go i przywiedli do rady.
12Kwa namna hiyo, waliwachochea watu, wazee na walimu wa Sheria. Basi, wakamjia Stefano, wakamkamata na kumleta mbele ya Baraza kuu.
13I stawili fałszywych świadków, którzy rzekli: Ten człowiek nie przestaje mówić słów bluźnierczych przeciwko temu świętemu miejscu i zakonowi.
13Walileta Barazani mashahidi wa uongo ambao walisema, "Mtu huyu haachi kamwe kusema maneno ya kupakashifu mahali hapa patakatifu na Sheria ya Mose.
14Albowiemeśmy go słyszeli mówiącego: Iż ten Jezus Nazareóski zburzy to miejsce i odmieni ustawy, które nam podał Mojżesz.
14Kwa maana tulikwisha msikia akisema eti huyo Yesu wa Nazareti atapaharibu kabisa mahali hapa na kufutilia mbali desturi zile tulizopokea kutoka kwa Mose."
15A patrząc na niego pilnie oni wszyscy, którzy siedzieli w radzie, widzieli oblicze jego jako oblicze anielskie.
15Wote waliokuwa katika kile kikao cha Baraza walimkodolea macho Stefano, wakauona uso wake umekuwa kama wa malaika.