Polish

Swahili: New Testament

Galatians

1

1Paweł, Apostoł (nie od ludzi, ani przez człowieka, ale przez Jezusa Chrystusa i Boga Ojca, który go wzbudził od umarłych;)
1Mimi Paulo mtume,
2I wszyscy bracia, którzy są ze mną, zborom Galackim.
2na ndugu wote walio pamoja nami, tunayaandikia makanisa yaliyoko Galatia. Mimi nimepata kuwa mtume si kutokana na mamlaka ya binadamu, wala si kwa nguvu ya mtu, bali kwa uwezo wa Yesu Kristo na wa Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka wafu.
3Łaska wam i pokój niech będzie od Boga Ojca i Pana naszego, Jezusa Chrystusa.
3Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
4Który wydał samego siebie za grzechy nasze, aby nas wyrwał z teraźniejszego wieku złego według woli Boga i Ojca naszego;
4Kristo alijitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na mapenzi ya Mungu wetu na Baba, ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu mbaya wa sasa.
5Któremu niech będzie chwała na wieki wieków. Amen.
5Kwake yeye uwe utukufu milele! Amina.
6Dziwuję się, iż tak prędko dacie się przenosić od tego, który was powołał ku łasce Chrystusowej, do inszej Ewangielii;
6Nashangaa kwamba muda mfupi tu umepita, nanyi mnamwasi yule aliyewaita kwa neema ya Kristo, mkafuata Habari Njema ya namna nyingine.
7Która nie jest inszą; tylko niektórzy są, co was turbują i chcą wywrócić Ewangieliję Chrystusową.
7Lakini hakuna "Habari Njema" nyingine. Ukweli ni kwamba wako watu wanaowavurugeni, watu wanaotaka kuipotosha Habari Njema ya Kristo.
8Ale choćbyśmy i my, albo Anioł z nieba opowiadał wam Ewangieliję mimo tę, którąśmy wam opowiadali, niech będzie przeklęty.
8Lakini, hata kama mmoja wetu au malaika kutoka mbinguni, atawahubirieni Habari Njema tofauti na ile tuliyowahubirieni sisi, basi huyo na alaaniwe!
9Jakośmy przedtem powiedzieli i teraz znowu mówię: Jeźliby wam kto inną Ewangieliję opowiadał mimo tę, którąście przyjęli, niech będzie przeklęty.
9Tulikwisha sema, na sasa nasema tena: kama mtu yeyote anawahubirieni Habari Njema ya aina nyingine, tofauti na ile mliyokwisha pokea, huyo na alaaniwe!
10Albowiem terazże do ludzi was namawiam, czyli do Boga? Albo szukamli, abym się podobał ludziom? Zaiste, jeźlibym się jeszcze ludziom chciał podobać, nie byłbym sługą Chrystusowym.
10Sasa nataka kibali cha nani: cha binadamu, ama cha Mungu? Au je, nataka kuwapendeza watu? Kama ningefanya hivyo, mimi singekuwa kamwe mtumishi wa Kristo.
11A oznajmuję wam bracia! iż Ewangielija, która jest opowiadana ode mnie, nie jest według człowieka.
11Ndugu, napenda mfahamu kwamba ile Habari Njema niliyoihubiri si ujumbe wa kibinadamu.
12Albowiem ja anim jej wziął, anim się jej nauczył od człowieka, ale przez objawienie Jezusa Chrystusa.
12Wala mimi sikuipokea kutoka kwa binadamu, wala sikufundishwa na mtu. Yesu Kristo mwenyewe ndiye aliyenifunulia.
13Boście słyszeli o mojem obcowaniu niekiedy w Żydostwie, żem nader prześladował zbór Boży i burzyłem go;
13Bila shaka mlikwisha sikia jinsi nilivyokuwa ninaishi zamani kwa kuzingatia dini ya Kiyahudi, na jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kupita kiasi na kutaka kuliharibu kabisa.
14I postępowałem w Żydostwie nad wiele rówieśników moich w narodzie moim, będąc nader gorliwym miłośnikiem ustaw moich ojczystych.
14Naam, mimi niliwashinda wengi wa wananchi wenzangu wa rika langu katika kuizingatia dini ya Kiyahudi, nikajitahidi sana kuyashika mapokeo ya wazee wetu.
15Ale gdy się upodobało Bogu, który mię odłączył z żywota matki mojej, i powołał z łaski swojej,
15Lakini Mungu, kwa neema yake, alikuwa ameniteua hata kabla sijazaliwa, akaniita nimtumikie.
16Aby objawił Syna swego we mnie, abym go opowiadał między poganami, wnetże nie radziłem się ciała i krwi;
16Mara tu alipoamua kunifunulia Mwanae kusudi niihubiri Habari Njema yake kwa watu wa mataifa mengine, bila kutafuta maoni ya binadamu,
17Anim się wrócił do Jeruzalemu, do tych, którzy przede mną byli Apostołami, alem szedł do Arabii i wróciłem się zasię do Damaszku.
17na bila kwenda kwanza Yerusalemu kwa wale waliopata kuwa mitume kabla yangu, nilikwenda kwanza Arabia, kisha nikarudi tena Damasko.
18Potem po trzech latach wstąpiłem do Jeruzalemu, abym się ujrzał z Piotrem; i mieszkałem u niego piętnaście dni.
18Ilikuwa tu baada ya miaka mitatu, ndipo nilipokwenda Yerusalemu kuonana na Kefa; nilikaa kwake siku kumi na tano.
19A inszegom z Apostołów nie widział, oprócz Jakóba, brata Paóskiego.
19Lakini sikuwaona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
20A co wam piszę, oto się przed Bogiem oświadczam, żeć nie kłamię.
20Haya ninayowaandikieni, Mungu anajua; sisemi uongo.
21Zatemem przyszedł do krain Syryi i Cylicyi;
21Baadaye nilikwenda katika tarafa za Siria na Kilikia.
22A byłem nieznajomym z twarzy zborom żydowskim, które są w Chrystusie;
22Wakati huo, mimi binafsi sikujulikana kwa jumuiya za Wakristo kule Yudea.
23Lecz tylko byli usłyszeli, iż ten, który prześladował nas niekiedy, teraz opowiada wiarę, którą przedtem burzył.
23Walichokuwa wanajua ni kile tu walichosikia: "Mtu yule aliyekuwa akitutesa hapo awali, sasa anaihubiri imani ileile aliyokuwa anajaribu kuiangamiza."
24I chwalili Boga ze mnie.
24Basi, wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.